Hongera Bwana Othman M. Bawaji na Amri M.Bawaji kwa kuturudishia jarida pendwa la Sani

Hongera Bwana Othman M. Bawaji na Amri M.Bawaji kwa kuturudishia jarida pendwa la Sani

Leak

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2012
Posts
52,916
Reaction score
43,505
Wasalaam.

Wanajamvi bila shaka bado wengi wetu tuna likumbuka jarida pendwa la Sani:

Sani ni mmoja ya majarida yaliyo jizolea umaarufu hapo nyuma na bila shaka kila mtu hakupenda kukosa kila toleo. Ndug AMRI.M.M BAWAJI na wenzie wameamua kurudisha tena hule uondo wa jalida la sani na hawa ni wabunifu sana kwenye story na mpangilio wa habari zao na wanajua kuvutia sana wasomaji na kuwafanya wasitake kukosa toleo lijalo.

Ubunifu wao kwenye uandishi wao na mpangilio wa matukio unanifanya niendelee kuamini hakuna jarida la burudani zuri zaidi ya SANI nap engine ni kutokana na uwezo na ubunifu wa wahariri wao na waandishi wa vitu vipya hasa vichekesho na hadithi za kusisimua.

Nimefurahishwa sana na ujio mpya wa jarida hili la sani na ukizingatia nilikuwa napenda sana zile match za BORN TOWN NA BUSH STARS bila kusahau vituko vya sokomoko na LODI LOFA kwakweli humu kumejaa ubunifu ambao siwezi jutia kulinunua.

Mimi huwa najiuliza huyu jamaa anaye weka maneno kwenye match ya Born town na Bush stars huwa anafikiri nini? Yani huwezi acha kucheka aisee tukija kwenye uchoraji wa watu na matukio ndio usiseme.

Kwakweli Bwana Bawiji na timu yako hongereni sana kwa ubunifu mzuri na kurudisha hili jarida.

Karibuni wana jamvi.
 
Daah safi sana,wahusika watakuwa ni walewale?,Dk pimbi.mzee sukununu,lord lofa,madenge na baba madenge,Betina na wengineo?wasisahau football match,na wajitahidi wapate mchoraji mzuri kama ilivyokuwa kwa Katembo criss....nawasubili.
 
Bora limerudi daah vile vihadithi Pimbi. Lodilofa. Betina na Zena. Wale mapacha all in all kwenye zile mechi za town na bush stats lol
 
Daah safi sana,wahusika watakuwa ni walewale?,Dk pimbi.mzee sukununu,lord lofa,madenge na baba madenge,Betina na wengineo?wasisahau football match,na wajitahidi wapate mchoraji mzuri kama ilivyokuwa kwa Katembo criss....nawasubili.
Limetoka leo na wahusika ni wale wale na linauzwa 3000 story za humo ni noma me nimesha chukua nakala.
 
Bora limerudi daah vile vihadithi Pimbi. Lodilofa. Betina na Zena. Wale mapacha all in all kwenye zile mechi za town na bush stats lol
qn of sheba zote zipo na maandalizi ya match kati ya Born town na bush stars ya meanza na wako mazoezini ni full vituko kuna sehemu born town wanafanyia mazoezi juu ya goli hahah
 
Last edited by a moderator:
Hivi la Sanifu litarudi lini, nilikua nalipenda sana hasa kwenye utabili wa nyota na katuni ya Mkapa,ndani ya nyumba, bingwa wa rivasi, maprosoo bingwa wa matanuzi bila kummsahau na Tolu.!!!
 
Daah safi sana,wahusika watakuwa ni walewale?,Dk pimbi.mzee sukununu,lord lofa,madenge na baba madenge,Betina na wengineo?wasisahau football match,na wajitahidi wapate mchoraji mzuri kama ilivyokuwa kwa Katembo criss....nawasubili.

Dah,
Umenikumbusha Mchoraji JOHN KADUMA (R.I.P), yaani huyu Katembo ingawa ni mzuri but pale alikua anasubiri!!
 
Hivi la Sanifu litarudi lini, nilikua nalipenda sana hasa kwenye utabili wa nyota na katuni ya Mkapa,ndani ya nyumba, bingwa wa rivasi, maprosoo bingwa wa matanuzi bila kummsahau na Tolu.!!!

Hapo kwenye Tolu malizia kabisa USITAKE NCHEKE!!
 
qn of sheba zote zipo na maandalizi ya match kati ya Born town na bush stars ya meanza na wako mazoezini ni full vituko kuna sehemu born town wanafanyia mazoezi juu ya goli hahah

Mshambuliaji hatari wa kutumainiwa wa Bush Stars MZEE MEKO Yupo?

Au kashastaafu?
 
Last edited by a moderator:
Daah safi sana,wahusika watakuwa ni walewale?,Dk pimbi.mzee sukununu,lord lofa,madenge na baba madenge,Betina na wengineo?wasisahau football match,na wajitahidi wapate mchoraji mzuri kama ilivyokuwa kwa Katembo criss....nawasubili.

Bila ya kumsahau mzee kifimbo cheza kwa mbaali anasumbuana na wale madogo...
 
Mshambuliaji hatari wa kutumainiwa wa Bush Stars MZEE MEKO Yupo?

Au kashastaafu?
Hahaha Shark mzee meko yupo na safari hii wamekwenda kupiga kambi kigoma na bush stars hawa kocha hivyo Meko ndio kachukua majukumu ya kuwa Kocha na mazoezi yameanzia ziwani juu ya mtumbwi wachezaji wanaambiwa wapige dana dana na wahakikishe mpira hauanguki kwenye maji ni vituko vitupuu
Mazoezi ya kukwepa faulo ndio komesha aiseee daaaa.....
 
Last edited by a moderator:
Mbele lina habari za udaku au? maana kuna gaazeti hili la sani wanaandika udaku?
 
Back
Top Bottom