Hoja: Bidhaa zote zinazosajiliwa Tanzania ziwe na maelezo ya mtumiaji kwa lugha ya Kiswahili

Hoja: Bidhaa zote zinazosajiliwa Tanzania ziwe na maelezo ya mtumiaji kwa lugha ya Kiswahili

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Nimeonelea nilete hii mada kwa mara ya pili.

Maelezo kwa mtumiaji ni muhimu sana hasa kwa vitu kama dawa. Sasa unakuta bidhaa inauzwa Tanzania na nyingine inatengenezwa hapahapa lakini inakuwa na maelezo ya Kiingereza, Kifaransa, kiarabu na lugha zingine lakini si Kiswahili.

Watumiaji wengi wa nchi hii wanajua Kiswahili tu, sasa maelezo ya hivyo yanamlenga nani? Kiingereza ni lugha rasmi lakini ni wangapi wanaielewa?

Watu wanatumia kitu bila kujua madhara yake na kumbe yameandikwa hapohapo ila shida lugha. Mtu unashindwa kurekebisha kaishu kadogo kumbe utatuzi umeandikwa hapohapo.

Mtu unanunua sabufa yako kali ila unashindwa kuconnect na maelezo ya kuconnect yameandikwa hapohapo.

Unanunua dawa, maelezo ya madhara na namna ya kutumia yameandikwa hapo ila unatumia upo gizani.

Mi nashauri bidhaa yeyote isisajiliwe kuuzwa Tanzania kama haina maelezo ya mtumiaji kwa lugha ya kiswahili. Iwe simu, TV, gari, dawa yaani bidhaa zote. Au nakosea ndugu zangu?
 
Hakikisha unanunua DAWA famasi

Maelekezo utayakuta hapo

Sabufa utauliza connection kwa rafiki kilaza na hakosei, hata mwanao
 
Hakikisha unanunua DAWA famasi

maelekezo utayakuta hapo

sabufa utauliza connection kwa rafiki kilaza na hakosei, hata mwanao
Vijijini na pembezoni hakuna hizo pharmacy. Pia kukiwa na wateja wengi kunakuwa hakuna muda wa kupeana maelezo.
 
Mbona watu huwa wanapewa maelezo kwamba uvutaji wa sigara Ni hatari kwa afya lakini bado wanavuta...usinywe na kuendesha vyombo vyamoto..but parking za bar zinajaa magari...
 
Mbona watu huwa wanapewa maelezo kwamba uvutaji wa sigara Ni hatari kwa afya lakini bado wanavuta...usinywe na kuendesha vyombo vyamoto..but parking za bar zinajaa magari...
Umewahi kujiuliza kuwa bila hayo maonyo matumizi ya hivyo vitu yangekuwaje?
 
hivi condomu nayo ni dawa au kifaa..? mbona hatusomi yale maelekezo pale nje ya box badala yake tunakimbilia kuvaa na kuchomeka haraka kama vile wote tulikuwa kwenye semina ya ngono elekezi
 
Nchi yenu kiingereza si ni lugha rasmi pia? Mnalia nini sasa? Mitaala yenu mnasoma kwa lugha gani?
 
Back
Top Bottom