Hofu yangu katiba mpya na tiba yake.

JEKI

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2013
Posts
4,845
Reaction score
2,957
Rais amekuwa akisisitiza sana kama katiba mpya haitapatikana basi ya zamani itaendelea, tunajua wapo watu wengi ndani ya utawala hawataki katiba mpya wanaweza kutuletea kitu cha hovyo ili tukikatae wao wapete. Nimejiuliza sana hivi suruhu ya katiba mpya ikikataliwa ni kuendelea na ya zamani tu? hakuna njia nyingine? kwa kweli iwavyo tusikubali kurudi kwenye katiba ya zamani, mfano kikatokea kipengere kimoja tu kibovu, je tuikatae yote?.

Tiba ya hoja hapo juu ni hii, kwa kuwa wengi hatutaki katiba ya zamani, basi siku ya kupiga kura tupigie kura rasimu hii iliyotolewa na Warioba na ile itakayotolewa na bunge la katiba, pia napendekeza vipengele vyote tata tuvipigie kura separate, mfano suala la muungano kuwe na kipengele cha wanaotaka serikali 1, 2 au 3 na itakayoshinda ndo iingizwe kwenye katiba mpya, hii ni kuzuia kipengele kimoja au viwili kukwamisha katiba nzima.

Karibuni tuchambue.
 
Hapo kwenye muungano naunga kiwiliwili hoja maana mkono mdogo hautatosha
 
mimi kwangu swala la muungano wala siyo hoja kweli tuko tofauti.
 
mimi kwangu swala la muungano wala siyo hoja kweli tuko tofauti.

kwa nini unasema hivyo, zaidi ya asilimia 99 ya wazanzibar wameongelea juu ya muungano, tume nayo imesema katika masuala yaliyoiumiza kichwa na kuchukua muda mrefu ni suala la muungano, funguka labda nitakuelewa mwa 4.
 
Last edited by a moderator:
tafadhali usiache kuomba kwenda kwenye bunge la katiba mkuu. unaonekana unahoja nzuri.
 
tafadhali usiache kuomba kwenda kwenye bunge la katiba mkuu. unaonekana unahoja nzuri.

asante mkuu, inabidi sasa mnipendekeze maana kule mtu hujipeleki tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…