Leo wakati mekaa sehem mida ya mchana pembeni yangu kuna baba mzee mtu mzima. Asa akapita kijana mmoja wa kiume amevaa kaptura fupi kama chupi alaf juu akavalia na taiti ambayo inaonesha ndani alaf chini akapiga bonge la buti kama yale mabuti wanaovaaga wazungu kipindi cha baridi 😂 mzee alianza kumtazama yule kijana toka yupo mbali mpaka akapita 😂 yule kijana alivotokomea mzee akatoa bonge la sonyo alaf akasema "I HATE THIS GENERATION" hii kauli ilinifanya ncheke sana alaf ikanifikirisha. Hivi kwanini wazee wengi wanachukia hiki kizazi? Hivi mkikiona hiki kizazi cha sasa na mambo wanayofanya nini hasa huwajia akilini mwenu?