Nimefuatilia utangazaji wako kwenye kipindi chako cha PPR kwenye wiki ya ubunifu.
Nimeuona umahiri wako. Kama kawaida nimefurahia utangazaji wako
Hongera sana Bwana Paschal.
Mkuu
DENAMWE , asante sana, hapa hapa unaponiona ujue ni tayari nimeisha staafu utangazaji rasmi, kwa sasa mimi ni mtangazaji wa kujitegemea kwa kujitolea tuu, walionifaidi ni wale walioniona zamani nikiwa newsroom na vipindi vyangu vya Mada Moto on DTV, Kiti Moto, on DTV na ITV na Ulingo wa Siasa on TVT, vilikuwa moto!.
Endelea kufurahia vipindi vya wiki ya Ubunifu
Maonyesho haya yalikuwa ni Maonyesho ya siku 5, kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa. Kila siku niliandaa kipindi kimoja cha 30 minutes program ambacho kinarushwa katika vituo 5 vya TV, TBC, ITV, Star TV, Channel Ten, na Azam TV.
Vipindi vyangu nafanya bure kwa kujitolea, kufanya Production bure, halafu wahusika wanachangia gharama za airtime kule kwenye TV husika.
Kufuatia sasa mimi kuwa ni msataafu wa kwenye media, nimejitolea kuwafundisha bure, Watanzania wenzangu wenye vipaji vya utangazaji
Je, Una Kipaji cha Utangazaji? Jinsi ya Kujiajiri Utayarishaji na Utangazaji Vipindi Vyako vya TV
Na kuna wakati huko nyuma, niliishauri JF Tuanzishe livestream TV yetu
Vipindi Maalum vya JF kwenye TV: Naomba Maoni Yako! lakini kufuatia members wengi wa JF kutumia majina vificho na majina bandia, members wakaligomea wazo hilo!.
Karibu sana nikuhudumie
Pasco.