Hoja ya Serikali tatu inapotoshwa

Hoja ya Serikali tatu inapotoshwa

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Hoja hii iliyo katika Rasimu ya Pili ya Katiba iliyokabidhiwa kwa Rais Kikwete na Rais Shein na kutetewa ipasavyo na Jaji Warioba inapotoshwa sana. Inaandamwa na propaganda.Mojawapo ni kuwa na Marais watatu! Nani amesema (au Rasimu gani iliyopendekeza Marais watatu)? Huu ni upotoshaji.

Rasimu ya Jaji Warioba inahusika na suala moja kuu:Serikali ya Muungano. Ni Tanzania tu na si Zanzibar wala Tanganyika. Kwakuwa Rasimu inazungumzia namna Serikali ya Muungano itakavyokuwa,ndiyo maana Serikali za Zanzibar na Tanganyika (iliyoitwa Tanzania Bara) zinadokezwa. Mantiki hapa ni kuwa Tanzania itakuwa moja lakini yenye Serikali tatu. Moja ni zao la muungano (Serikali ya Muungano).Ya pili ni Serikali ya Tanzania Bara (kama mshiriki wa muungano) na Serikali ya Zanzibar(mshiriki mwingine wa muungano).

Kinachozaa propaganda zote hizi dhidi ya serikali tatu ni Urais. Vipo vyama na watu wenye 'airtime' kwenye vyombo vya habari na Serikalini waliojaa mawazo ya 'Urais' tu. Wakilala-urais;wakiamka-urais. Wanapotosha hoja kwa kusema kuwa Tanzania itakuwa na Marais watatu. Si lazima kuwa na Marais watatu. Mbona Ujerumani yenye Serikali za Majimbo 16 haina Marais 17? Marekani kuna utawala wa aina hiyo hiyo lakini Rais mmoja.

Hakuna hata Ibara moja ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba inayopendekeza muundo wa Serikali za Tanzania Bara na Zanzibar. Wasingeweza kupendekeza hivyo kwakuwa hiyo haikuwa kazi yao.Wao walikuwa kimuungano. Mfumo na ukubwa wa Serikali za Tanzania Bara na Zanzibar vimeachwa kwa wahusika wenyewe. Watafanya hivyo na watakavyo iwapo Rasimu ya Muungano itapitishwa kama inavyopendekeza.

Hakuna hata Ibara moja ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba iliyopendekeza aina ya viongozi wa Serikali za Tanzania Bara na Zanzibar;kama ziongozwe na Marais,Mawaziri Wakuu,Wafalme au Wakuu wa Mikoa. Hii hoja ya Marasi watatu inatokea wapi zaidi ya kuwa upotoshaji wa Rasimu?

Wengi wetu tunajua,tunatambua na kuthamini kazi ya Tume ya Jaji Warioba. Imewasikiliza watanzania na kuandika maoni yao juu ya Katiba yao katika Rasimu. Wao wameandika tu maoni ya watanzania. Yeyote atakayejaribu,kulazimisha au kushawishi kuchakachuliwa kwa maoni hayo,hatabaki salama. Huo ndio ukweli. Kadiri muda unavyokwenda,ndivyo tunavyoendelea kuwaona wapotoshaji na kujiandaa kuwashughulikia.

Time will tell!
 
Umenena! Na nimewasikia vigorous kabisa wa siku nyingi pamoja na wana taaluma wakidai eti itakuwa ghali kwani kutokuwepo maafisa watatu! Watu wengine ni ubishi tu na Kwa Ndugu zangu CCM wameamua sasa Hoja ya Nguvu!

asante Kwa mada iliyoutulia
 
Wewe Mkuu Bongolander umeipitia Rasimu? Inataja Marais wangapi?

Ninakubalina na wewe kwenye kitu kimoja ambacho watanzania wengi tunashindwa kuelewa: yaani cheo na madaraka. Kutokana na kutokuelewa tofauti hizo, tumeshindwa pia kuelewa kuwa Tanzania mpaka sasa hivi tuna serikali nyingi kutokana na madaraka yake. Serikali ya jiji la Dar es Salaam inaongozwa na DAKTA Massabburri kwa mfano wakati ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaongozwa na DAKTA Kikwete na ile ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaongozwa na Dr Sheni. Tanzania mpaka leo tuna serikali nyingi sana zinazoitwa serikali za mitaa au serikaliza vijiji. Kama ambavyo madaraka ya DAKTA Massabburri yalivyokwenye jiji la Dar es Salaam tu wala hayafiki kule kwao Tarime, na yale ya DAKTA Kikwete yako Tanzania nzima wala hayaingiliani na Meya ya Bagamoyo wala yale ya Dr. Shein kule Zanzibar ni kuwa kinachotakiwa ni kwa Katiba kuweka bayana mipaka ya madaraka ya viongozi wa serikali hizo.

Tukishatofautisha maana ya madaraka na serikali nadhani hatutaona ugumu kabisa wa kuwa na serikali tatu. Tatizo ni kuwa baadhi ya wanaotaka serikali tatu au zaidi kuendana na madaraka ya mwisho; hiyo ndiyo inayotisha na kuleta mkanganyiko, kwani hatuwezi kuwa na watu wengi ndani ya nchi moja wakiwa na madaraka ya mwisho kuhusu maisha yetu ya kila siku. Wenzetu Marekani wana serikali nyingi sana, yaani za miji, county, state na ile ya federal inayoongozwa na Obama lakini madaraka ya viongozi hizo serikali nyingine hayaingiliani kabisa na yale ya Obama anayeongoza Federal government.
 
Wewe Mkuu Bongolander umeipitia Rasimu? Inataja Marais wangapi?

Mkuu suala hapa sio nani kuwa rais, suala ni serikali. Kama mkuu wa serikali ataitwa Waziri, gavana au mkuu, haina maana kuwa hiyo sio serikali.

suala ni mamlaka, madaraka, nguvu , raslimali nk za hizo serikali. Hata kama wakiita jimbo la Tanganyika na mkuu wake akaitwa mkuu wa mkoa jimbo la Tanganyika, kama likiwa na bunge, makahama, jeshi na raslimali nyingine nyingi ambazo Rais wa Jamhuri ya Tanzania atazitegemea....basi kiongozi wa hilo jimbo atakuwa na nguvu kuliko rais.

Suala ni serikali tatu, sio marais watatu.
 
Mkuu suala hapa sio nani kuwa rais, suala ni serikali. Kama mkuu wa serikali ataitwa Waziri, gavana au mkuu, haina maana kuwa hiyo sio serikali.

suala ni mamlaka, madaraka, nguvu , raslimali nk za hizo serikali. Hata kama wakiita jimbo la Tanganyika na mkuu wake akaitwa mkuu wa mkoa jimbo la Tanganyika, kama likiwa na bunge, makahama, jeshi na raslimali nyingine nyingi ambazo Rais wa Jamhuri ya Tanzania atazitegemea....basi kiongozi wa hilo jimbo atakuwa na nguvu kuliko rais.

Suala ni serikali tatu, sio marais watatu.
Ni kweli Mkuu Bongolander.Lakini,hata Serikali zilizopo sasa ikisemwa zigawanywe zitatoka Serikali ngapi? Idadi ya waunda-serikali itawekwa na Katiba husika ya Tanzania Bara na Zanzibar. Halafu, hakutakuwa na matumizi yatakayozidi mapato ya Serikali.Hofu inatoka wapi kabla ya kuijadili KATIBA?
 
Last edited by a moderator:
Hoja hii iliyo katika Rasimu ya Pili ya Katiba iliyokabidhiwa kwa Rais Kikwete na Rais Shein na kutetewa ipasavyo na Jaji Warioba inapotoshwa sana. Inaandamwa na propaganda.Mojawapo ni kuwa na Marais watatu! Nani amesema (au Rasimu gani iliyopendekeza Marais watatu)? Huu ni upotoshaji.

Rasimu ya Jaji Warioba inahusika na suala moja kuu:Serikali ya Muungano. Ni Tanzania tu na si Zanzibar wala Tanganyika. Kwakuwa Rasimu inazungumzia namna Serikali ya Muungano itakavyokuwa,ndiyo maana Serikali za Zanzibar na Tanganyika (iliyoitwa Tanzania Bara) zinadokezwa. Mantiki hapa ni kuwa Tanzania itakuwa moja lakini yenye Serikali tatu. Moja ni zao la muungano (Serikali ya Muungano).Ya pili ni Serikali ya Tanzania Bara (kama mshiriki wa muungano) na Serikali ya Zanzibar(mshiriki mwingine wa muungano).

Kinachozaa propaganda zote hizi dhidi ya serikali tatu ni Urais. Vipo vyama na watu wenye 'airtime' kwenye vyombo vya habari na Serikalini waliojaa mawazo ya 'Urais' tu. Wakilala-urais;wakiamka-urais. Wanapotosha hoja kwa kusema kuwa Tanzania itakuwa na Marais watatu. Si lazima kuwa na Marais watatu. Mbona Ujerumani yenye Serikali za Majimbo 16 haina Marais 17? Marekani kuna utawala wa aina hiyo hiyo lakini Rais mmoja.

Hakuna hata Ibara moja ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba inayopendekeza muundo wa Serikali za Tanzania Bara na Zanzibar. Wasingeweza kupendekeza hivyo kwakuwa hiyo haikuwa kazi yao.Wao walikuwa kimuungano. Mfumo na ukubwa wa Serikali za Tanzania Bara na Zanzibar vimeachwa kwa wahusika wenyewe. Watafanya hivyo na watakavyo iwapo Rasimu ya Muungano itapitishwa kama inavyopendekeza.

Hakuna hata Ibara moja ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba iliyopendekeza aina ya viongozi wa Serikali za Tanzania Bara na Zanzibar;kama ziongozwe na Marais,Mawaziri Wakuu,Wafalme au Wakuu wa Mikoa. Hii hoja ya Marasi watatu inatokea wapi zaidi ya kuwa upotoshaji wa Rasimu?

Wengi wetu tunajua,tunatambua na kuthamini kazi ya Tume ya Jaji Warioba. Imewasikiliza watanzania na kuandika maoni yao juu ya Katiba yao katika Rasimu. Wao wameandika tu maoni ya watanzania. Yeyote atakayejaribu,kulazimisha au kushawishi kuchakachuliwa kwa maoni hayo,hatabaki salama. Huo ndio ukweli. Kadiri muda unavyokwenda,ndivyo tunavyoendelea kuwaona wapotoshaji na kujiandaa kuwashughulikia.

Time will tell!
Mkuu wangu swala la serikali 3 halina Ubishi. Ni lazima kila serikali itakuwa na kingozi wake sasa umuite Rais, sijui waziri kiongozi, au Waziri mkuu (Premier), senator bado nafasi hizo tatu (kiongozi wa Znz, Kiongozi wa Bara na Kiongozi wa muungano)zinahitajika na watavuta mshahara sawa na marais iwe kwa jina lolote.

Kwa hiyo iwe rasimu imeacha ama vyovyote bado haiwezekani kuundwa serikali ikakosa mkuu wa nchi hiyo! ni logic tu mkuu wangu. Na pia ufahamu kila serikali itakuwa na mawaziri na wabunge wa kujaza serikali zote 3 haihitaji sayansi kutambua hilo maana tunaunda serikali inayofanana na serikali za nchi nyinginezo. Hivyo tutakuwa na mawaziri wa Tanganyika (bara) na wabunge wake wa majimbo kama ilivyo leo Zanzibar halafu tuna mawaziri na wabunge wa bunge Jamhuri (muungano). Hatuwezi kuwa na serikali 3 isokuwa na vyombo hivyo!
 
Mkuu wangu swala la serikali 3 halina Ubishi. Ni lazima kila serikali itakuwa na kingozi wake sasa umuite Rais, sijui waziri kiongozi, au Waziri mkuu (Premier), senator bado nafasi hizo tatu (kiongozi wa Znz, Kiongozi wa Bara na Kiongozi wa muungano)zinahitajika na watavuta mshahara sawa na marais iwe kwa jina lolote.

Kwa hiyo iwe rasimu imeacha ama vyovyote bado haiwezekani kuundwa serikali ikakosa mkuu wa nchi hiyo! ni logic tu mkuu wangu. Na pia ufahamu kila serikali itakuwa na mawaziri na wabunge wa kujaza serikali zote 3 haihitaji sayansi kutambua hilo maana tunaunda serikali inayofanana na serikali za nchi nyinginezo. Hivyo tutakuwa na mawaziri wa Tanganyika (bara) na wabunge wake wa majimbo kama ilivyo leo Zanzibar halafu tuna mawaziri na wabunge wa bunge Jamhuri (muungano). Hatuwezi kuwa na serikali 3 isokuwa na vyombo hivyo!

Mkuu Mkandara,hoja yangu kuu ni kuwa si lazima katika uwepo wa Serikali tatu kuwepo Marais watatu
 
Last edited by a moderator:
sawa lakini viongozi watatu wa serikali hizo tatu watakuwepo au sio?
Sahihi Mkuu,ndivyo itakavyokuwa.Lakini,ukubwa wa Serikali husika na matumizi yake ni maamuzi ya waunda Katiba za Serikali hizo
 
Sahihi Mkuu,ndivyo itakavyokuwa.Lakini,ukubwa wa Serikali husika na matumizi yake ni maamuzi ya waunda Katiba za Serikali hizo
wewe kama mwananchi iwe wa Bara au visiwani unafikiri uundwaji wa serikali hizi utafanywa kama unavyopenda iwe? au hao hao watarajiwa wenye nafasi zao (viongozi) watajipangia madaraka!
Kifupi nini nafasi yako ktk uundwaji wa serikali hizo?
 
wewe kama mwananchi iwe wa Bara au visiwani unafikiri uundwaji wa serikali hizi utafanywa kama unavyopenda iwe? au hao hao watarajiwa wenye nafasi zao (viongozi) watajipangia madaraka!
Kifupi nini nafasi yako ktk uundwaji wa serikali hizo?
Ni hawa hawa wa SIRI na DHAHIRI
 
Ni hawa hawa wa SIRI na DHAHIRI
Hii ndio sababu mimi napinga serikali 3 kwa sababu nawajua viongozi tulokuwa nao, wao wanafikiria maslahi yao na kuwapa serikali 3 ni kuwapa fursa sisi wenyewe kujipangia madaraka na ulaji.
Swala la serikali 3 limetokana haswa na kero za muungano jambo ambalo serikali 3 haliwezi kuwa muarobaini isipokuwa ni kutia kidonda chunvi, na umaskini huu watatumaliza.
 
Back
Top Bottom