Hodi mi nasema hodi

JENDALUJEJE

Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
43
Reaction score
22
Hodi naipiga humu,JENDALUJEJE nasema,
:violin:Imeniingia hamu,Jukwaani kuja sema,
Mawazo mengi matamu,ya kumeza si kutema,
Hodi mi nasema hodi,ndio kwanza naingia.

Jamvini nasogelea,KARIBU naisubiri,
Kwa pupa sitoingia,subira yavuta heri,
Enyi mlotangulia,nasema SABALKHERI,
Hodi mi nasema hodi,ndio kwanza naingia.

Midomo mkifungua,tabasamu mkaweka,
:violin:Woga shaka nitavua,na imani nitaweka,
Ndugu mkinitambua,makazi nitayaweka,
HODI MI NASEMA HODI,NDIO KWAANZA..NAINGIA!
 
Karibu, lakini najiuliza swali hili,siku hizi hakuna jukwaa la utambulisho?Maana naona wageni wanapotea kila siku.
 
Karibu sana jamvini, jisikie uko nyumbani, wala usiwe na soni kumwaga yako maoni, nasema tena karibu ukaribie jamvini.
 
Karibu, lakini najiuliza swali hili,siku hizi hakuna jukwaa la utambulisho?Maana naona wageni wanapotea kila siku.

Kama njia mepotea,mwenyeji ngesaidia,
Vipi wanitangazia,jamvini kuniumbua?
Taratibu ngenambia,wapi pa kuingilia,
Haya sasa nasubiri,mjuzi nielekeze.
 
Karibu sana jamvini, jisikie uko nyumbani, wala usiwe na soni kumwaga yako maoni, nasema tena karibu ukaribie jamvini.

Asante kwa ukarimu,jamvini ngoja nikae,
Umeona umuhimu,mgeni kulonga nae,
Hakika umenikimu,BHULULU achana nae,
Kwa hakika sitasita,maoni yangu kutoa.
 

Salam twaitikia, huu ndio ufunguo,
Acha woga karibia,hapa ndipo kimbilio,
Usihofu nakwambia,hutopata karipio,
Karibu ndugu karibu,uje pata matukio.
 
Salam twaitikia, huu ndio ufunguo,
Acha woga karibia,hapa ndipo kimbilio,
Usihofu nakwambia,hutopata kalipio,
Karibu ndugu karibu,uje pata matukio.

Asante JIDU pokea,kwa hofu kuniondoa,
Funguo nishapokea,na ndani nimeingia,
Roho imenitulia,mazuri nasubiria,
Kwahakika sitasita,maoni yangu kutoa.

Nimeanza pitapita,huku kule humu ndani,
Ya busara kutafuta,yafaayo maishani,
Mengi nimeshayapata,na hayana nuksani,
Kwahakika sitasita,maoni yangu kutoa.

Vyumba vingi nimeona,ila hiki chanivuta,
Kidogo nimesonona,wengi wanaokipita,
Najua wanakiona,ila lugha mewapita,
Kwahakika sitasita,maoni yangu kutoa.

JIDU na wewe GLOBU,hakika mmenivuta,
Kuwasifu ni wajibu,subira mmeivuta,
Acha nende taratibu,uzoefu kutafuta,
Kwahakika sitasita,maoni yangu kutoa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…