Hizi Bilioni 24.5 walizopokea Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa (TMA) zitatumikaje kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi?

Hizi Bilioni 24.5 walizopokea Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa (TMA) zitatumikaje kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi?

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Takriban siku 2 zilizopita Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilipokea msaada wa dola milioni 9 za Marekani (takriban shilingi bilioni 24.5) kwa ajili ya kuboresha huduma za hali ya hewa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TMA, Jaji Mshimbe Bakari, alitangaza msaada huo jijini Dar es Salaam ambapo alidokeza kuwa fedha hizo zitatumika kuimarisha miundombinu ili kufanikisha upatikanaji bora wa data za hali ya hewa.

Ukiangalia kwa umakini Dola Milioni 9 (Bilioni 24.5) ni pesa nyingi sana na hii inaonesha ni kwa kiasi gani Marekani imejikita katika kuhakikisha huduma za hali ya hewa Tanzania zimeboreshwa. Lakini je kwa nature ya taasisi zetu ambazo mara nyingi zimejaa rushwa na ukiritimba, je fedha hizo zitasaidia kweli mamlaka hiyo kutatua tatizo la mabadiliko ya tabia ya nchi?

Nauliza hivyo kwa sababu, katika kauli yake wakati anapokea pesa hizo mapema wiki hii, kauli ya Jaji Mshimbe Bakari ilikuwa kama haijajitosheleza. Jaji Bakari alidokeza tu kuwa ufadhili huo utaimarisha juhudi za kutoa taarifa za hali ya hewa za hali ya juu nchini na pia aliwaomba wananchi wasipuuze taarifa za TMA.

TMA.png

Hakuongelea namna ambavyo pesa hizo zitatumika including, kuweka mpango mkakati au kuorodhesha ni kitu gani ataweka kama kipaumbele.

Je fedha hizo zote zitasaidia kusaidia tatizo la mabadiliko ya tabia ya nchi, tatizo ambalo kwa sasa linasababisha mafuriko na kuongezeka kwa joto hapa Tanzania?

Soma pia: TMA: Mvua za El-Nino kuendelea hadi Aprili 2024

Haya ni maswali ambayo yanafaa kupatiwa majibu especially ukizingatia kwamba pesa hizo ni nyingi.

Nawasilisha!
 
Nadhani ujenzi wa miundombinu ya kumonitor phyisically na logically(software) wise ndiyo inacost...ila siyo zote zitatumika nyingine ni kwenye warsha,semina,makongamano,study tour etc
 
Misaada yote kutoka nje huwa inaishia kutangazwa tu lakini ilichofanya hatukioni

Ni kweli mkuu, wangetuambia hizo pesa wanazifanyia nini hasa ili tuwe na metrics za kufanya wawajibike!
 
Nadhani ujenzi wa miundombinu ya kumonitor phyisically na logically(software) wise ndiyo inacost...ila siyo zote zitatumika nyingine ni kwenye warsha,semina,makongamano,study tour etc

Umeiweka vyema. Nashangaa kwanini kwa upande wao hawajatupa mchanganuo!
 
International money laundering ndo hii sasa, kwa akili za kawaida marekanj anakupaje pesa nyingi ivyo bila kusoma proposal iliyo nyooka!?

Basi kama wanatoa tu mipesa ivyo bila kujua all steps money gone be spended basi marekani wenyewe wanaitaji kuombewa maana kule kwao kuna beggars wengi tu na wanashambuliwa mno na majanga kama mafuriko kule florida.

Basi kama wametoa mipesa ivyo bila kusoma na kuona ukweli wanachokisoma basi wanaakili mbovu sana awana uchungu na pesa zao.

Ila kwa kawaida nchi iliyo na uwezo mdogo wakupata taarifa kwa usahihi kama tz basi money laundering international inafanyika tuu maana media zenyewe aziaminiki amna media skuizi inayotoa taarifa za hakika kila siku hapa Tanzania kama ipo ikwapi??

Hatuna information ndo maana taarifa za kupikwa za kulaunder pesa ni rahisi mno kufanyika nchi iliyo na viongozi mbofumbofu kma hii.

🔪
 
Wakuu,

Takriban siku 2 zilizopita Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilipokea msaada wa dola milioni 9 za Marekani (takriban shilingi bilioni 24.5) kwa ajili ya kuboresha huduma za hali ya hewa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TMA, Jaji Mshimbe Bakari, alitangaza msaada huo jijini Dar es Salaam ambapo alidokeza kuwa fedha hizo zitatumika kuimarisha miundombinu ili kufanikisha upatikanaji bora wa data za hali ya hewa.

Ukiangalia kwa umakini Dola Milioni 9 (Bilioni 24.5) ni pesa nyingi sana na hii inaonesha ni kwa kiasi gani Marekani imejikita katika kuhakikisha huduma za hali ya hewa Tanzania zimeboreshwa. Lakini je kwa nature ya taasisi zetu ambazo mara nyingi zimejaa rushwa na ukiritimba, je fedha hizo zitasaidia kweli mamlaka hiyo kutatua tatizo la mabadiliko ya tabia ya nchi?

Nauliza hivyo kwa sababu, katika kauli yake wakati anapokea pesa hizo mapema wiki hii, kauli ya Jaji Mshimbe Bakari ilikuwa kama haijajitosheleza. Jaji Bakari alidokeza tu kuwa ufadhili huo utaimarisha juhudi za kutoa taarifa za hali ya hewa za hali ya juu nchini na pia aliwaomba wananchi wasipuuze taarifa za TMA.


Hakuongelea namna ambavyo pesa hizo zitatumika including, kuweka mpango mkakati au kuorodhesha ni kitu gani ataweka kama kipaumbele.

Je fedha hizo zote zitasaidia kusaidia tatizo la mabadiliko ya tabia ya nchi, tatizo ambalo kwa sasa linasababisha mafuriko na kuongezeka kwa joto hapa Tanzania?

Soma pia: TMA: Mvua za El-Nino kuendelea hadi Aprili 2024

Haya ni maswali ambayo yanafaa kupatiwa majibu especially ukizingatia kwamba pesa hizo ni nyingi.

Nawasilisha!
Fanya kazi yako usilo na elimu nalo liache halikuhusu
 
Back
Top Bottom