Hizi St.Kayumba ni tatizo

Hizi St.Kayumba ni tatizo

Joined
Aug 27, 2013
Posts
40
Reaction score
8
Nina mdogo wangu kamaliza form four na kapata ziro kipindi chote nilichokaa nae nimejaribu kumchunguza hana kitu kabisa kichwani hadi nimekubali kuwa ziro aliyopata inamstahili kabisa sasa kituko kiko hapa hajui hata afanye nini nimejaribu kumuuliza anasema wala hajui mi nimtafutie chochoote sasa kwa elimu yake naweza kumpeleka coz gani isiyoitaji elimu ya kutosha tena ya muda mfupi
 
Kama yeye sifuriii,jaribu wewe kumuangalia anaweza kufit wap,,ilo jibu lake "chochote" ni hatar sana
 
Umeona mkuu yaani nimekaa nae sana nikimdadisi baadhi ya ndugu wanashauri arudie shule lkn kwangu mi naona itakuwa nikupoteza muda tu mtu kasoma miaka minne hata aina za maneno hajui ni nini hata ukimuuliza Waziri Mkuu ni nani hajui sasa kweli hapo si kazi ipo nawaza sijui nimfanyie nini huyu.
 
According to Socrates huyo ni IRON.
Anahitaji manual works, so itakuwa vizuri ukimpeleka veta hasa ufundi wa computer nahisi atakuwa interested nao, akizingua mpeleke akasomee muziki au uselemala ataweza tu, trust me.
 
Nina mdogo wangu kamaliza form four na kapata ziro kipindi chote nilichokaa nae nimejaribu kumchunguza hana kitu kabisa kichwani hadi nimekubali kuwa ziro aliyopata inamstahili kabisa sasa kituko kiko hapa hajui hata afanye nini nimejaribu kumuuliza anasema wala hajui mi nimtafutie chochoote sasa kwa elimu yake naweza kumpeleka coz gani isiyoitaji elimu ya kutosha tena ya muda mfupi


Ina maana miaka yote alipokua shule ulimuacha tu apashe viti joto,leo ndio unagundua kua alikua msindikizaji.Nakushauri umpeleke chuo chochote kinachotambulika na serikali asomee ufundi na udereva wa magari makubwa.Ukimwacha tu hapo nyumbani utashangaa anaanza kutumia jani la mmea korofi akishushia na viroba,jicho nyanya,mlegezo na ataanza kubana pua.
 
According to Socrates huyo ni IRON.
Anahitaji manual works, so itakuwa vizuri ukimpeleka veta hasa ufundi wa computer nahisi atakuwa interested nao, akizingua mpeleke akasomee muziki au uselemala ataweza tu, trust me.

useremala niliwahi kuufikiria lakini ni wakike halafu nikahisi vitu kama hivi inabidi msomaji avipende mwenyewe huo ufundi wa computer nawweza kujaribu jee mkuu unaweza nisaidia veta wanaanza lini hizi course zao niweze kumchukulia form ama chuo chochote kinachotoa hayo mafunzo
 
Ina maana miaka yote alipokua shule ulimuacha tu apashe viti joto,leo ndio unagundua kua alikua msindikizaji.Nakushauri umpeleke chuo chochote kinachotambulika na serikali asomee ufundi na udereva wa magari makubwa.Ukimwacha tu hapo nyumbani

Ni wakike mkuu halafu sikuwa nakaa nae mimi alikuwa anakaa kijijini baada ya kufeli ndo nikamchukua mjini ili nijue nitamsaidiaje hapo ndio nilipogundua kuwa kichwa chake hakifanani na elimu yake ndio nipo naangaika nimsaidie vipi huyu dogo
 
useremala niliwahi kuufikiria lakini ni wakike halafu nikahisi vitu kama hivi inabidi msomaji avipende mwenyewe huo ufundi wa computer nawweza kujaribu jee mkuu unaweza nisaidia veta wanaanza lini hizi course zao niweze kumchukulia form ama chuo chochote kinachotoa hayo mafunzo

Nadhani itakuwa vema ukienda kwenye ofisi za veta za mkoa uliopo ili upate taarifa zote za muhim unazozihitaji.

Kitu kingine, jaribu kuwa naye friendly maana huwenda anakuogopa.
 
Muozeshe kwangu maana natafuta mke, joke. Mkuu kama waliposaidia wadau waliopita pia sio vibaya kama utaangaalia fani ya full secretarial course kwa maana inawasaidia sana watu hao na pia huwa rahisi kujiajiri au kuajiriwa ktk hizi internet cafe au stationaries pia nimegundua pia wanajifunza masomo mengi kama english course, book keeping, typing nk tena kwa bei nafuu zaidi. Pia kama utaona veta inamfaa kwako basi sio mbaya ukamtafutia fani ambayo ni rahisi kwake kujiajiri binafsi kwa kuajiriwa ni tatizo san
 
Nina mdogo wangu kamaliza form four na kapata ziro kipindi chote nilichokaa nae nimejaribu kumchunguza hana kitu kabisa kichwani hadi nimekubali kuwa ziro aliyopata inamstahili kabisa sasa kituko kiko hapa hajui hata afanye nini nimejaribu kumuuliza anasema wala hajui mi nimtafutie chochoote sasa kwa elimu yake naweza kumpeleka coz gani isiyoitaji elimu ya kutosha tena ya muda mfupi

Mkuu mwanachondogoro kwa sababu ni wa kike, na kwa kazi nyingine hata akisomea mfano ufundi computer bado unahitaji upeo zaidi na itamchukua muda hadi kuwa competent na kukubalika sokoni!

Kwa mtazamo wangu yeye bado anasaidika, unachotakiwa kufanya ni kumkalisha chini na maadam amekuachia ww umchagulie cha kufanya basi mjenge kwenye kusoma ufundi cherehani lengo likiwa ajue ushonaji katika nyanja pana lkn pia ukimweleza kuwa lengo la yeye kusomea hiyo ni wewe kuja kumpa mtaji kwa maana ya kuwa na cherehani zake let say 4, mashine ya kudarizi na mashine nyingine zenyemkuwezeshankakiwandankadogomka udhonaji na ufumaji masweta ili aje aajiri watu watakaomsaidia kufanya kazi ktk kakiwanda hako.

Nina imani katika soma yake ata cope na wenzie hata kupata wasaidizi baadae itakuwa sio issue.

Hakikisha akiwa chuo wewe unafanya mpango wa kusajiri hiyo sijui niite garments au tailoring mart kwajina lenye mvuto kwa biashara hiyo na ili ijulikane kisheria hivyo mtaweza hata kufanya kazi zinazohusiana na ushonaji, ufumaji nembo, masweta etc kwa taasisi na kampuni kubwa na hivyo kukuza kipato mara dufu!

ningeweza kukupa idea zaidi namna ya kufanya hii kazi ila ndo muda wa mwajiri huu naomba nimtendee haki!

unaweza kuni-pm au uliza swali ntakujibu hapahapa jamvini!
Asante
 
Last edited by a moderator:
jichange hata umfungulie m-pesa umfundishe kazi apate chake kufeli shule cyo kwamba hana ki2 kichwani
 
Nina mdogo wangu kamaliza form four na kapata ziro kipindi chote nilichokaa nae nimejaribu kumchunguza hana kitu kabisa kichwani hadi nimekubali kuwa ziro aliyopata inamstahili kabisa sasa kituko kiko hapa hajui hata afanye nini nimejaribu kumuuliza anasema wala hajui mi nimtafutie chochoote sasa kwa elimu yake naweza kumpeleka coz gani isiyoitaji elimu ya kutosha tena ya muda mfupi
ugwigwa go mbulu mininga mmatu,huu ni msemo wa kisukuma ukimaansha kusikia kwa kenge ni mpaka damu imtoke sikioni,ina mana wewe hukujua siku zote kuwa hizi siyo shule mpaka yamtokee mdogo wako,kama ulikwepa gharama kumpeleka shule nzuri saizi gharama ya kumsaidia ni kubwa mno na hutaiweza na maisha yake si rahisi yakaendeshwa na elimu tena mana hata yeye anajua hana akili kumbe tatzo lilikuwa shule.

hapo kama unafikiria biashara mpe na kama ataimudu sawa,ama akasome kozi zingine kama wadau wanavyoshauri lakini haziwezi sana kumtoa,labda sector za welding,umeme majumbani nk huko veta zaweza saidia kwa kiasi fulani.
 
Mkuu mwanachondogoro kwa sababu ni wa kike, na kwa kazi nyingine hata akisomea mfano ufundi computer bado unahitaji upeo zaidi na itamchukua muda hadi kuwa competent na kukubalika sokoni!

Kwa mtazamo wangu yeye bado anasaidika, unachotakiwa kufanya ni kumkalisha chini na maadam amekuachia ww umchagulie cha kufanya basi mjenge kwenye kusoma ufundi cherehani lengo likiwa ajue ushonaji katika nyanja pana lkn pia ukimweleza kuwa lengo la yeye kusomea hiyo ni wewe kuja kumpa mtaji kwa maana ya kuwa na cherehani zake let say 4, mashine ya kudarizi na mashine nyingine zenyemkuwezeshankakiwandankadogomka udhonaji na ufumaji masweta ili aje aajiri watu watakaomsaidia kufanya kazi ktk kakiwanda hako.

Nina imani katika soma yake ata cope na wenzie hata kupata wasaidizi baadae itakuwa sio issue.

Hakikisha akiwa chuo wewe unafanya mpango wa kusajiri hiyo sijui niite garments au tailoring mart kwajina lenye mvuto kwa biashara hiyo na ili ijulikane kisheria hivyo mtaweza hata kufanya kazi zinazohusiana na ushonaji, ufumaji nembo, masweta etc kwa taasisi na kampuni kubwa na hivyo kukuza kipato mara dufu!

ningeweza kukupa idea zaidi namna ya kufanya hii kazi ila ndo muda wa mwajiri huu naomba nimtendee haki!

unaweza kuni-pm au uliza swali ntakujibu hapahapa jamvini!
Asante
hapo inabidi mpe mtaji wa maana na apate mashine za kisasa zaidi ya chelehani,pia anaweza hata kumfungulia mgawahawa akawa mama lishe maana zinalipa sana kwa wamama
 
Hawa wapo wengi sana jamaa sio huyo tu.mi naona nafasi ya kusoma VETA anayo kwa kozi kama shelehani,saloon,upambaji,uundaaji wa vyakula kwa ajili ya sherehe/makongamano na zinginezo,ila inabidi asiwe tozi maana hataziweza.
 
Back
Top Bottom