Hongera JK kwa kututoa katika Umaskini duniani! ila bado ....

Sawa, Bajeti ya tanzania inatokana na matumizi, elewa kwamba budget sio mauzo ya Taifa lakini kama tunapata share ktk miradi yetu bank zitatupa mtaji wa kuchimba dhahabu kwa kutumia credit ya hao Barrick. Ndivyo walivyofanya Botswana na nchi nyinginezo..Ebu jiulize inakuwaje Bank za dunia zinaweza kutupa mikopo na asilimia 45 au 30 ya bajeti yetu kwa matumizi ya ujenzi wa miundombinu kwa makubaliano ya kulipa interest bila ushuhuda wa fedha hizo kuzalishwa lakini Bank hizo hizo watunyime billioni 600 kwa biashara inayoonyesha faida. Mkuu ni bank hizo hizo zimeweza kuwapa barrick billioni 600 bila kuwa na dhahabu mkononi watashindwa vipi kutupa sisi wenye dhahabu tukishirikiana na Barrick!..

Sema mfumo wenyewe ndio unatugandamiza sisi, mfumo ambao unatumika kwao wakitumia mashirika yao wanataka kuutumia kwetu ambao hatuna mashirika yale yale. Leo hii Barrick wakichimba dhahabu Canada kuna tofauti kubwa sana ya kimapato na mafao baina yetunna canada kwa sababu kila mauzo ya Barrick yanaingia ktk bank zao, mzunguko unakuwepo ndani na mikopo itatolewa kwa wafanyabiashara wengine, mishahara matumiz ya manunuzi na kadhalika lakini kwetu sisi Barrick wanakuja na kila kitu kutoka nje hadi accounts zao. Tunachofaidika sisi ni kiduchu kabisa labda hiyo mishahara na umeme maanake hata mafuta wanaleta yao nahayalipiwi kodi. karibu kila kitu wanachonunua Barrick hakina kodi sisi tunafaidika vipi na mauzoi ya Barrick kama sii hiyo ruzuku tu?
 
Marekani kwa sasa ukiwa na mshahara wa $20,000 kwa mwaka na una familia ya watoto wawili unaishi kwenye kile wanaita poverty level.
Ukiwa na mshahara wa $11,000 na unaishi peke yako vivyo hivyo.

Sawa sawa na Tanzania kuna watu wana pato la $100,000 kwa mwaka, kuna wenye kupata pato la $100 kwa mwaka lakini average ni $1,410 kwa mwaka. Unequal distribution of income is everywhere kama alivyosema Herman Cain (Mgombea wa republican mweusi) haingii akilini wewe hufanyi kazi halafu unataka kuwa sawa sawa na mtu anayeamka saa 9 usiku kwenda kujitafutia chakula. However, our country relative economic performance with respect to other countries is far better off na kwa hapo JK nampongeza. Tulikuwa tunashika mkia leo tuko wa 50 kutoka mkiani sio kitu cha kubeza hata kidogo.
 
Wow!.. slow down mkuu wangu unanipeleka puta sana kama Bacelona!... sikiliza nijuavyo mimi miaka ya Nyerere hawa UN hawakuwa na data kamili za uchumi wetu lakini maadam wewe umeonyesha tulikuwa na GDP per capital 386 Kenya walikuwa na 337 na Zaire walikuwa na 313 mwaka huo...Tanzania ilikuwa ya ngapi nadhani unaweza kuipata tukifanya utafiti mzuri lakini nakuhakikishia tulikuwa nafasi nzuri zaidi ya wewe unavyofikiria. Licha ya hivyo nimeshakwambia haya ni makuzi ya kimwili yaani kama mwaka 1980 tulikuwa foot 4 leo hii tumeongezeka na kuwa foot 6 haina maana tuna afya nzuri kuliko Kenya ambao wana urefu wa foot 5 na nusu. Wewe unapima urefu kama maendeleo ya kimakuzi nasi tunakwambia makuzi ya mwili hayana maana mtu huyo ana Afya nzuri zaidi..
 
Economic development matters more to statisticians and economists, not the common mwananchi. They need human development, that why the GDP rose while his votes fell.

1) Who is the common and who is the not so common mwananchi?

2) Human development, you mean as in their brains?

3) What has vote got to do with statistics if it "matters more to statisticians and economists"?
 

Sasa mkuu hapo tatizo tunarudi kule kule mipango mibovu pengine. Kwani why turuhusu wasilipe fueld duty ? Pengine kiundani zaidi utakuta it goes down kuwa hatuwekezi kitu katika uchimbaji hivyo kupoteza negotiating power. Our only investment is land ni sawa sawa na wale wenye viwanja kariakoo wanaokubali wawekezaji kujenga magorofa na matokeo yake hawana jinsi isipokuwa kukubali makubaliano ambayo mmiliki hatafaidi labda wajukuu zake au watoto wake.

Barrick wanatakiwa walipe kila kitu kwani wanapata faida kubwa, na wanatakiwa kuwepo nchini kwani tunawahitaji kukuza pato la nchi.
 
Ningependa pia kukumbusha kwamba, viashiria vya uchumi kama vile total GDP, per capita income (PPP) vimekubalika kimataifa kwa kusudi moja kubwa na la msingi. Ni kuwezesha ulinganifu wa uchumi wa mataifa mbalimbali duniani. Ndiyo maana hata wewe mtoa mada hiyo ukaongelea Tanzania kuwa karibu na Kenya katika kiwango hicho cha per capita income (ppp) kwa two steps. Hata hivyo, linapokuja suala la kupima kuimarika kwa uchumi wa kila mmoja ndani ya nchi yetu ama yeyote, kiashiria hicho hapo juu hakiwezi kutumika tena.

Hivyo basi, viashiria vinavyohijika kupima maendeleo ya kijamii ndani ya nchi yatokanayo na kukua huko kwa per capita income (ppp) ni vile vinavyohusika na kuona mgawanyo wa pato hilo la taifa/income distribution inaendaje. Huduma mbalimbali za kijamii na hali ya ajira ni viashiria muhimu sana inapokuja kutazama hatua hiyo ya mgawanyo wa pato/income distribution.

Kupitia UNDP (Human Develoment Index), viashiria muhimu vya kujua kuimarika kwa huduma za kijamii ikiwa ni matokeo ya ukuaji wa uchumi iliyokubalika kimataifa na mataifa hupimwa kwa ulinganifu wa viashiria vitatu (elimu, afya/life expectancy, uelewa wa kusoma na kuandika/literacy) kuona nchi fulani iko wapi. Hivyo basi, mtoa mada hii alitakiwa atuletee pia takwimu za viashiria hivyo ili tuweze kumpongeza mzee Kikwete ama la. vinginevyo tunajidanganya kama tutaishia kupongeza Rais wetu kwa kigezo kimoja cha kukua kwa per capita income.
 
Hivi umenipata kweli maana naona kama hunielewi vile.. Uwekezaji Kariakoo leo hii mwenye nyumba yaani kiwanja anachukua asilimia 30 hadi 35 wakati mwekezaji anachukua asilimia 65 hadi 70 ya pato la mauzo baada ya ujeniz na kupanginsha. Wengine wanafanya mwekezaji anajenga ghorofa 10, tatu za mwenye nyumba na saba za mweklezaji..Tena basi siku hizi imefikia hadi kupeana miaka unawekeza ktk ujenzi na kumiliki kwa miaka 10 baada ya hapo nyumba inarudi kwa mwenye kiwanja..Kwa nini sisi tunashindwa kufanya (option yeyote ile) hivyo na wawekezaji wa nje Kitaifa?

Hakuna sababu ya kukubali kodi pakee kwa sababu wewe na mimi hatuwezi kwenda Marekani tukataka kuwekeza pasipo kuwa wahamiaji au raia. Wanahakikisha wanakufunga kamba mguuni kwanza na unafungua account kwao hata uwe unauza nyanya. Hiyo dhahabu ndio hutaichima hata kama una mtaji wa Mubarak na mitambo ya ajabu gani. Mfano mdogo, kumbuka tu Wajapan walikuwa wakiuza magari yao yakitengenezwa Japan na kuuzwa Marekani, waakawaambia hapana! biashara hiyo imekwisha.. ni lazima hayo magari wayatengenezee hapo hapo Marekani na mfungue Makampuni hapa ya uuzaji... Yote hii ni kutazama Afya ya uchumi wa nchi na sii makuzi ya mwili..

Haya ndio ameyakataa Chavez na leo hii wanamtafuta kwa kila hila, ndivyo alitaka kufanya saadam na Ghadaff hawa wote ni viongozi waliopinga mfumo wa ukolonimamboleo na yamewakuta. Sema tu sisi hatuna ujasiri wa kusimama na kufanya kweli. Mkapa alijaribu kuomba sana ktk mikutano ya kimataifa hizi nchi za G8 watushirikishe nasi lakini kwao haiwezekani inatakiwa moyo na ushenzi kama wa mwarabu. Kwa nini Saudia. Qatar, Bahrain na nchi za kiarabu wanafaidika na mafuta ni kwa sababu Mali ni ya Sultan sii ya Taifa wala mwekezaji wa nje, hivyo hawa wawekezaji wanalazimika kuingia Ubia na Sultan ambaye ndiye mwenye account ya Taifa!..Ni ujanja fulani umetumiwa dhidi ya Ukoloni mamboleo yaani Sultan naye anakuwa kama wao lakini mauzo yanarudi kwa Waarabu ndio maana unaona wanafanya maajabu bila akili ya darasani bali akili ya biashara.
 
ki2 cha mpongeza jk ni kuwa mtanashati na tabasamu lake kwenye mambo ya uchumi hayumo.He is economically undefined afadhali na waliomtangulia jkn-mjamaa halis,mwinyi-ruhsa na ben-kubana matumizi

"Year","Tanzania"
"1999","550"
"2000","710"
"2001","610"
"2002","630"
"2003","600"
"2004","700"
"2005","700"
"2006","800"
"2007","1300"
"2008","1300"
"2009","1400"
"2010","1400"

Compare ukuaji kuanzia 2005 alipochukuwa Kikwete na kabla yake kisha ulete hoja ya nani zaidi.
 
Bibie kama unakumbuka vizuri, tazama pia makuaji hayo na bei ya dollar moja utakuta kwamba kinachoelezwa hapo ni sawa na kusema exchange rate ya dollar moja toka mwaka 2000 hadi leo ni kiasi! gani tena basi zimepungua ilitakiwa zionyeshe 2010 figure iwe 1,600..Hivyo tunazungumzia dollar moja ile ile ya mwaka 200 hadi 2010.
 
Tanzania Shilling Falls a 3rd Day on Manufacturer Dollar Demand BusinessWeek - 5 hours agoBy David Malingha Doya Oct. 6 (Bloomberg) -- Tanzania's shilling
depreciated for the third day as manufacturers
increased demand for dollars. The currency of East
Africa's second-biggest economy lost as much as
0.8 percent at 1687 per dollar, ... LIVING HISTORY: More people in the city, more trouble The Citizen Daily - 10 hours agoAt independence, mainland Tanzania had a population of around
eight million. The figure has since risen five-fold, if
the 10-yearly head count was properly conducted
and superstitious parents did not hide any
children from the enumerators. ... More bread makers apply for TBS standard certification IPPmedia - 10 hours agoAt least 40 percent of owners of bakeries in Dar es Salaam have shown
interest in having their products tested and given
a mark of quality. Speaking to this paper in an
interview in Dar es Salaam recently. Tanzania
Bureau of Standards ... Tanzania: Human Trafficking Problem Grows in Dar es Salaam AllAfrica.com - 7 hours ago Trafficking in human beings has become a global problem which affects
every region and is considered to be the fastest
growing form of organized crime and the largest
transnational crime profit source. According to the
Anti Trafficking Unit Desk of the ... Tanz
 

Kuna article moja,

The social impact of Adjustment in Tanzania in the 1980s. Economic crisis and Household survival strategies. by Mahmood Meskoub namnukuu.

"
In the ranking of the world's poorest countries, the position of Tanzania changed dramatically in the 1980s. It dropped from the 14th poorest country in 1982, with a GNP per capita of $280, to the second poorest in 1990, with a GNP per capita of $110. A more telling piece of evidence of the deteriorating economic conditions of the masses of Tanzanians is the declining growth of the real GDP per capita in the 1980s. Whilst for most of the 1960s and 1970s the real GDP per capita was growing at an average annual rate of 1.5-1.9 per cent, it registered a negative annual growth rate of 2 percent in the 1981-86 period. (Maliyamkono and Bagachwa, 1990, World Bank, 1984, World Bank, 1992) It was during this period that the Tanzanian government started negotiations with the International Monetary Fund (IMF) and the World Bank (WB) leading to the adoption of a series of structural adjustment and economic recovery programmes in the 1980s. The social impact of these programmes on Tanzania is the subject of this article. "

Taarifa zaidi ya kuongezea katika kumbukumbu yako. Tanzania iliwahi kushika namba 2 kwa umaskini duniani.
 
So unatuambia JK tusimpongeze katika hili? Nafikiri utakuwa mkosaji wa shukrani. Hebu chungulia tena hizo data kipindi cha mwinyi GDP per capital ilikuwa baina 400-600 (sehemu ambayo Zimbabwe, Congo wapo sasa hivi). Mkapa GDP per capital income ilikuwa baina ya (600-1000) which is commendable. JK from 2005-2011 ni baina ya (1000-1400 ) je haikutoshi kumpongeza kwani yuko sawa sawa na mkapa kwa ukuaji wa uchumi kwa kipindi cha miaka 4. Tuwe watu shukrani wakuu sio kubeza kila kitu kwangu mie haya ni mafanikio mwanauchumi yeyote ayasifu.

Nahitaji kuelimishwa zaidi juu ya uhusiano uliopoa kati ya tarakimu na asilimia zake, kwa sababu inaonesha kwa kikwete tarakim ni kubwa(1400) lakin % iko chini (5%) compare to Mwalimu's tarakimu ambozo ni chini ya 400 ina 7%
 
Nahitaji kuelimishwa zaidi juu ya uhusiano uliopoa kati ya tarakimu na asilimia zake, kwa sababu inaonesha kwa kikwete tarakim ni kubwa(1400) lakin % iko chini (5%) compare to Mwalimu's tarakimu ambozo ni chini ya 400 ina 7%
 

Ikiwa ukuaji wa uchumi wa TZ tuuangalie kwa kutazama rates za shilingi yetu dhid ya ile ya Marekani, so tukitaka kuangalia ukuaji wa uchumi wa Marekani tutalinganisha na currency ya nchi gani?! Tangu lini benchmark ya ukuaji wa uchumi ikawa ni exchange rate?! I knw kwamba wengi tunapotaka kuangalia ukuaji wa uchumi wetu huwa tunaangalia xchange rate ( TZS v/s US$) but this's economically very wrong. ningekuelewa endapo unge-keep into consideration suala zima la inflation rate na sio vigezo vya xchange rates! tatizo la uchumi ni kwamba kila mtu anajitia mchumi na matokeo yake tunaishia kutumia weak indicators!!!! strong currency doesnt always reflect the stability of national economy na ndio maana wakati wa Nyerere TZS ilikuwa na high value ingawa uchumi ulikuwa very poor ingawaje wapo wanao-quote hali hiyo kuwa tulikuwa na strong economy! Likewise, US $ kila wakati inashuka dhidi ya Euros, then wht can we say abt USA and European Economy?! Wapo watakaosema kwamba USA economy is under recession; then wht abt Kenyan economy as compared to Japanese economy ambapo u need more Yen to have just a Kenyan Shilling?!
 
Hapa mkuu ni kwamba inachukuliwa hela ya Manji+Rostam+Mengi+Bakrhesa+Ridhiwani+Lowasa+hela za matajiri wote+vijisenti vyako+sufuri za walalahoi wote wa tz then wanagawanya kwa idadi yao. wazungu wanaiita aggrigate economic index number. hapo ndo unapata hii $1,400.
 
Samahani nilitoka kidogo, well inaonyesha bado huelewi hata kidogo..Tuseme kweli Tanzania iliwahi kuwa maskini na ya pili kutoka chini kwa sababu hiyo S110 per Capita lakini kweli tuliuza sisi kiasi kadhaa na kuufanya huo mgao, tofauti na leo tuko ranked 25 na GDP per capita ya 1416 lakini hatukuuza sisi mali hiyo wala sii yetu ila imetokana na sisi.

Nitarudia tena kusema kama wewe unauza nyanya na pato lako ni Tsh 100,000 kwa siku, utaonekana maskini kuliko yule mpishi wa ChefPride anayeuza kila siku 500,000 lakini mauzo sii yake na hupewa Tsh 10,000 kwa siku..pato analotakiwa kulizungumzia huyu mpishi ni Tsh 10,000 anayopeleka nyumbani kwake kama unataka kumlinganisha na wewe muuza nyanya..

Tofauti baina yetu na Ulaya wao wanapopiga GDP ya Marekani jua asilimia kubwa ya fedha hizo zinazunguka Marekani kweli wameuza kiasi hicho na fedha zimeingia ktk benki zao wakati sisi tunauza lakini fedha hatuzioni..Kwa hiyo ukitazama GDP yao per capita ina mahusiano makubwa na Human developmnet Index (HDI) wakati sisi kupanda kwa GDP hakuna mahusiano na HDI kutokana na mfumo duni wa ukoloni mamboleo..Kweli tunauza zaidi lakini kinachoingia mfukoni ni duni halafu bado tuna Mafisadi ambao hicho kidogo wanakimega vile vile sawa na kuwa na baba malaya anayehonga mshahara mzima.

Leo hii huko Marekani kuna watu wanaandamana kupinga Wallstreet wakitoa ujumbe kwamba ni asilimia 1 ya watu wanaomiliki Utajiri wa dunia nzima kupitia Wallstreet na kati ya hawa asilimia 99 hawajui wanauza kitu gani!... Huoni maajab ya Firaun?... Sisi wenye dhahabu huku tunahenyeka weee lakini wenye hisa zao Barrick ndio wanafaidika hali hawajui hata dhahabu hiyo inatoka wapi..

Hivyo basi pamoja na kwamba mwaka 1990 tulikuwa maskini lakini umaskini wetu uliendana na tulichokuwa nacho mfukoni hivyo kimaisha na maendeleo ya binadamu Tanzania ilikuwa ya 28 kwa umaskini! Kwa maana kwamba zipo nchi zilikuwa na GDP nzuri kuliko sisi lakini ukitazama HDI sisi tulikuwa bora zaidi yao.

Samahani naongezea kitu kidogo, nimepata hii dossier ipitie:- Bofya
 

Naona hatutaelewana. Relative performance of GDP ya Tanzania against other countries Tanzania is doing very good mkuu. Wewe sasa unataka economic performance based actual figure hilo hata wanauchumi hawawezi kulipima na maishani mwangu sijakutana na mwanauchumi mwenye kuwa na economic indicator yenye kuonyesha hali halisi ya maisha ndio maana nikakuuliza marekani GDP per capital income is $42,000 but wako wamarekani who live under a dollar a day. Hivyo hizi economic indicators haziwezi hata siku moja kutoa picha halisi ya nchi tusidanganyane kwenye hilo.

Umezungumzia Human Development Index inayopimwa na UNDP but ile inazungumzia development na sio uzalishaji na pato la mtu nchini. Kumbuka kuwa GDP ni total domestic production yaani vitu tulivyozalisha na kununulika nje au ndani ya nchi. Sasa ukiangalia UNDP development index inaangalia sekta kama afya, elimu na makazi na latest figures zinaonyesha sisi wa 22 duniani kutoka chini (2011 figures) Hata hivyo Human Development index haipimi vitu kama pato la mtanzania, pato la Tanzania kwa ujumla na kadhalika na this Index has so many flaws. Hivyo tafuta indicator nyengine Human Development Index naikataa mkuu.

Let us agree to disagree mkuu sikubaliani na argument yako kuwa GDP per capital ya 1980 ni sawa na ya 2011 but rather naona in terms of relative performance we are doing a lot better and our president deserve a credit for that!!!
 


Huu ni usiku kwetu TZ, huko uliko ni usiku ama mchana! naona kama unaota! have a nice dream!
 
Shida ndo hii, ungekuwa mwauchumi bila shaka ungeweza kutambua 386 mwk 1980 na thamani ya dola wakt huo ilikuwaje na ulinganishe na 2day's inflation rate na individuals' personal income's difference ndo ungeweza kujua ni hali gani tunayokuwa nayo. Pitia monetary value google bila shaka jibu utapata.

Acha kuhangaika na tarakimu (figures) bali thamani {value}
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…