Hizi ndizo sababu? Wakaka inawahusu

Hizi ndizo sababu? Wakaka inawahusu

Tausi Mzalendo

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2010
Posts
1,470
Reaction score
722
KWA NINI WANAUME WENGI SIKU HIZI WANAKWEPA KUOA
1. Kujitambulisha ukweni. Hapo utatakiwa uende kijijini alikozaliwa mkeo
mtarajiwa ukajitambulishe huko. Kama mfano mkeo anatokea Mwanza, na mnaishi
Dar, andaa nauli ya watu wawili, malazi kwa siku mbili, na utagharamia
shuhuli hiyo ya utambulisho. We tenga 500,000. Hapo tuna assume mkeo
atajitegemea. Otherwise 800,000 itakutoka.
2. Kumtambulisha mkeo kwenu. Kama nyie nyumbani ni Arusha, utatakiwa
umpeleke huko Ngarenanyuki. Sio umlete hapo Tabata mlipopanga. Hapo sio
kwenu! Andaa nauli yako na atakaekusindikiza, nauli ya binti na mwenzie, na
gharama za vinywaji na chakula siku hiyo. Utahitaji kama 700,000
3. Kifuatacho ITV ni kuwaalika wakwe zako nyumbani. Uwatoe watu kama nane
Mwanza, uwalete Arusha. Wale, walale, wajisaidie, kwa gharama zako. We acha
ubishi, tenga 800,000 tu.
4. Kwani we wazazi wako wanajua unakooa? Sasa je? Wasafirishe kwenda
Mwanza! Watu watano. Utahitaji kuwa na 500,000. Beba pia ATM card yako, kuna
imejensi.
5. MAHARI ndio topic inayofuata sasa. Ukiwa mjanja, unganishia kwenye
hiyo safari hapo juu uue ndege wawili. Pamoja na hayo, itabidi ubebe
2,000,000.
6. Sasa kijana unaweza kumvisha mchumba wako pete. Nunua ya kawaida
kabisa ya dhahabu. 350,000. Tukio lenyewe la kumvisha pete unaweza ita
marafiki wawili watatu ukatumia 200,000. Au fanya sherehe kabisa. Mi simo
7. Oke, sasa unaweza kuitisha vikao vya harusi. Tengeneza kadi za mwaliko
wa kamati kwa 200,000, kikao cha kwanza gharama zote ni juu yako. Andaa
500,000. Swali la kwanza kwenye kikao: "We una shing ngapi?" Sema 1,000,000.
8. Utahitaji 100,000 ya sms na simu kukumbushia michango. (Shukuru Mungu
kuna cheka time)
9. Wakati vikao vinaendelea, utatuma 200,000 kwa m-pesa ili mambo ya
kimila yaendelee kule nyumbani. We unaelewa
10. "Darling, sasa mi kwenye kitchen party ntavaa nini?" 300,000!
11. "Darling, kuna mahali nimeona gauni zuri la send." 400,000!
12. "Baby, rafiki yangu alinunua gauni la harusi China yani lilimpende..."
700,000!
13. Wakati huo wewe mwenyewe hujajua utavaa nini, hujanunua pete za
harusi, hujamvalisha best man na mkewe. Tuseme unahitaji kama 1,500,000
maana utalia lia sana. Kumbuka, gharama hizi huchangiwi na kamati. Wala
hutarudishiwa.
14. Siku ya send off lazma uende Mwanza. Utaenda mwenyewe? Ndugu wawili
watatu na mshenga 600,000. Kwenye send off utatakiwa kutoa sijui blanketi la
bibi, vitenge vya mashangazi, na vikorokoro kibao. Nunua hivyo vitu 300,000
uende navyo ili kupunguza gharama. Beba 200,000 za wale mashangazi
watakaoibuka ghafla!
15. Mshonee baba mkwe suti 100,000 mama mkwe yeye atavaa gauni la 50,000.
16. Fotokopi hiyo hapo juu (namba 15) kwa wazazi wako. 150,000
17. Watu watakaopenda kuvaa sare wajitegemee! Mimi sina hela! Ila
utavishonea nguo vile vitoto kwa 80,000.
18. Siku mbili kabla ya harusi, utaanza kupokea wageni. Unatakiwa
uwatafutie malazi na chakula. Kwa ujumla utahitaji kama 500,000
19. Jioni watoe auti mashemeji zako ambao hawajawahi kufika Dar
ukawanunulie bia ili wakuone wa maana. 200,000
20. Siku ya harusi bibi harusi na mwenzie na watoto na ma maids watatakiwa
wakapambwe saluni. 200,000
21. We na mwenzio mtaenda kunyoa hapo kwa nanii. Ndevu na nywele na black
kibishi 40,000
22. Siku ya harusi beba sadaka 10,000. Wakati huo umeshamtuma kijana
akakulipie hoteli mtakayofikia baada ya harusi. Kamati haitoi hela hiyo, so
utalipa malazi ya siku mbili 200,000
23. Kama mtaenda honeymoon sehemu yoyote nzuri nzuri nje ya mji, si chini
ya 800,000 kwa angalau siku 5.
24. Wakati uko huko honeymoon, huna hata kumi, mwanakamati mmoja ambae
hakuchanga anakupigia simu " Sasa tunavunja lini kamati?" Pesa yote
iliyochangwa ilitumika kwenye harusi, sasa gharama za kuvunja kamati ni za
nani?? 500,000!
25. SASA MNAANZA MAISHA YA UNYUMBA. 14,180,000 poorer.

KAAZI KWELI KWELI!
Sasa nini kifanyike kama hizo ndizo sababu?
 
kupunguziana cost na pamoja na kutokuoa mwanamke ambaye yupo mbali na familia yako..

Kwenye bold ina maana kuoana kabila moja au ?
Kupunguzianaje costs mkuu? Ina maana mwanamke achangia mahari yake au kwenye maeneo gani? Mimi sitakubali kujinunulia nguo ya harusi lol..itabidi mchumba anunue.Vikao vya harusi gharama ni zake pia maana nasi kwetu vitakuwepo vya send off!Gharama siyo upande wa bwana tu hata kwetu zipo.
 
Unachosema Tausi Mzalendo kina ukweli kwa sehemu, gharama zimekuwa kubwa ingawa sidhani kama zinafika huko! Kwa upande wangu naona ni vzr kijana kuoa kama amempata mwenziye. Ni vzr zaidi wadada kuwa considerable kwa kujaribu kupunguza gharama zisizo za lazima kwenye hayo maandalizi, na kuacha kufanya masherehe makubwa kwa kuiga iga sherehe za wenzao, badala ya kufanya kitu kilicho ndani ya uwezo wenu!

Lakini nafikiri pia kuna sababu nyingine nyingi zinazowafanya vijana wasioe siku hizi ikiwemo kukwepa majukumu, kuchungwa, kulindwa, kufuatiliwa, kuwa tabia ya kuwa na wasichana zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja, commitment, wengine hupendwa kutunzwa na wadada, kukosa kazi, kukosa kipato, frustration, sababu za kibailojia na mengineyo mengi!
 
Mwanaume ambaye hana uwezo hatakiwi kuoa hayo mbona yanajulikana toka zamani, sasa kipi kipya.
 
Gharama tu ndio sababu ya kutoooa au watu nao akili zao zimekaa kushoto kulia? Kwani lazima uhakikishe mji mzima unajua unaoa?
 
izo ni gharama za harusi sio ndoa bwana
mwenye shida ya ndoa anione mimi nahamia hivohivo bila harusi
sina makuu mie

Smile , basi siku zote hizi mie najua tayari u-ndoani !
Kumbe bado !
Sasa leo ndiyo nimeishajua sababu ya vituko na vibwekwa vyako coz ni nini .
Kumbe tatizo lako si la India, ukishapatiwa dawa muafack acha kukosea kunywa sumu, hata maji yasiochemshwa huwezi kosea ukayanywa.
 
Smile , basi siku zote hizi mie najua tayari u-ndoani !
Kumbe bado !
Sasa leo ndiyo nimeishajua sababu ya vituko na vibwekwa vyako coz ni nini .
Kumbe tatizo lako si la India, ukishapatiwa dawa muafack acha kukosea kunywa sumu, hata maji yasiochemshwa huwezi kosea ukayanywa.
ndo ivo bwana sina ndoa.sasa unanisaidiaje?
 
Kwenye bold ina maana kuoana kabila moja au ?
Kupunguzianaje costs mkuu? Ina maana mwanamke achangia mahari yake au kwenye maeneo gani? Mimi sitakubali kujinunulia nguo ya harusi lol..itabidi mchumba anunue.Vikao vya harusi gharama ni zake pia maana nasi kwetu vitakuwepo vya send off!Gharama siyo upande wa bwana tu hata kwetu zipo.

kabila moja au mkoa jirani na wakwenu pili kuhusu kushare cost nizile za kuwatunza ndugu zake na wako kipindi cha harusi kuliko kumuachia mtu mmoja na hilo gauni la harusi kwanini usijinunulie kumpunguzi mmeo gharama zisizokuwa na ulazima kwake..

hasa wanaongoza kwa kutolewa gharama na upande mmoja ni pale mwanamke asipokuwa na kazi ndipo inapokuwa kazi..
 
kabila moja au mkoa jirani na wakwenu pili kuhusu kushare cost nizile za kuwatunza ndugu zake na wako kipindi cha harusi kuliko kumuachia mtu mmoja na hilo gauni la harusi kwanini usijinunulie kumpunguzi mmeo gharama zisizokuwa na ulazima kwake..

hasa wanaongoza kwa kutolewa gharama na upande mmoja ni pale mwanamke asipokuwa na kazi ndipo inapokuwa kazi..

hahhah... gauni ya harusi sinunui hata kwa kiboko!
Halafu baadhi ya gharama mwanaume anajitakia mwenyewe - kuwatoa mashemeji wakajinafasi - anatafta sifa za kijinga mwenyewe.
Malazi na chakula kwa wageni na wakwe mbona kamati inatenga fungu kutoka kwenye michango.
Mi ningeshauri, wahusika wenyewe waamue aina ya sherehe wanayoitaka na kuweka kiwango chini.Tatizo waoaji wanatafuta mashindano wenyewe kwa wenyewe.
 
Mie bana nishamwambia mtu wangu sihitaji mamilolongo ya sherehe na magara kibao kwa ajili tu ya kuoana,
Km ana hela agaramikie km hana familia yangu ikishaniaga,siku ya ndoa tukishatoka kanisan tunakua tumeandaa kitafrija tu kidogo na ndugu wa karibu na marafiki zetu tule na kunywa na kupongezana hata pale hm au hotelini kitu cha masaa 2 tu tuwe tushamaliza twende zetu hane muni basi na kila mtu arudi makwao.

Haya mambo yakupeana stress na madeni kwa ajili ya siku moja wala sinaga mzuka nayo kbs!.
 
Mie bana nishamwambia mtu wangu sihitaji mamilolongo ya sherehe na magara kibao kwa ajili tu ya kuoana,
Km ana hela agaramikie km hana familia yangu ikishaniaga,siku ya ndoa tukishatoka kanisan tunakua tumeandaa kitafrija tu kidogo na ndugu wa karibu na marafiki zetu tule na kunywa na kupongezana hata pale hm au hotelini kitu cha masaa 2 tu tuwe tushamaliza twende zetu hane muni basi na kila mtu arudi makwao.

Haya mambo yakupeana stress na madeni kwa ajili ya siku moja wala sinaga mzuka nayo kbs!.
rejao akufanyii tena harusi?
 
Kwa kweli hii mada na yenyewe inaweza kuwa sababu watu kwanini wasije kuamua kuoa maana ukipiga mahesabu hayo yote? Laiti watu wasingejua u naenda tu na flow...
 
gharama tu ndio sababu ya kutoooa au watu nao akili zao zimekaa kushoto kulia? Kwani lazima uhakikishe mji mzima unajua unaoa?

ukweli umedhihiri ktk maneno yako haya, mwenye kuuhitaji na aufanyie kazi, kila mmoja ni vyema akaishi awezavyo, na si apendavyo!
 
mimi jamani marafiki ndugu na jaa samahani nataka nizoeleke kwd ndugu, halafu awe jirani yangu wa pale maskani nadhani hyo figure ita pungua
 
Back
Top Bottom