Mkalibari
JF-Expert Member
- Mar 20, 2012
- 659
- 399
Habari Wadau ,hivi Sasa nimepitia maeneo ya Kigamboni Tungi kwenye Round about kuelekea Darajani,Kibada na Feri kwa mbele kidogo Kuna Kituo Cha mafuta.
Nimekuta Kuna zogo kubwa la watu,kutahamaki ni milio ya Risasi na watu wanakimbia hovyo.
Sijajua chanzo rasmi ni Nini,japo wengi wanasema kile Kituo Cha mafuta kina mgogoro wa umiliki.
Nimeona mabaunsa zaidi ya 10 wakizunguka zunguka wengine wameshika mapanga na wengine wameshika Bunduki.
Taharuki ni kubwa na istoshe watu ni wengi kwakua Leo ni siku ya mnada wa wakazi wa kikagamboni eneo lile.
Pia Kuna taarifa zisizo rasmi kua Kuna watu wamekufa kwa kukaganyagwa na Roli liloingia kwa Kasi ndani ya sheli na kuondoka Kasi pasipo kujulikana ni Nani alikua analiendesha.
Baadae niliona polisi wanaingia kutuliza ghasia,Mimi kwa usalama wangu nikaamua kuondoka zangu.
Sijui Kuna Nini siku hizi,michezo ya Bunduki imeanza Tena
Update
Yeah nasikia mabati Yale yamewekwa alfajiri ya leo kuzunguka eneo lote,na nembo na jina la sheli zikazibwa na stika baadae wakawekwa mabaunsa kibao kulinda hapo.
Ndio mida ya jioni imekuja kichwa Cha Roli kikiwa Kasi kigaingia ndani kwa kugonga mabati Yale na kikakanyaga watu kadhaa na inasemekena wamekufa papo hapo, hofu ni kubwa Sana aiseh.
---
Dar es Salaam 27, Agosti, 2021
Jeshi la Polisi Kanda Maalim Dar es Salaam linamshikilia Mohamed Jumaa@Lardh JM (37),Mkazi wa Kariakoo kwa tuhuma za mauaji ya walinzi wawili waliofahamika kwa majina ya Eliakim Morali(30), Mkazi wa Mbezi Beach, Mlinzi wa Kampuni ya LOCK FORT SECURITY na Saunkoo Bakari(35), Mkazi wa Buguruni, Mlinzi Binafsi (BAUNSA).
Mnamo tarehe 26 Agosti, 2021 majira ya saa 12 jioni huko eneo la Tungi Wilaya Kigamboni katika kituo cha kuuzia mafuta cha JM PETROL STATION, mtuhumiwa aliwaua walinzi hao kwa kuwagonga kwa makusudi na gari lenye namba T 176 CVP aina ya DAF lori lililokuwa na tera ambalo halina namba za usajili.
Mtuhumiwa alifika katika kituo hicho cha kuuzia mafuta cha JM PETROL STATION alichokuwa ana kimiliki kwa ajili ya kuhamisha mali zake lakini alichukua gari lake na kutoka nje ya kituo na ghafla alirudi nalo kwa kasi huku likiwa halina tera na kuwagonga walinzi hao waliokuwa getini na kupelekea kufariki dunia papo hapo na kuwajeruhi watu sita ambao walikimbizwa hospitalini kwa matibabu.
Mtuhumiwa huyo alikuwa na kesi ya madai namba 118/2018 mahakama kuu iliyofunguliwa na ACCESS Benki baada ya kushindwa kulipa mkopo kwa muda muafaka aliochukua katika benki hiyo na mtuhumiwa alishindwa mahakamani licha ya kukata rufaa mara kadhaa na hatimaye mahakama ilitoa amri ya kuuzwa kwa kituo chake cha kuuzia mafuta maarufu kama JM PETROL STATION kilichopo kigamboni.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na uchungunguzi wa kina juu ya tukio hili na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani hivi karibuni kujibu tuhuma zinazomkabili.
Imetolewa na:-
MULIRO J.MULIRO- ACP
KAMANDA WA POLISI,
KANDA MAALUM,
DAR ES SALAAM
Nimekuta Kuna zogo kubwa la watu,kutahamaki ni milio ya Risasi na watu wanakimbia hovyo.
Sijajua chanzo rasmi ni Nini,japo wengi wanasema kile Kituo Cha mafuta kina mgogoro wa umiliki.
Nimeona mabaunsa zaidi ya 10 wakizunguka zunguka wengine wameshika mapanga na wengine wameshika Bunduki.
Taharuki ni kubwa na istoshe watu ni wengi kwakua Leo ni siku ya mnada wa wakazi wa kikagamboni eneo lile.
Pia Kuna taarifa zisizo rasmi kua Kuna watu wamekufa kwa kukaganyagwa na Roli liloingia kwa Kasi ndani ya sheli na kuondoka Kasi pasipo kujulikana ni Nani alikua analiendesha.
Baadae niliona polisi wanaingia kutuliza ghasia,Mimi kwa usalama wangu nikaamua kuondoka zangu.
Sijui Kuna Nini siku hizi,michezo ya Bunduki imeanza Tena
Update
Yeah nasikia mabati Yale yamewekwa alfajiri ya leo kuzunguka eneo lote,na nembo na jina la sheli zikazibwa na stika baadae wakawekwa mabaunsa kibao kulinda hapo.
Ndio mida ya jioni imekuja kichwa Cha Roli kikiwa Kasi kigaingia ndani kwa kugonga mabati Yale na kikakanyaga watu kadhaa na inasemekena wamekufa papo hapo, hofu ni kubwa Sana aiseh.
---
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Dar es Salaam 27, Agosti, 2021
KUKAMATWA KWA MTUHUMIWA WA MAUAJI YA WATU WAWILI WILAYA YA KIGAMBONI
Jeshi la Polisi Kanda Maalim Dar es Salaam linamshikilia Mohamed Jumaa@Lardh JM (37),Mkazi wa Kariakoo kwa tuhuma za mauaji ya walinzi wawili waliofahamika kwa majina ya Eliakim Morali(30), Mkazi wa Mbezi Beach, Mlinzi wa Kampuni ya LOCK FORT SECURITY na Saunkoo Bakari(35), Mkazi wa Buguruni, Mlinzi Binafsi (BAUNSA).
Mnamo tarehe 26 Agosti, 2021 majira ya saa 12 jioni huko eneo la Tungi Wilaya Kigamboni katika kituo cha kuuzia mafuta cha JM PETROL STATION, mtuhumiwa aliwaua walinzi hao kwa kuwagonga kwa makusudi na gari lenye namba T 176 CVP aina ya DAF lori lililokuwa na tera ambalo halina namba za usajili.
Mtuhumiwa alifika katika kituo hicho cha kuuzia mafuta cha JM PETROL STATION alichokuwa ana kimiliki kwa ajili ya kuhamisha mali zake lakini alichukua gari lake na kutoka nje ya kituo na ghafla alirudi nalo kwa kasi huku likiwa halina tera na kuwagonga walinzi hao waliokuwa getini na kupelekea kufariki dunia papo hapo na kuwajeruhi watu sita ambao walikimbizwa hospitalini kwa matibabu.
Mtuhumiwa huyo alikuwa na kesi ya madai namba 118/2018 mahakama kuu iliyofunguliwa na ACCESS Benki baada ya kushindwa kulipa mkopo kwa muda muafaka aliochukua katika benki hiyo na mtuhumiwa alishindwa mahakamani licha ya kukata rufaa mara kadhaa na hatimaye mahakama ilitoa amri ya kuuzwa kwa kituo chake cha kuuzia mafuta maarufu kama JM PETROL STATION kilichopo kigamboni.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na uchungunguzi wa kina juu ya tukio hili na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani hivi karibuni kujibu tuhuma zinazomkabili.
Imetolewa na:-
MULIRO J.MULIRO- ACP
KAMANDA WA POLISI,
KANDA MAALUM,
DAR ES SALAAM
.