Hoja ya Kukera: Ingekuwa nchi nyingine Kikwete angekuwa impeached

Hoja ya Kukera: Ingekuwa nchi nyingine Kikwete angekuwa impeached

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
[h=5]Kama kuna mtu yeyote anayejua anisaidie; ni wapi katika Katiba ya sasa ambapo Rais au mtu yeyote yule amepewa madaraka ya kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya? Ikumbukwe kuwa viongozi wote walioanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya waliapa "kuitetea, Kuilinda, na kuihifadhi" Katiba ya sasa![/h]Fikiria kuwa walipoanzisha huu mchakato wa kuandika "Katiba Mpya" walifanya hivyo kwa matakwa yao tu. Hakukuwa na hoja Bungeni, hakukuwa na kikao cha Kamati Kuu ya CCM na wale hakukuwa na utaratibu ambao ulikuwa unafuatwa. Cha kushangaza hata hivyo ni kuwa waliposema wanakubali kuandika Katiba Mpya (kinyume na Katiba ya sasa) wakasema baadhi ya mambo yaliyomo ndani ya Katiba ya sasa hayawezi kuhojiwa na wananchi! Kwamba wananchi wanaweza kuzungumzia mambo mengine yote isipokuwa mambo fulani fulani! Nani aliwapa madaraka ya kuamua nini kisizungumzwe? Walipata wapi madaraka ya kuwakataza wananchi wasijadili na kuamua baadhi ya mambo kwa mfano uwepo wa Jamhuri ya Muungano?

Ndio maana nasema ingekuwa nchi nyingine...

Lakini kwa vile hii ni Tanzania....
 
Kweli imekukera pole sana ndiyo mambo, umeishachelewa mkuu ndege imeishapaa muda mrefu, ulikuwa wapi kuyasema haya mapema.
 
Angekuwa ameanzisha mada hii mtu mwingine thread ingefutwa fasta . Kwa kuwa ni MMM aah itaendelea kujadiliwa
 
Mzee mimi huwa nachoka na mafumbo yako, kwanini usifunguke kila kitu wazi ili hata mjinga akuelewe vizuri? Lete uzi uliokamilika kabisa wenye dukuduku na kutoa suruhu nini kifanyike, usiwe kama hawa vibaraka wa Lubumba akina Lukosi.
 
Kweli imekukera pole sana ndiyo mambo, umeishachelewa mkuu ndege imeishapaa muda mrefu, ulikuwa wapi kuyasema haya mapema.
Pamoja na kuchelewa hoja yake ni nzito response yako inapwaya sana.
 
Pamoja na kuchelewa hoja yake ni nzito response yako inapwaya sana.

Aina uzito wowote labda tuambie wewe ambaye unaiona ina uzito ingekuwa nchi gani Kikwete angekuwa impeached?

Kila nchi ina taratibu zake unaleta habari ingekuwa.
 
Kweli imekukera pole sana ndiyo mambo, umeishachelewa mkuu ndege imeishapaa muda mrefu, ulikuwa wapi kuyasema haya mapema.

Mkuu ritz, kwako wewe ukweli ni ule unaotokea upande wako tu? Mtu wa upande wa pili akikwambia saa hizi ni asubuhi utalazimika kummuliza mtu mwingine wa upande wako kama kweli ni asubuhi!!Lumumba product.
 
Pamoja na kuchelewa hoja yake ni nzito response yako inapwaya sana.

Uzito wake ni upi hapo... ??? Hoja yake haina mshiko kabisa... Amesubiri yashatokea ndio ahoji leo .. si ndio unafki wenyewe huu ...

Msiturudishe nyuma maona wananchi washatoa .. walio wengi wapewe
 
Mkuu ritz, kwako wewe ukweli ni ule unaotokea upande wako tu? Mtu wa upande wa pili akikwambia saa hizi ni asubuhi utalazimika kummuliza mtu mwingine wa upande wako kama kweli ni asubuhi!!Lumumba product.

Hakuna ukweli mkuu, labda niambie ukweli ni upi hapa?
 
Obama said chill on the beach you got me impeached you gonna learn today
 
Ngoja tupate katiba mpya mkuu,sii unajua watawala wetu wanaendana na matukio kutoa maamuzi
 
Ngoja nijaribu kutafuna tafuna kama meno yangu yatakuwa bado ni 32 na hayajaoza.

Anachosema Mwanakijiji ni kuwa viongozi waliopo waliapa kuilinda na kuitetea katiba ya sasa.
Kama kulikuwa na haja basi utaratibu ulikuwa kuwafikia wananchi kwa kupitia bunge ili hoja ya kuanzisha mchakato ianze.
Hapa watu watofautishe na suala la kufikisha mswada wa kuanzisha mchakato. Hivyo ni vitu viwili tofauti.

Hakuna hoja iliyoletwa kuhusu kuanzishwa kwa mchakato. Na katika kumbu kumbu hiyo haikuwa katika ilani ya uchaguzi wa chama tawala chenye serikali.

Na pia hautukuwahi kusikia kikao cha dharura alau cha kamati kuu kuhusu muanzishwa kwa mchakato.
Tunachokumbuka ni rais kuhutubia taifa kila mwezi na kuleta hoja na mswada ukafuata.

Katika mswada huo ikasemwa jambo kadha wa kadha lisijadiliwe.
Hapo ndipo swali likaja kuwa kwavile hakukuwa na hoja ya kuanzishwa mchakato, hii nguvu ya wao kusema hiki hapana kile ndio inatoka wapi tukizingatia kuwa hakuna hoja iliyopelekwa bungeni wala katika vikao vya chama tawala?

Kwa maneno mengine ni mtu au watu waliamua pengine kwa kusikia kelele za watu. Ni jambo jema, lakini wapi walipata mguvu ya kuzifanya kelele hizo ziwe na nguvu ya kisheria na kikatiba kama tulivyokubaliana?

Ni kutokana na kukiuka taratibu ndiyo maana tulisikia Rais akitangaza ratiba ya mchakato badala ya mwenyekiti wa tume.
Inaweza kuwa ni katika kufanya majukumu pamoja, la haualaa! sasa hivi kuna issue.

Ratiba nzima ya kupata katiba mpya imetoka, kumbe tumesahau kuwa lazima Tanganyika irudi sasa sijui tunaiweka wapi katika ratiba.

Ujumbe ni kuwa matatizo tunayoyaona ya kuwa na rasimu ya muungano kabla ya Tanganyika, ni matokeo ya kutokuwa na mjadala ambao ungetokea katika hoja kisha mswada halafu mchakato.

Treni imeanza kurudi nyuma ndiyo haya ya vikao vya CC vya dharura.

Hata hiyo CC ya CCM sijui inajadili nini, imejikuta inajadili tatizo la mtoto bila kujua kutongozana,ndoa, utungo wa mimba ulikuwaje. Wapo bize kujadili huyu mtoto alelewee vipi!
 
Back
Top Bottom