Elections 2010 'Hodhi' ya majimbo... Inakuwaje?

Elections 2010 'Hodhi' ya majimbo... Inakuwaje?

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2008
Posts
5,457
Reaction score
963
Inakuwaje mbunge ulalamike ati kuna watu wananyemelea jimbo lako! Kwani hilo jimbo umeliwekea "hatimiliki"? Nijuavyo mimi mtu anapopata ubunge, anadumu miaka mitano kisha uchaguzi unapowadia wananchi watapima na kuamua wamrudishe au wamuondoshe ili waweke mtu mwingine atakayewahudumia vema.Sasa wananchi watachagua vipi kama incumbent anang'ang'ania na kukataa ushindani? Nimeshaona hadi sasa wabunge kadhaa "wakilia" wanaingiliwa majimbo yao - mfano ni mama Anne Kilango Same Mashariki na Dr Zainab Gama - mbunge wa Kibaha.Badala ya kulialia kwanini msiache wananchi ( mabosi wenu) waamue wanamtaka nani?
Ndugu yangu kama mpiga kura je hii imekaaaje?..kwangu mimi imekaa vibaya sana!
 
Inakuwaje mbunge ulalamike ati kuna watu wananyemelea jimbo lako! Kwani hilo jimbo umeliwekea "hatimiliki"? Nijuavyo mimi mtu anapopata ubunge, anadumu miaka mitano kisha uchaguzi unapowadia wananchi watapima na kuamua wamrudishe au wamuondoshe ili waweke mtu mwingine atakayewahudumia vema.Sasa wananchi watachagua vipi kama incumbent anang'ang'ania na kukataa ushindani? Nimeshaona hadi sasa wabunge kadhaa "wakilia" wanaingiliwa majimbo yao - mfano ni mama Anne Kilango Same Mashariki na Dr Zainab Gama - mbunge wa Kibaha.Badala ya kulialia kwanini msiache wananchi ( mabosi wenu) waamue wanamtaka nani?
Ndugu yangu kaka mpga kura je hii imekaaaje?..kwangu mimi imekaa vibaya sana!

nadhani wanacholilia (kama tunaweza kuita hivyo) ni mbinu chafu za kuwanyima wananchi nafasi ya kuwachagua tena. Mbinu ambazo wakati mwingine kwa maoni yao zinapakana na vitendo vya uhalifu na ndio maana wanataka vyombo vya sheria vifuatilie. Sidhani kama kuna mtu ambaye atalalamika kama watu wanajitokeza kugombea katika mazingira mazuri.
 
nadhani wanacholilia (kama tunaweza kuita hivyo) ni mbinu chafu za kuwanyima wananchi nafasi ya kuwachagua tena. Mbinu ambazo wakati mwingine kwa maoni yao zinapakana na vitendo vya uhalifu na ndio maana wanataka vyombo vya sheria vifuatilie. Sidhani kama kuna mtu ambaye atalalamika kama watu wanajitokeza kugombea katika mazingira mazuri.

Mwanakijiji,
Mbinu walizoingilia madarakani akina Kilango na wenzake ndo hizo hizo ambazo zinatumiwa na wale wanaotangaza 'NIA' za kugombea majimbo hayo. Sijajua kwa nini hawa wabunge walio madarakani wanalia lia ovyo utadhani majimbo ni 'YAO'. Tatizo wanataka kuziba njia ambazo wao walipitia, ili wanaokuja wasipite hizo, wakati njia hizo ndio short cut za kuelekea kwenye unono.
 
What goes round comes round.. sidhani kuna mbunge hata mmoja anaweza kujigamba kuwa ati hakutumia mbinu "tainted" kama siyo "chafu" kuwalainisha wapiga kura haswa wale walio kwenye "vulnerability". Kila mbunge ama katoa chakula, au katoa chochote japo hata " kitochi" ili akumbukwe kwenye kura....Bila shaka wanaowania nao wanatumia mbinu ili waonekane kwa mpiga kura. Takrima ilishapigwa marufu kisheria lakini bado kuna vijitakrima vinaendelea pamoja na TAKUKURU kutoa onyo.

Labda ndugu zanguni MKJJ na wengineo tujadili ni vipi mbunge utaenda jimboni na maneno matupu uwavute wananchi waache mashamba yao na shughuli zao waje wakusikilize wewe na ahadi zako.

Ninatumia uzoefu wangu kwenye shughuli za kijamii huko vijijini.Ukienda hata kwenye utafiti angalau lazima u oganazi wananchi wapate japo ubwabwa na chai ya rangi ndipo wakusikilize na wakupe ushirikiano na hapo ni kwa manufaa yao- huendi kuwaomba kura wala kula!
 
Bado tuna mengi ya kusikia
Watuachie wananchi tuamue na wasitupangie
Siku zote wanatumia mbinu chafu mno!!!!!!!!!!!!!
Tuwe macho na uppuzi uliojaa ndani ya ahadi zao
 
Back
Top Bottom