Mimi siyo mtu wa Pwani, kwetu ni Mahoma, Old Moshi, Kilimanjaro. Kuna mtu niliona hapa Jukwaani anatumia jina la Kikarara, Kikarara na Mahoma ni vijiji vilivyopakana. Kama jina lake linauhusiano na Kikarara ni lazima atakuwa anapajua kwa Mozee kwasababu hapo ni sehemu maarufu sana kwa kuuza mbege nzuri. Ngoja nimMention.
Kikarara78
Turudi kwenye mada, unataka kuniambia Tanzania ya leo ni sawa na ya 1999? Kwanini mnakosa shukrani hivyo ndugu zangu? Kuna siku niliona Dr. Slaa akijitetea kwamba ameshindwa kutembea wilaya zote Tanzania kwasababu ya ukubwa wa Tanzania sasa jamani kama mtu kutembea tu imekuwa ngumu ndiyo itawezekana kila shule iwe kama Ubungo National Housing Primary School? Acheni hizo bana. Mnaboa.