NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,587
- 13,425
Kipa huyu mwenye umri wa miaka 29, jina lake ni Jefferson Luis Szerban de Oliveira Junior ana urefu wa mita 1.9 na kabla ya kujiunga na Simba alikuwa akiitumikia Resende FC ambayo inashiriki Ligi Daraja la nne, Brazil.
Hata hivyo, tangu aliposajiliwa na Resende mwaka 2017 muda mwingi alikuwa akitolewa kwa mkopo kwenda timu mbalimbali hadi kufikia hatua ya kutua Simba.
Luis ametolewa kwa mkopo kwenye jumla ya timu tano tofauti ambazo alikuwa kwa nusu msimu ama msimu mmoja pekee.
Timu hizo tano ambazo fundi huyu alipelekwa kucheza kwa mkopo ni pamoja na Athletic, Itabaiana, Volta Redonda, SC Aymores na Itabirito FC-MG.
Kwa msimu uliopita akiwa na Resende, kipa huyu amecheza mechi 21 za michuano yote akaruhusu mabao 35 na akamaliza mechi tatu bila ya nyavu zake kutikisika.
Je ataweza kuondoa utawala wa Diara??
Hata hivyo, tangu aliposajiliwa na Resende mwaka 2017 muda mwingi alikuwa akitolewa kwa mkopo kwenda timu mbalimbali hadi kufikia hatua ya kutua Simba.
Luis ametolewa kwa mkopo kwenye jumla ya timu tano tofauti ambazo alikuwa kwa nusu msimu ama msimu mmoja pekee.
Timu hizo tano ambazo fundi huyu alipelekwa kucheza kwa mkopo ni pamoja na Athletic, Itabaiana, Volta Redonda, SC Aymores na Itabirito FC-MG.
Kwa msimu uliopita akiwa na Resende, kipa huyu amecheza mechi 21 za michuano yote akaruhusu mabao 35 na akamaliza mechi tatu bila ya nyavu zake kutikisika.
Je ataweza kuondoa utawala wa Diara??