Uchaguzi 2020 Hoja za wapinzani zinaleta mashaka dhamiri zao juu ya taifa letu

Uchaguzi 2020 Hoja za wapinzani zinaleta mashaka dhamiri zao juu ya taifa letu

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
Habari,

Kwa mawazo yangu, upinzani ni upande wenye fikra, sera, mawazo na maoni mbadala wa chama kilichopo madarakani. Hivyo basi, katika nchi nyingine watu hufikiri kwenda na upinzani kwa sababu ya sera mbadala ilizonazo katika uongozi.

Hali hii ni tofauti na hapa kwetu Tanzania, watu wanaona upinzani kama dodoki la kusafishia mafisadi, wala rushwa na wengineo na mifano katika hili ipo dhahiri kabisa. Hii inaleta hofu kwa watu kuuelewa upinzani una dhamira gani kwa nchi yetu?

Tukiachana na hilo la kuwa dodoki, upinzani umejijenga katika kujenga hoja dhaifu sana. Kwa mfano kuna mmoja alipoulizwa juu ya michango ya kampeni za Lissu akaishia kujibu kwamba tayari tumeichangia CCM kwenye kodi zetu.

Hii jibu ni mtu mwenye hoja dhaifu anaweza kujibu na kwa majibu haya ni dhahiri nia ya upinzani si njema kwa taifa letu ila tuendelee kuwasikiliza na kuwapima zaidi ili tusifanye makosa ya kuchagua.
 
Cha msingi tuweke midahalo kwa wagombea uraisi wa ccm, Chadema na ACT tutajua mwenye dhamira ya kweli.
 
Jana nimewasikiliza ACT wazalendo. Sitashangaa kama act kikawa chama kikuu cha upinzani.
 
Cha msingi tuweke midahalo kwa wagombea uraisi wa ccm,cdm na act tutajua mwenye dhamira ya kweli
Mdahalo wa Tundu Lisu, Katambi anaumaliza peke yake, na Lisu hawezi pata jibu kwake.
Hatuwezi kupeleka raisi kwenye mambo ya kitundulisu.
 
ACT Wazalendo wako serious zaidi kuliko hayo Chadema!

Ndio maana mimi huwa nasema mbadala wa ccm huenda ikaja kuwa ACT
 
Uchaguzi umekosa morali sababu tume imewekwa mfukoni na chama dola, ground ikiwa fair mgombea yeyote wa ccm akisimama hata na gunia la viazi mbatata, nakuhakikishia gunia linashinda mapema tu
 
Cha msingi tuweke midahalo kwa wagombea uraisi wa ccm,cdm na act tutajua mwenye dhamira ya kweli

Mkiishiwa hoja mnakimbilia kwenye Mdahalo. Kwann hizo hoja mnazotaka kutoa kwenye mdahalo msitoe kwenye hadhira watu waelewe?

Mfano: mwingine naye kasema.

“Polisi, mnapoona umati kama huu wa Arusha, ukiamua hamna polisi wala jeshi linaloweza kuwazuia. Mkiona umma umetulia, mjue kuna viongozi wao wenye busara wanawatuliza. Lakini uvumilivi unamwisho"-; @freemanmbowetz, M/kiti wa Chadema Taifa.


Sasa najiuliza hii ni sera au chair anaamasisha vurugu na vita katika taifa letu?
 
Tumeshuhudia wizi mkubwa wa Raslimali za Watanzania, Mikataba mibovu ya sekta zote. Ufisadi mkubwa wa watawala na watu wao EPA, DOWANS, KAGODA ,IPTL,ESCROW,NK.

Wapinzani ndio wa kwanza kufichua mabaya yoote haya leo unamashaka nao???

Kweli ELIMU ELIMU ELIMU
 
CCM ndio yenye hoja za maana kwa kudanganya wananchi wake, ajira Mil 8.....seriously......zile ajira mil 1 za miaka mitano iliyopita zipo wapi?
 
Back
Top Bottom