Hongera sana Ally Kamwe kwa uungwana wako dhidi ya shabiki maandazi aliyempiga kibao Dokta Mohamed

Hongera sana Ally Kamwe kwa uungwana wako dhidi ya shabiki maandazi aliyempiga kibao Dokta Mohamed

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
390
Reaction score
1,425
Nimehuzunishwa sana na kitendo cha shabiki wa Yanga kumtandika ngumi ya uso mwanachama wa Simba Doctor Mohamed akiwa anahojiwa na chombo cha habari, shabiki huyo aliyekuwa amefuatana na Ally Kamwe wakiwa wanatoka uwanjani alimtandika kibao dokta Mohammed kufuatia Yanga kuondolewa mashindanoni.

Ally Kamwe aliangalia tukio hilo na akarudi nyuma kumuomba radhi Doctor Mohamed kwa kitendo hicho.

Nimefurahi sana kwa kitendo hicho cha Ally Kamwe. Ndugu zangu mashabiki, Yanga kutolewa leo imekuwa nongwa hadi mnapiga mashabiki kweli?

Hasira za nini, kwa mfano wewe uliyempiga kibao Doctor Mohamed unajulikana maana social media zote zimekumulika, akienda kuripoti polisi kuwa umemshambulia, amepoteza simu Iphone 16, umemvunja taya, huoni atavunja kibubu chako, hongera Kamwe umekuwa muungwana mnooooo.
 
Kuna shabiki wa utopolo nilikua nimekaa nae karibu kamtukana kocha huku macho kayatoa, "Huyu kocha si amuingize Kibu Dennis ndio dakika zake, nikamjibu kwa upole Kibu Dennis haruhusiwi kucheza huku kwani yeye yuko Simba namuona kanyweea huku akivuta punzi ndefu🤣🤣🤣
 
Jamaa kazingua sana unapiga mtu na wala hajatukana wala kuvunja sheria anaongea tena kama shabiki mstaarabu
 
Mi washkaji zangu wote ni yanga na leo nimewatania sana na hakuna hata mmoja ambaye amewahi kuchukia na kutaka kurusha ngumi we live very friendly and peacefully.

Juzi kati nilikuwa kariakoo mtaa wa uhuru kijiwe cha mwendokasi nimewatania sana wana fulani wa yanga na wala hawaja catch feelings though mi ni mbavu nene nanyanyua sana vyuma vizito labda inanisaidia.
 
Yule sio shabiki ni baunsa wa Yanga anaitwa Twalibu. Huyo jamaa kazoea kupiga raia pindi Yanga wakifungwa akikukuta unahojiwa uwe shabiki wa Yanga au timu nyingine anakulamba makofi. Yanga wacha waendelee kumlea
 
Yule sio shabiki ni baunsa wa Yanga anaitwa Twalibu. Huyo jamaa kazoea kupiga raia pindi Yanga wakifungwa akikukuta unahojiwa uwe shabiki wa Yanga au timu nyingine anakulamba makofi. Yanga wacha waendelee kumlea
Anaangalia na wa kuwapiga, aje kwangu mbona atajuta aisee
 
Yule sio shabiki ni baunsa wa Yanga anaitwa Twalibu. Huyo jamaa kazoea kupiga raia pindi Yanga wakifungwa akikukuta unahojiwa uwe shabiki wa Yanga au timu nyingine anakulamba makofi. Yanga wacha waendelee kumlea
Kumbe huyo mvuta bangi ndio alimpiga pia shabik mwingine wa yanga aliekua anahojiwa
 
TUKIWAAMBIA KUSHABIKIA SANA SIMBA NA YANGA ZINARUKA NA UNAANZA KUWA MWEHU MNABISHA.

KISA MPIRA WATU WANAPIGANA NGUMI ZA USO, HAWAONI THAMANI YA KICHWA, MACHO,UBONHO NK...

MUNGU AWASAMEHE.
 
Back
Top Bottom