Habari ya wakati huu ndugu zangu.
Hili suala la mtu kulundikiwa dawa ukienda hospitali hasahasa sisi wa bima ni kwamba madaktari mnataka tupone kwa haraka au limekaa kibiashara zaidi.Niliwahi kwenda hospitali nilipewa dawa kama aina 3 hivi na zote ni antibiotics sijajua ni kubahatisha au ili mupige pesa tu.Hivi juzi kuna ndugu yangu alienda hospitali kapewa dawa ukizigoogle uses zake haziendani kabisa na tatizo analoumwa ili mradi tu zimeandikwa na pesa kwao zimeingia bila kujali sisi wanatujaza sumu mwilini.Tufikiriane katika hili hizi sumu tunazopeana ili mradi tu mmepiga pesa sio vizuri.
Nawasilisha