Hizi status za WhatsApp balaa!

Simplicity.

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2013
Posts
2,636
Reaction score
1,662
Hivi WhatsApp mtu anatakiwa aweke status ya aina gani hasa kama ni mwenye staha?

Ni mimi tu ambaye labda siendi na mwendokasi au inakuwaje?

Nachungulia status ya mdada mmoja hapa inasomeka hivi "Kill them with success and bury them with a smile".

Tunaouwawa na mafanikio yake ni sisi sote ambao tupo kwenye contact book yake au kuna walengwa?

Ni kawaida na nyie mnakutana na hizi status wakuu? Hebu tupia moja kama kweli!
 
Mm naona kuna mtu anakua kalengwa haswaaaaaa
Maana status kama hiyo, mtu anaweka special kwa ajili ya mtu Fulani...kama ikiwa inakuhusu ndo utajua.... Lakn kusema hivyo haimaanishi na mm imenitokea ni research tu nimefanya kwa wa2
 
Mm naona kuna mtu anakua kalengwa haswaaaaaa
Maana status kama hiyo, mtu anaweka special kwa ajili ya mtu Fulani...kama ikiwa inakuhusu ndo utajua.... Lakn kusema hivyo haimaanishi na mm imenitokea ni research tu nimefanya kwa wa2

Sasa mkuu mimi huwa sielewi, mtu anaweka status kama hiyo, yupo chuo mwaka wa pilia anategemea boom, success gani sasa?
 
hahah kuna hii hapa!!!!!!
Kazi ya Moyo ni kusukuma damu nakupenda ni kihelehele chako. huku whatpp noma.
 
Kuna kajamaa itakuw kalimpiga kibuti sasa ndio kanafikishiwa ujumbe. Ukute huyo mdada keshanunua ka Paso basi ndio anajiona kama keshamaliza kila kitu...
 
Sasa mkuu mimi huwa sielewi, mtu anaweka status kama hiyo, yupo chuo mwaka wa pilia anategemea boom, success gani sasa?
Duh! Hiyo kama ww co mhusika haiwez ikakugusa....kama ww unahc inaweza kukuhusu lakn unaona kama haiji(non sense) yawekana kaiweka kwa ajili ya best yake mwingne na haimhusu yy
 
Status nyingine unaishia kucheka na kutikisa kichwa tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…