Hongera Bondia mpya Mandonga kwa kupigana nje ya Nchi, Mabondia Wazoefu wanaogopa

Hongera Bondia mpya Mandonga kwa kupigana nje ya Nchi, Mabondia Wazoefu wanaogopa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hili jambo linapaswa kufanyiwa kazi na Viongozi wa Masumbwi Tanzania .

Zipo tuhuma kwamba mabondia wa Tanzania hawana uwezo , na huwa wanabebwa na waamuzi wa ndani kwa kuwapora ushindi mabondia wa kigeni , Hii ndio sababu kubwa ya mabondia hawa kutotaka kupigana Nje ya nchi , maana huko watachakazwa , maana Mwamuzi hatokuwa Mlundwa .

Ninao ushahidi wa bondia duni wa Tanzania Cosmas Cheka kupewa ushindi dhidi ya bondia mzuri kutoka Malawi katika pambano lililofanyika Morogoro , Cosnas Cheka alipigwa mwanzo mwisho lakini kwa Aibu ushindi akapewa yeye ! mambo kama haya nje ya nchi hayawezi kutokea , Hata pambano la Kwanza la Kidunda na Katompa , Ukweli ni kwamba Kidunda alipigwa ila Uzalendo ukatumia kumuokoa , nje ya nchi huwezi kufanya njama duni kama hiyo .

Mifano ya Matokeo ya kubebwa kwa mabondia wa Tanzania ni mingi na ya kutia aibu sana , hatuwezi yote kuiweka hapa

Nampongeza sana Mandonga kwa kupata ujasiri wa kupigana nje ya nchi na kushinda , hawa mabondia wa Kubebwa hawawezi kuthubutu .

Nakala : Chaurembo Palasa
 
Hili jambo linapaswa kufanyiwa kazi na Viongozi wa Masumbwi Tanzania .

Zipo tuhuma kwamba mabondia wa Tanzania hawana uwezo , na huwa wanabebwa na waamuzi wa ndani kwa kuwapora ushindi mabondia wa kigeni , Hii ndio sababu kubwa ya mabondia hawa kutotaka kupigana Nje ya nchi , maana huko watachakazwa , maana Mwamuzi hatokuwa Mlundwa .

Ninao ushahidi wa bondia duni wa Tanzania Cosmas Cheka kupewa ushindi dhidi ya bondia mzuri kutoka Malawi katika pambano lililofanyika Morogoro , Cosnas Cheka alipigwa mwanzo mwisho lakini kwa Aibu ushindi akapewa yeye ! mambo kama haya nje ya nchi hayawezi kutokea , Hata pambano la Kwanza la Kidunda na Katompa , Ukweli ni kwamba Kidunda alipigwa ila Uzalendo ukatumia kumuokoa , nje ya nchi huwezi kufanya njama duni kama hiyo .

Mifano ya Matokeo ya kubebwa kwa mabondia wa Tanzania ni mingi na ya kutia aibu sana , hatuwezi yote kuiweka hapa

Nampongeza sana Mandonga kwa kupata ujasiri wa kupigana nje ya nchi na kushinda , hawa mabondia wa Kubebwa hawawezi kuthubutu .

Nakala : Chaurembo Palasa

Mtu kazi… anakwambia yeyote wa uzito wangu napitanae, hakuna unyonge
 
Kuna somo kubwa sana kwa Vijana kujifunza kwa Mandonga.

Ni mtu kazi asiyekata tamaa wala kuogopa
 
Mandonga ana miaka 49 upya wake uko wapi?
 
Utani utani tu, unashangaa Mandonga mtu kazi anaenda Marekani/Uingereza kwa ajili ya pambano la ngumi za kulipwa.

Jamaa amekuwa maarufu ghafla bin vuu.
 
Mandonga ana ujasiri na anajiamini kama namuona Mohammed Ali [emoji1] kwa mbwembwe na anapiga haswa

Huwa sifuatilii ngumi za nyumbani ila kwa huyo jamaa acha awachakaze
Kabla hajakupiga ngumi anakupiga kwa maneno

Big up Mandonga piga sana
 
Wakati wenzake wanaogopa yeye sasa anahitajika Uingereza
 
Back
Top Bottom