Hivi WCB huwa wana mpango gani na LAVALAVA?

screpa

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2015
Posts
10,857
Reaction score
15,866
Huyu jamaa licha ya watu kusema ana gundu ila mimi naona sio gundu tu, ni kwamba menejimenti yake pia haimpush vile inavyopaswa. Nimeshuhudia mara nyingi Mbosso/Zuchu na boss mwenyewe wakiandaliwa zinduzi mbalimbali za Album/EP kwa gharama kubwa, huku wakipewa promo kubwa na Wasafi Tv/Redio bila kusahau machawa wao lakini sikumbuki kama Lavalava amewahi kufanyiwa hivi. Hata ukikakaa kwenye TV yao nyimbo za Boss, Mbosso na Zuchu zinachezwa sana kuanzia mpya hadi za zamani, lakini ni nadra kuona nyimbo za Lavalava. Na si kwamba Lavalava hatoi ngoma kali, ana nyimbo nzuri nyingi tu. Je, wana mpango gani na huyu mtu pale WCB mbona anaishi kama mtoto yatima?
 
Jambo hilo liko sehemu zote ata kwenye maisha kuna baadhi ya familia baadhi ya watoto hupewa kipaumbele kuliko wengine.

Lavalava ana kipaji labda ni bahati au namna anajiweka
Wampe promo analopewa Zuchu/Mbosso, asipoenda mjini nitaamini kweli riziki yake haipo kwenye muziki atafute kazi nyingine
 
Lava kinamsumbua ameshindwa kutengeneza hitsong, ana nyimbo kali sana ila bado hajapata hitsong.

Mwaka unaokuja ni wa project zake na dogo mpya wanaetaka mtoa.
Hata za kwake zikipromotiwa zinakuwa hitsongs; ngoma kama Inatosha,Ng'aring'ari na Desh Desh hizi zote zingepangiwa mikakati mizuri ni hitsongs, ni ngoma kali
 
Hata za kwake zikipromotiwa zinakuwa hitsongs; ngoma kama Inatosha,Ng'aring'ari na Desh Desh hizi zote zingepangiwa mikakati mizuri ni hitsongs, ni ngoma kali
Bro hizo ni ngoma kali ila sio hitsong, kupata hitsong kwa promotion ni kazi kubwa sana hata Mondi mwenyewe hawezi.
Hitsong ni kama ngekewa kuna watu zinawakubali tu, ila pia inabidi uwe unajua kutengeneza hit sio muziki mzuri tuuu.
 
Bro hizo ni ngoma kali ila sio hitsong, kupata hitsong kwa promotion ni kazi kubwa sana hata Mondi mwenyewe hawezi.
Hitsong ni kama ngekewa kuna watu zinawakubali tu, ila pia inabidi uwe unajua kutengeneza hit sio muziki mzuri tuuu.
Kwa mfano kwenye ep ya Mbosso hitsong ni ipi?
 
Je zisingeboostiwa na promo zingekuwa hits? Hiyo yataniuwa hadi Baunsa wa Diamond kaifanyia challenge ya kucheza[emoji16][emoji16][emoji16]
Yes promotion ni muhimu ila kwanza lazima utengeneze hitsong bila hivyo utatumia nguvu nyingi na nyimbo haitoenda. Kuna nyimbo za diamond anatoa na zinabuma pamoja na investment kubwa ya promotion.
 
Yes promotion ni muhimu ila kwanza lazima utengeneze hitsong bila hivyo utatumia nguvu nyingi na nyimbo haitoenda. Kuna nyimbo za diamond anatoa na zinabuma pamoja na investment kubwa ya promotion.
Sawa, kwahiyo Lavalava inabidi asubiri hadi apate hitsong ndo tumfanyie promo na zinduzi ya EP auvipi?[emoji1][emoji1]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…