Hivi wenzangu huwa mnawezaje kupiga "mizinga" kuomba omba

Mwanga Lutila

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2016
Posts
4,208
Reaction score
14,143
Hii tabia binafsi imenishinda kabisa hata kama niwe na shida gani.

Labda nikope

Lakini utakuta mwingine hana aibu, popote pale hata mtu ambae hamjui " mwanangu una elfu tatu karibu hapo..."

Au hata bar " mwanangu na Mimi moja basi"...

Hivi huo ujasiri mnapata wapi?

Achana na wale ombaomba wa barabarani.
 
Ni afadhali upige mzinga upewe kuliko ukaambiwa "sina broo" huwa naona umejiaibisha sana .
 
Noma sana!Ila usiogope hata Mungu tunampiga mizinga kila siku.πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
MKUU KUNA LEVELS UKIFIKIA HUWEZI KUPIGA MIZINGA(Hii inakuja automatically)...mf.tumekutana bar mimi ni mnywaji wa CP(captain morgan) naanzaje kukupiga mznga wa 50k
 
MKUU KUNA LEVELS UKIFIKIA HUWEZI KUPIGA MIZINGA(Hii inakuja automatically)...mf.tumekutana bar mimi ni mnywaji wa CP(captain morgan) naanzaje kukupiga mznga wa 50k
Kupiga mizinga ni kipaji.Wengine wanakufa huku wanatukutia moyoni tu.Ni uwezo fulani wa ajabu kama kutongoza tu.
 
Wengine siku hizi wanakuja pm wanakuomba buku tano au ten.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…