Itovanilo
JF-Expert Member
- Jul 30, 2018
- 2,314
- 5,150
Kiukweli mpira wa Tanzania ili utoboe unahitaji kujituma, kutokata tamaa na uvumilivu wa viwango.
Kiukweli Mimi ni shabiki na pia mwanachama wa Dar es salaam Young African, naipenda sana hii timu na huwa naumia sana pindi ikifanya vibaya, lakini yote kwa yote mpira huwa na matokeo matatu.
Turudi kwenye mada, Jana nilikuwa nazurula kunako YouTube kuokoteza umbeya mbalimbali ndipo nilipokutana na interview Kati ya Ahmed Ally na Kibu. Kiukweli niseme tu nisiwe mchoyo wa fadhila, nampongeza sana huyu dogo.
Yupo humble, si mjivuni, anaonekana ana heshima ambayo kwa jinsi anavyoongea ni chachu kutoka kwa wazazi wake, Ni mpole na mwenye uwezo wa kusimulia jambo likaeleweka. Pia siyo muongo maana Kuna dot nilikuwa naunganisha nikatambua ni mkweli kwa asilimia nyingi.
Kibu ni mmoja wa wachezaji waliopitia changamoto kipindi fulani pale Simba huku akiwa anazomewa na kusemwa vibaya, hata Mimi mwenyewe pindi akiwa timu ya taifa nikiri sikuwa nampenda hata acheze vizuri vipi. Lakini kwa mtiririko wa timu ndogo ndogo alizopitia na jinsi ambavyo nidhamu na kutokata tamaa vikiwa ni silaha kwake, ndivyo vilimfikisha alipo sasa na Imani hata goli alilofunga jumapili halikuwa la kubahatisha.
Hongera Kibu, na ongeza bidii zaidi katika safari yako
Itovanilo
Kiukweli Mimi ni shabiki na pia mwanachama wa Dar es salaam Young African, naipenda sana hii timu na huwa naumia sana pindi ikifanya vibaya, lakini yote kwa yote mpira huwa na matokeo matatu.
Turudi kwenye mada, Jana nilikuwa nazurula kunako YouTube kuokoteza umbeya mbalimbali ndipo nilipokutana na interview Kati ya Ahmed Ally na Kibu. Kiukweli niseme tu nisiwe mchoyo wa fadhila, nampongeza sana huyu dogo.
Yupo humble, si mjivuni, anaonekana ana heshima ambayo kwa jinsi anavyoongea ni chachu kutoka kwa wazazi wake, Ni mpole na mwenye uwezo wa kusimulia jambo likaeleweka. Pia siyo muongo maana Kuna dot nilikuwa naunganisha nikatambua ni mkweli kwa asilimia nyingi.
Kibu ni mmoja wa wachezaji waliopitia changamoto kipindi fulani pale Simba huku akiwa anazomewa na kusemwa vibaya, hata Mimi mwenyewe pindi akiwa timu ya taifa nikiri sikuwa nampenda hata acheze vizuri vipi. Lakini kwa mtiririko wa timu ndogo ndogo alizopitia na jinsi ambavyo nidhamu na kutokata tamaa vikiwa ni silaha kwake, ndivyo vilimfikisha alipo sasa na Imani hata goli alilofunga jumapili halikuwa la kubahatisha.
Hongera Kibu, na ongeza bidii zaidi katika safari yako
Itovanilo