Hodi hodi wana jf

Hodi hodi wana jf

LOGARITHM

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2010
Posts
974
Reaction score
475
Waheshimiwa Wana JF na wapenda maendeleo wote. Mimi ni mwanachama mupya kabisa nabisheni hodi. Nimeipenda hii forum na nimekuwa msomaji mzuri sana kwa muda mrefu. Sasa ni wakati wangu wa kujumuika kivitendo kama ilivyo wakati muafaka kwa ukombozi wa Tanzania yetu, kwa ajili yetu na vizazi vyetu vilivyopo na vijavyo. Naamini sawasawa na mawazo ya Balozi wa Ujerumani nchini kuwa Tanzania yenye neema kwa watu wake inawezekana mno ikiwa tu tutaweza kufanya mambo yaliyo sahihi.
 
Umeshatoa mchango wako wa fedha kwa CHADEMA? Kama uko Tanzania umejitokeza kusaidia kufanya kazi za CHADEMA kipindi hiki muhimu?
 
Karibu sana Logarithm.........nahisi utakuwa ni mtaalamu au unapenda sana hesabu.
 
Ndugu Katavi na wengine , nashukuru kwa ukaribisho wenu. Nimejiita jina hilo kwa kumbukumbu ya jinsi hesabu zilivyonishinda na zilivyonigaragaza enzi hizo. Lakini zile za kariakoo shimoni sio mbaya, hizo, naziweza!

Kawa mara nyingine tena, asanteni.
 
karibu sana log, wewe ni moja kati ya hesabu ambazo zilinisumbua sana form four ila nakukaribisha kwa moyo mkunjufu kabisa
 
Mimi ni mwanachama mupya kabisa nabisheni hodi.

Karibu sana. Kumbuka kupitia kwa makini sheria na kanuni za JF. Kila la heri katika ushiriki wako wa mada mbalimbali hapa JF.
 
karibu sana log, wewe ni moja kati ya hesabu ambazo zilinisumbua sana form four ila nakukaribisha kwa moyo mkunjufu kabisa

Duuh, wewe kweli LOG zilikusumbua mpaka umesahau hata huwa zinafundishwa kidato kipi, hesabu za LOG huwa zinafundishwa form two baada ya kusoma quadratic equations, exponents na indices. Anyway, labda nyie mlikuwa mnafuata syllabus tofauti. Ni maoni tu!
 
Back
Top Bottom