mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,227
- 6,670
Nasema, bila kupepesa macho wala kumng'unya maneno, na kwa kujiamini kuwa hoja za upinzani zenye lengo la kumchafua Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, zimejaa unafiki, uzushi na ulaghai.
Ifuatayo ni orodha ya baadhi ya hoja hizo, ambazo pasipo na shaka ni VIOJA
1) Utawala wa kidikteta uliowanyima nafasi ya kufanya siasa: Serikali ya CCM imehakikisha hali ya amani na utulivu nchini inaimarika kutokana na hatua mbalimbali zilizochukuliwa za kuhakikisha wananchi wanapata fursa ya kushiriki katika shughuli za maendeleo bila kuwepo bugudha. Mifano ipo mingi km wawakilishi (madiwani na wabunge) waliendelea na shughuli zao za uwakilishi pasipo kuingiliwa. Au wafanya biashara ndogo ndogo wamepewa vitambulisho vinavyowapa fursa ya kuendelea na biashara zao popote nchini.
2) Maendeleo ya vitu badala ya vitu: Kuna upotoshaji wa hali ya juu, na wa makusudi, kwa maana halisi ya maendeleo ya watu (people-centred development). Serikali ya CCM imetekeleza mikakati iliyowezesha rasilimali za Taifa kutumika kimkakati na kikamilifu katika ujenzi wa msingi wa uchumi wa viwanda na ustawi wa jamii, ikiwa ni pamoja na kuandaa na kutekeleza Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2016/17 - 2020/2. Mafanikio ya utekelezaji huo ni viashiria kadhaa vinavyoonesha umasikini umepungua na ustawi wa watu umeimarika:
√ Wastani wa miaka ya kuishi kwa Watanzania umeongezeka kutoka miaka 61 mwaka 2015 hadi takribani miaka 65 mwaka 2020;
√ Umasikini wa mahitaji ya msingi umepungua kutoka asilimia 28.2 mwaka 2011/12 hadi asilimia 26.4 mwaka 2017/18; na
√ kiwango cha umasikini wa chakula kimepungua kutoka asilimia 9.7 mwaka 2011/12 hadi asilimia 8.0 mwaka 2017/18.
3) Uchumi wa nchi umeporomoka kutokana na Sera za Serikali ya CCM zilizowafanya baadhi ya wafanya biashara kufunga au wawekezaji kuondoka. CCM kwa kutambua na kuthamini sana nafasi ya sekta binafsi katika kujenga uchumi wa kitaifa na ambao ni shindani uliojikita katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda na katika kuleta mageuzi kwenye kilimo, ufugaji, uvuvi, utalii na sekta nyingine zote.
CCM imezisimamia serikali zake kuhakikisha sekta binafsi inalindwa na kuendelezwa na kwamba haki ya kila mtu, kikundi, ushirika na kampuni ya kuendesha shughuli za uchumi na biashara kwa uhuru na kwa mujibu wa sheria zinalindwa wakati wote. Hivyo basi, Serikali ya CCM imetekeleza yafuatayo:
√ imeimarisha ubora wa miundombinu na huduma wezeshi kama vile uchukuzi, nishati na mawasiliano;
√ imeweka mazingira ya urahisi, ufanisi na uhakika wa sheria, kanuni, taratibu na utendaji wa sekta ya umma katika kuwezesha shughuli za uchumi na biashara za sekta binafsi;
√ inewezesha uwepo wa rasilimaliwatu ya kutosha yenye elimu, ujuzi na maarifa stahiki hususan katika nyanja za sayansi na teknolojia.
Matokeo ya sera na mikakati hiyo ya kiuchumi ni kama:
√Pato la Taifa limeendelea kukua kwa wastani wa asilimia 6.9 katika kipindi cha mwaka 2016 - 2019;
√ Pato la wastani la kila mtu limeongezeka kutoka shilingi 1,968,965 (Dola za Kimarekani 992) mwaka 2015 hadi kufikia shilingi 2,458,496 (Dola za Kimarekani 1,086) mwaka 2018;
Yapo mengi ya maendeleo yaliyofanywa na Serikali ya CCM ambayo hakuna chama cha upinzani kinaweza kuyafanya ikizingatiwa baadhi ya hivyo vyama vimeshindwa hata kuendeleza vyama vyao km kutokuwa na ofisi za makao makuu ingawa mabilioni ya ruzuku hulipwa. Ada ya mja ni kunena, mwungwana ni vitendo.
Kwa kuwa vyama vya upinzani havina cha kuonesha ili viongozi waje waaminike, wagombea wa upinzani wanadi tu HOJA siyo VIOJA.
Ifuatayo ni orodha ya baadhi ya hoja hizo, ambazo pasipo na shaka ni VIOJA
1) Utawala wa kidikteta uliowanyima nafasi ya kufanya siasa: Serikali ya CCM imehakikisha hali ya amani na utulivu nchini inaimarika kutokana na hatua mbalimbali zilizochukuliwa za kuhakikisha wananchi wanapata fursa ya kushiriki katika shughuli za maendeleo bila kuwepo bugudha. Mifano ipo mingi km wawakilishi (madiwani na wabunge) waliendelea na shughuli zao za uwakilishi pasipo kuingiliwa. Au wafanya biashara ndogo ndogo wamepewa vitambulisho vinavyowapa fursa ya kuendelea na biashara zao popote nchini.
2) Maendeleo ya vitu badala ya vitu: Kuna upotoshaji wa hali ya juu, na wa makusudi, kwa maana halisi ya maendeleo ya watu (people-centred development). Serikali ya CCM imetekeleza mikakati iliyowezesha rasilimali za Taifa kutumika kimkakati na kikamilifu katika ujenzi wa msingi wa uchumi wa viwanda na ustawi wa jamii, ikiwa ni pamoja na kuandaa na kutekeleza Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2016/17 - 2020/2. Mafanikio ya utekelezaji huo ni viashiria kadhaa vinavyoonesha umasikini umepungua na ustawi wa watu umeimarika:
√ Wastani wa miaka ya kuishi kwa Watanzania umeongezeka kutoka miaka 61 mwaka 2015 hadi takribani miaka 65 mwaka 2020;
√ Umasikini wa mahitaji ya msingi umepungua kutoka asilimia 28.2 mwaka 2011/12 hadi asilimia 26.4 mwaka 2017/18; na
√ kiwango cha umasikini wa chakula kimepungua kutoka asilimia 9.7 mwaka 2011/12 hadi asilimia 8.0 mwaka 2017/18.
3) Uchumi wa nchi umeporomoka kutokana na Sera za Serikali ya CCM zilizowafanya baadhi ya wafanya biashara kufunga au wawekezaji kuondoka. CCM kwa kutambua na kuthamini sana nafasi ya sekta binafsi katika kujenga uchumi wa kitaifa na ambao ni shindani uliojikita katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda na katika kuleta mageuzi kwenye kilimo, ufugaji, uvuvi, utalii na sekta nyingine zote.
CCM imezisimamia serikali zake kuhakikisha sekta binafsi inalindwa na kuendelezwa na kwamba haki ya kila mtu, kikundi, ushirika na kampuni ya kuendesha shughuli za uchumi na biashara kwa uhuru na kwa mujibu wa sheria zinalindwa wakati wote. Hivyo basi, Serikali ya CCM imetekeleza yafuatayo:
√ imeimarisha ubora wa miundombinu na huduma wezeshi kama vile uchukuzi, nishati na mawasiliano;
√ imeweka mazingira ya urahisi, ufanisi na uhakika wa sheria, kanuni, taratibu na utendaji wa sekta ya umma katika kuwezesha shughuli za uchumi na biashara za sekta binafsi;
√ inewezesha uwepo wa rasilimaliwatu ya kutosha yenye elimu, ujuzi na maarifa stahiki hususan katika nyanja za sayansi na teknolojia.
Matokeo ya sera na mikakati hiyo ya kiuchumi ni kama:
√Pato la Taifa limeendelea kukua kwa wastani wa asilimia 6.9 katika kipindi cha mwaka 2016 - 2019;
√ Pato la wastani la kila mtu limeongezeka kutoka shilingi 1,968,965 (Dola za Kimarekani 992) mwaka 2015 hadi kufikia shilingi 2,458,496 (Dola za Kimarekani 1,086) mwaka 2018;
Yapo mengi ya maendeleo yaliyofanywa na Serikali ya CCM ambayo hakuna chama cha upinzani kinaweza kuyafanya ikizingatiwa baadhi ya hivyo vyama vimeshindwa hata kuendeleza vyama vyao km kutokuwa na ofisi za makao makuu ingawa mabilioni ya ruzuku hulipwa. Ada ya mja ni kunena, mwungwana ni vitendo.
Kwa kuwa vyama vya upinzani havina cha kuonesha ili viongozi waje waaminike, wagombea wa upinzani wanadi tu HOJA siyo VIOJA.