Mphamvu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 10,702
- 3,319
Si lengo la bandiko hili kuchukua sura ya kidini, lakini mara kadhaa nimeona watu wakienda katika nyumba za ibada kupokea sadaka kutoka kwa watu wenye uwezo. Wakati fulani nikiwa shule ya msingi tulikuwa tukitoroka kwenda kwa mama mmoja wa Kihindi kuchukua Sh.100 za msaada. Hadi leo ipo baadhi ya misikiti matajiri fulani hutoa fedha kwa kila muumini anayekuja kuswali siku ya Ijumaa.
Hoja yangu inawalenga hasa hawa matajiri wawezeshaji wa fedha, ya kuwa kwanini wasitafute mbinu nyingine ya kuwawezesha hawa watu 'masikini' kuliko kuwapa fedha mkononi? Kawaida hii inaendeleza umasikini wa fikra, hufika hatua ya watu kukopa na kuahidi kuwa ikifika siku fulani nitalipa (kwa kuwa ana uhakika wa kupokea hii sadaka).
Wanaotoa wanaweza kuwa na nia tu ya kutimiza wajibu wao kiimani, kwa kuwa imani nyingi husema tuwasaidie wenye shida lakini nina shaka na aina hii ya usaidizi. Wapo watu wabunifu lakini wanakwama kwa kukosa mitaji pamoja na kuwa mawazo yao ni murua kabisa. Kwanini watoaji hawa wasielekeze nguvu huko kuliko kumpa mtu fedha taslimu, ambayo hajaitolea jasho na inazidi kumtia umasikini?
Naombeni mrejesho.
Hoja yangu inawalenga hasa hawa matajiri wawezeshaji wa fedha, ya kuwa kwanini wasitafute mbinu nyingine ya kuwawezesha hawa watu 'masikini' kuliko kuwapa fedha mkononi? Kawaida hii inaendeleza umasikini wa fikra, hufika hatua ya watu kukopa na kuahidi kuwa ikifika siku fulani nitalipa (kwa kuwa ana uhakika wa kupokea hii sadaka).
Wanaotoa wanaweza kuwa na nia tu ya kutimiza wajibu wao kiimani, kwa kuwa imani nyingi husema tuwasaidie wenye shida lakini nina shaka na aina hii ya usaidizi. Wapo watu wabunifu lakini wanakwama kwa kukosa mitaji pamoja na kuwa mawazo yao ni murua kabisa. Kwanini watoaji hawa wasielekeze nguvu huko kuliko kumpa mtu fedha taslimu, ambayo hajaitolea jasho na inazidi kumtia umasikini?
Naombeni mrejesho.