Hongera Ridhiwani Kikwete!!!

Nampa hongera zake ila nampa angalizo kuwa awe makini na maadili ya kazi yake.
asiikimbie siasa hata ikimtenda ila ajue kuwa rushwa ina lugha nyingi........

nimempa ushauri mara 100 hapa. mwenye jicho a afahamu.
 
NAFURAHI KUONA KATIKA LIST HII MAJINA YA WANAWAKE NI MACHACHE....NINAANZA KUAMINI KUWA JINSIA HAS SOMETHING TO DO WITH WIZI...maana wa mama wengi tu wapo kwenye positions mbalimbali lakini hawatajwi sana katika ubadhirifu....I conclude by saying that .....bora wapewe nchi

mix with yours
 

Hivi kati ya majaji wote walio kabidhiwa vyeti, ni ridhiwani tu ndo wa kupewa hongera? Hao wengine hawakustahili hongera? Naona kuna ujumbe tofauti unaokusudiwa hapa na si hongera tu.
 

Kulikuwa na mawakili zaidi ya mia moja na sitini na nane lakini magazeti yote yalicentre kwake, that was purely kupoliticise hii issue. It was not fair kwa press kumfanya yeye ni lead story kwani hakuna alichofanya zaidi ya wenziwe 168 waliopewa vyeti.

Magazeti yangepiga kelele kuhusu uhaba wa mawakili ukilinganisha na idadi ya watu Tanzania, mikoa mingine kutokuwa na mawakili kabisa, proffessional standards za mawakili, jinsi gani tumetayarisha mawakili wetu kwenda Kenya, Uganda Rwanda na Burundi ( cross border) kuliko kuhangaika na picha ya wakili mmoja out of 168 waliopewa vyeti.
 
Hongera sana Ridhiwani, zingatia haki! Mwanasheria asiyezingatia haki ni binadamu hatari kuliko binadamu yeyote duniani!

Kama baba ananyonga haki mtoto atawezaje kuzingatia haki? Baba anawalinda wezi wa mali za nchi na mwanae anaona ; ujue na yeye ataendelea kuwalinda mafisadi katika kazi hiyo ya uwakili kwani it is in their GENES to rape the national resources!! Mtoto wa nyoka ni nyoka tu hawezi kuwa panzi!
 


Kwa waanasheria wanajuwa namna huu mtihani-BAR EXAM ulivyo mgumu.....watu na akili zao huwa wanafanya hadi mara mbili au tatu kabla ya kufaulu....na majaji wako makini mno kupitisha watu credible.....sikatai inawezekana kuwa huyu basi atakuwa soo geneious such that kila siku yupo mitaani ..kwenye siasa na analala late .....yet ame seat bar exam na amefaulu....du!!!...sidhani kama mitihani itakuwa imepunguzwa makali....atakuwa geneous huyu!!!!!!!

itabidi wanasheria mumvulie kofia huyu learned fellow wenu!!!....sisi ma commoners ni vigumu ku comment lolote juu ya uhalali wowote!!
 
Na wewe uliyeleta Hongera hizi una matatizo gani kichwani?

Wengine hukuwaona? Kapata kitu ambacho huamini angeweza kukipata?

ONYO: Usiwe mtiifu kiasi hicho maana kuna watu wa aina ya Caanan Banana wanasubiri nafasi waitumie.
 
Nina wasiwasi na credibility yake; kwani nasikia huko Mlimani alikwisha pigwa disco ila mambo yakafanyika na kuonekana amefauru!!!

Mkuu Heshima Mbele Mwanamayu, Je, una hako ka ushahidi au tu-treat hii kama lame allegation?
 
huyo mwanamke wa kwanza kapiga picha na majaji kwa sababu na yeye kijana wake ni muhitimu au??
Labda kaja kama mgeni rasmi,maana kama angekuja kama mzazi mwalikwa angekaa huko na wazazi wenzie. Tatizo ni kimbelembele kwa kila kitu mpaka inachefua. Washauri wawe makini na First family maana inalikoroga ktk mambo mengi.
 
Nina wasiwasi na credibility yake; kwani nasikia huko Mlimani alikwisha pigwa disco ila mambo yakafanyika na kuonekana amefauru!!!
.
Mwanamayu, DISCO UDSM. mbona ni kitu cha kawaida, mimi pia nimesoma sheria hapo UD, nimejiunga na chuo na DIV II, wakati bila DIV 1 Sheria hupati.
Tulijiunga na vichwa vyenye DIV 1 kali toka haya mashule ya Academic na ma-international, mwisho wa siku, kuna wengi tuu walio Disco na Div I zao, na kuna wengi waliopata Upper 2nd na Div II zao.

Hata mimi binafsi niliDisco 2nd-year, na kutoka na upper 2nd mwaka wa mwisho. Kudisco Chuo, hakuna maana ndio kilaza, kuna maprofesa wazuri tuu hapo hapo chuo, vichwani akili nyingi, kwenye kufundisha ni vilaza tuu. Na kuna wanafunzi wa kawaida tuu, maksi za kawaida, ili hali ni vichwa kiukweli ukweli.

Tusihukumu watu for what they did/were, bali tuwahukumu for what they do now and in future.

Nawapongeza wanasheria wote waioukwaa uwakili, kusoma sheria ni kitu kimoja, kuwa wakili ni kitu kingine, ila kuwa wakili mzuri, ni kingine kabisa na hakina uhusiono ulikuwa mzuri vipi darasani, ndio maana mawakili wengi wazuri, wamepata pass tuu kama kina Mkono, na vile vichwa haswa vya sheria, vyenye Ist Class, kama kina Prof. Kabudi, huishia kwenye chaki ubaoni, na wakisimama mahakamani, ndio kama vile "amicus curiae", yaani friends of the court!.

Pia naomba msiwashangao, waandishi kumshobokea kijana wa Mzee, big names, makes news as well as prominance makes news, kijana ana both, silver spoon from 1st familiy, his own merit kwenye UV-CCM, sasa personal achievement as a member of the Bar from his own brain. Kati ya degree za kupewa pale UD, LL.B haipo, kila aliyesoma LL.B na kumaliza ni mwanasheria, ila sio kila aliyesoma LL.B na kuhitimu ni wakili.

Kwa hili la uwakili jamani, hongera zake mpeni!.
 

Mkuu Pasco,

Hebu fafanua maana maelezo yako yamenitatiza japo yanamake sense........ Hapo unaposema ulidsco halafu ukamaliza na maksi hizo au ulianza upya? Ulidisco au ulirudi sept 11 conference?

La Ridhiwani simo kabisa, namsikia tu magazeti busy for UVCCM huko kwenye sheria wanajuana wenyewe.
 

Mkuu umeinasa vizuri kweli!!!
Naona shughuli yote ni ya RK, miafrika bana!!!

Kwa mtu kama Justice R, kujikomba kiasi hicho ni hatari katika muhimili wetu wa judiciary!!!
 

Kweli mkuu PASCO tueleze iweje U DISCO halafu uakaendelea, au unachanganya DISCO na SUPP? mkuu Ku Supp ndio kitu cha kawaida pale UD lakini DISCO noooo! Uki DISCO we ni KILAZA tu!
 
Hongera dogo!!

Lakini uwe kweli unajua ethics za advocates, siyo unakuwa fuata mkumbo!!! Nna wasiwasi sana na kazi uliyopewa na babayo kumtafutia wadhamini!!! Haitokuingiza kwenye haya mambo kweli?
 
Kweli mkuu PASCO tueleze iweje U DISCO halafu uakaendelea, au unachanganya DISCO na SUPP? mkuu Ku Supp ndio kitu cha kawaida pale UD lakini DISCO noooo! Uki DISCO we ni KILAZA tu!

Mkuu Pasco, rekebisha hapo maana huwezi disco 2nd year na umalize kwenye chuo hichihicho!!!

Rudi fasta mkuu urekebishe......
 
kweli mkuu pasco tueleze iweje u disco halafu uakaendelea, au unachanganya disco na supp? Mkuu ku supp ndio kitu cha kawaida pale ud lakini disco noooo! Uki disco we ni kilaza tu!
ukidisco chuo kikuu manake ni home tuu, yaani hakuna disco afu tena uje umalize...either uliapply chuo upya so ukaanza tena..ila kama ulidisco na ukaja kumaliza ndo haya wanaita magumashi, mtu anadisco lakini mbinu zinafanyika, anapewa maksi masomo machache (hata likiwa moja kama litaweza kumuondosha na adha ya kudisco) then anaendelea kudunda....so mkulu pasco huwezi disco afu ukamaliza tena sijui na upper second sijui kitu gani..
 
Taaluma rahisi kabisa hapa duniani ni pamoja na ukahaba, uandishi wa habari na sheria. Hongera Ridhiwani. Kumbe ungeweza lipi sasa.
 
.
Narudia kwa msisitizo, sio kila disco ni kilaza, na sio kila anayepasua ni kichwa, kuna wanaopasua kwa kuulopu tuu au kuzifumania pepa, na kuna wanaodisco kwa matatizo megine non academic, ndio maana kuna rufaa.

Kweli nili disco mwaka wa pili, na LL.B safi tuu nikaikwa ila nimeiweka kabatini nikisubiria wakati, kwa sasa naganga njaa na issues nyingine tuu.
 

Unajisifia kudisco, wewe mzima kweli???
 
Kweli mkuu PASCO tueleze iweje U DISCO halafu uakaendelea, au unachanganya DISCO na SUPP? mkuu Ku Supp ndio kitu cha kawaida pale UD lakini DISCO noooo! Uki DISCO we ni KILAZA tu!

No disco ni disco, na supp ni supp, mbona kuna technical disco, unaapeal na linapanguliwa?. Kwa sheria za chuo si wote mnazijua, hata kama wewe ni kichwa, hujapiga paper for whatever reasons, matokea yakija, si yanakuja na desh mwisho ni disco, mtu wa disco hilo, utamuita kilaza?, unajenga hoja, unakabidhi macheti, unapigwa special exam na unapasua na kusonga mbele!.

Tatizo la Disco, ni unyanyapaa unaandamana na hilo disco kuwa kila anaepigwa disco ni kilaza, ndio maana hata mtu kukubali, umechezea disco, unaona noma. Jamani UD disco ni kawaida tuu, na linapangulika kutegemeana na unavyojenga hoja.

Wale wanaopigwa disco na kufungasha, ndio wale wanaokubali matokeo, kama unajiamini, na uwezo wako unaujua, disco ni muziki tuu kama miziki mingine, unaruka disco, muziki ukizima, unarudi darasani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…