Hizi Net Kwenye Majengo ya Gorofa Huwa Zinasaidia Nini?

How? Kama ni usalama kwani ni ngazi hizo?
Ngazi ni za kupandia, haziwezi kuzuia vitu kama nondo, tofali mbao nk zisiweze kudondoka, hivyo kwa usalama wa wapita njia au wanaokuwa njiani lazima waweke nyavu na pia inazuia hata takataka kama vumbi kusambaa hovyo.

Ndio maana mda wote unapokuwa eneo la ujenzi kama hilo hata kama sio fundi unatakiwa kuvaa kofia ngumu.
 
Kuzuia chembe chembe zisidondoke chini na kuleta usumbufu; wakati mwingine utumika kwa ajili ya usalama kwa mjenzi
 
1.Usalama.
Kuzuia vitu vinavyohusiana na ujenzi, vikidondoka viwe eneo moja visiumize watu wa chini na wapita njia.

2.kuzuia uoga (phobia)
Kila binadamu ana uwezo wake wa kuhandle vitu, mfano kadri jengo linavyozidi kuwa refu, mwingine huweza kupata kuzunguzungu akiwa umbali wa floor fulani hivyo akiwa ndani ya uzio wa net inasaidia kumpa uwezo wa kujiamini na kufanya shughuli zake vizuri

3.Kuongeza umakini
Inasaidia kudeal na kazi zako husika kuliko kuangalia vitu visivyokuhusu nje hasa ukizingatia mtu upo juu zaidi.

4.Kuficha ujuzi.
Kila kazi Zina utaalamu wake, hivyo si vyema mtu kucopy na kupaste mambo, mfano: ramani, michoro, shepu ni design za mijengo mbalimbali bila ruhusa.
Siyo mtu anazoom jengo lako na kwenda kufanya habari zake kiholela.

5.Heshima na ustaarabu.
Jengo linaweza kujengwa uswazi /uswahilini, ambako nyumba nyingi ni duni huku vyoo na mabafu vikiwa ni vya nje tena havijafunikwa chochote juu. hivyo net husaidia watu wengine kufanya mambo yao kwa uhuru.

Yapo mengi ya kitaalamu zaidi , ila kamata hizi nyepesi nyepesi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…