Hofu Inavyotawala Historia ya Uhuru wa Tanganyika

Hofu Inavyotawala Historia ya Uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1730313026291.jpeg

Daily News 12 October 1988​

Ilibakia kidogo Daily News wakatae kuchapa kumbukumbu hiyo hapo juu ya miaka 20 ya kifo cha Abdul Sykes.​

Reginald Mhango ambae sasa ni marehemu, aliyekuwa mhariri wa Daily News alisema hawezi kuchapa kumbukumbu ya Abdul Sykes mpaka apewe ruhusa kutoka Dodoma.

Maneno hayo anamweleza marehemu Kleist Sykes mtoto wa Abdul Sykes.

Hawa walikuwa wakijuana vyema na wamesoma shule moja Aga Khan Secondary School.

Kleist akamwambia Reginald Mhango kuwa yote yaliyoandikwa katika kumbukumbu ya baba yake ni ya kweli na ndiyo historia ya baba yake kama vile kuasisi chama cha TANU na kuwa kadi yake ni No. 3 nk. nk.

Akamwambia Mhango kuwa ikiwa ana shaka na ukweli huo afanye rejea kwenye taazia ya baba yake iliyochapwa na Sunday News 20 October 1968 wakati huo mhariri wa Tanganyika Standard Muingereza Brendon Grimshaw.

Siku ya pili kumbukumbu ilichapwa lakini ilifanyiwa uhariri mkali sana.

Haikuchapwa kama nilivyoiandika.

Waswahili tuna msemo, "Heri nusu shari kuliko shari kamili."

1730313123842.jpeg

Sunday News 20 October 1968
 
View attachment 3139461
Daily News 12 October 1988​

Ilibakia kidogo Daily News wakatae kuchapa kumbukumbu hiyo hapo juu ya miaka 20 ya kifo cha Abdul Sykes.​

Reginald Mhango ambae sasa ni marehemu, aliyekuwa mhariri wa Daily News alisema hawezi kuchapa kumbukumbu ya Abdul Sykes mpaka apewe ruhusa kutoka Dodoma.

Maneno hayo anamweleza marehemu Kleist Sykes mtoto wa Abdul Sykes.

Hawa walikuwa wakijuana vyema na wamesoma shule moja Aga Khan Secondary School.

Kleist akamwambia Reginald Mhango kuwa yote yaliyoandikwa katika kumbukumbu ya baba yake ni ya kweli na ndiyo historia ya baba yake kama vile kuasisi chama cha TANU na kuwa kadi yake ni No. 3 nk. nk.

Akamwambia Mhango kuwa ikiwa ana shaka na ukweli huo afanye rejea kwenye taazia ya baba yake iliyochapwa na Sunday News 20 October 1968 wakati huo mhariri wa Tanganyika Standard Muingereza Brendon Grimshaw.

Siku ya pili kumbukumbu ilichapwa lakini ilifanyiwa uhariri mkali sana.

Haikuchapwa kama nilivyoiandika.

Waswahili tuna msemo, "Heri nusu shari kuliko shari kamili."

View attachment 3139462
Sunday News 20 October 1968
Sawa mzee wetu
 
Kwa hiyo huyu Kleist Sykes mtoto wa Abdu Sykes alirithi jina la babu yake ambaye ni baba wa Abdu Sykes kama sijakosea au sio kwa maana rahisi ni Kleist Sykes Juniour si ndio mzee wetu Mohamed mtoa mada?
 
Kwa hiyo huyu Kleist Sykes mtoto wa Abdu Sykes alirithi jina la babu yake ambaye ni baba wa Abdu Sykes kama sijakosea au sio kwa maana rahisi ni Kleist Sykes Juniour si ndio mzee wetu Mohamed mtoa mada?
Nos...
Sykes Mbuwane (Askari katika jeshi la Wajerumani) kutoka Mozambique, Kleist Sykes (kazaliwa Pangani) muasisi wa African Association, Abduwahid Sykes muasisi wa TANU, Kleist Sykes Mayor wa Dar-es-Salaam, Abduwahid Sykes...
 
Nos...
Sykes Mbuwane (Askari katika jeshi la Wajerumani) kutoka Mozambique, Kleist Sykes (kazaliwa Pangani) muasisi wa African Association, Abduwahid Sykes muasisi wa TANU, Kleist Sykes Mayor wa Dar-es-Salaam, Abduwahid Sykes...
Mzee umenikoroga sasa fanya hivyi andika linearly kuanzia kwa huyo mbuwane hadi kumfikia Abdulu ndio tutaelewana
 
Asante kanisa katoliki kwa kuhakikisha amani ya Tanzania
 
Kihistoria, kleist sykes ndio alieijenga taa, huyo abdul alirithi tu mikoba ya baba yake, hakuwa na uwezo wa kuongoza
Laki...
Kleist Sykes hakupata kuwa kiongozi wa TAA alifariki mwaka wa 1949.

Abdul Sykes alikuwa Secretary wa TAA 1950 na 1951 hadi 1953 alikuwa Act. President na Secretary wa TAA.

Alikuwa pia mjumbe wa TAA Political Subcommittee 1950 pamoja na Dr. Vedasto Kyaruzi, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Hamza Mwapachu, Steven Mhando na John Rupia.

Katika uchaguzi wa TAA 1953 Julius Nyerere alichaguliwa President Abdul Sykes Vice President.
 
Laki...
Kleist Sykes hakupata kuwa kiongozi wa TAA alifariki mwaka wa 1949.

Abdul Sykes alikuwa Secretary wa TAA 1950 na 1951 hadi 1953 alikuwa Act. President na Secretary wa TAA.

Alikuwa pia mjumbe wa TAA Political Subcommittee 1950 pamoja na Dr. Vedasto Kyaruzi, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Hamza Mwapachu, Steven Mhando na John Rupia.

Katika uchaguzi wa TAA 1953 Julius Nyerere alichaguliwa President Abdul Sykes Vice President.
Abdul sykes alidumu kweye uvice president wa taa kkwa muda gani?
 
Ndani ya TANU alipewa cheo gani?
Laki...
Baada ya kuundwa kwa TANU Abdul Sykes na mdogo wake Ally hawakuwa na wadhifa wowote ndani ya chama mbali na kupewa majukumu ya kutekeleza kuiimarisha TANU na kumsaidia Mwalimu Nyerere.

Kazi ya kusajili TANU walikabidhiwa Abdul na Ally Sykes pamoja na Nyerere.

Nyerere alipoacha kazi alikwenda kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes.

Vikao vyote muhimu vya siri vikifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes.
 
Laki...
Baada ya kuundwa kwa TANU Abdul Sykes na mdogo wake Ally hawakuwa na wadhifa wowote ndani ya chama mbali na kupewa majukumu ya kutekeleza kuiimarisha TANU na kumsaidia Mwalimu Nyerere.

Kazi ya kusajili TANU walikabidhiwa Abdul na Ally Sykes pamoja na Nyerere.

Nyerere alipoacha kazi alikwenda kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes.

Vikao vyote muhimu vya siri vikifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes.
Kama hakuwa na cheo tanu mchango wake kwenye kudai uhuru ni mdogo sana
 
Kama hakuwa na cheo tanu mchango wake kwenye kudai uhuru ni mdogo sana
Laki...
Kughitilafiana katika fikra ni silka yetu binadamu.

Mimi nimepata umaarufu mkubwa na tuzo kadhaa kwa kuandika kitabu cha Abdul Sykes.

Miaka 23 iliyopita niliandika kwenye shajara yangu taarifa kuwa Abdul Sykes na Julius Nyerere waligimbea nafasi ya urais wa TANU tarehe 17 April 1953 katika Ukumbi wa Arnautoglo.

Kisha nikaandika kutawazwa kwa Malkia Elizabeth II chini yake nikaandika tarehe ya uchaguzi wa Rais wa TAA mwaka 1953.

Uchaguzi ulifanyika Arnatouglo Hall tarehe 17 April 1953 kati ya Abdulwahid Kleist Sykes na Julius Kambarage Nyerere.

Wakati huu nilikuwa katika utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes.
Taarifa hizi mbili katika Nyaraka za Sykes zilinisisimua sana.

Sababu yake ni kuwa ingawa Judith Listowel alikuwa ameeleza uchaguzi huu katika kitabu chake, "The Making of Tanganyika," (1965) hakueleza tarehe ya uchaguzi ule.

Jambo la pili ni kuwa baada ya uchaguzi huu uongozi mpya wa TAA President Julius Nyerere na Vice-President Abdul Sykes pamoja halmashauri yote ya TAA waliandika barua ya pongezi kwa Malkia Elizabeth na wote walitia saini zao katika barua hii.

Barua hii ipo katika Nyaraka za Sykes.

Mwaka wa 2012 Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Othman Yahya na Dr. Ng'waza Kamata walipokuja kunihoji kuhusu historia ya Julius Nyerere wakati wanaandika "Nyerere Biography," (2020) waliniomba nakala na niliwapa.

Imekuwa kawaida kila nikiingia Maktaba kupumzika lazima nitakuta kitu.
Tutazame hizi Nyaraka za Sykes katika "In Praise of Ancestors," makala iliyozua taharuki.

Katika rejea kutoka Nyaraka za Sykes foot note no. 16 kuna barua ya Julius Nyerere ya tarehe 10 August, 1953 anamwandikia Gavana Edward Twining.

Kwa mara yangu ya kwanza kuiona saini ya Mwalimu Nyerere nje ya saini yake kwenye noti nimeiona kwenye hizi Nyaraka za Sykes.

Lakini nilikuwa nasisimkwa na mwili pamoja na akili pale Ally Sykes alipokuwa akinieleza mazingira yaliyopelekea kuandikwa kwa barua fulani.

Kitendawili nilichokutananacho kilikuwa rasimu ya katiba ya TANU.
Katiba hii iliyeyuka kama moshi.

Haipo kwenye Nyaraka za Sykes wala Maktaba ya CCM Dodoma.

Katika Maktaba ya CCM nilionyeshwa majalada mengi lakini karibuni yote kulikuwa na nyaraka zilizonyofolewa.

Nilibahatika kuliona jalada la Hamza Mwapachu na jalada la Abdul Sykes.
Majalada yote haya hayakuwa na hata karatasi moja ndani.

Nilipata tabu sana na mhariri wangu wa kitabu cha Abdul Sykes alipokuwa anaupitia mswada kwa ajili ya kuchapa kitabu.

Mimi nilikuwa nimeandika nyaraka zimeibiwa yeye akinitahadharisha kuhusu neno hilo la kuibiwa akiniambia linaweza kusababisha matatizo tukashitakiwa.

1734987490667.jpeg

1734987580510.jpeg
 
Tuji...
Hiyo ndiyo nakala bora niliyokuwanayo.
Asante. kwa kuwa nakala unayo, kama hautojali, naomba uiandike neno kwa neno hapa JF na kwenye uzi huu ilitufaidi matunda ya makala hiyo, Mkuu. Natanguliza shukrani.
 
Back
Top Bottom