Hongera sana rais wangu Kikwete. Umetudhihirishia utanzania wako wa kweli

Hongera sana rais wangu Kikwete. Umetudhihirishia utanzania wako wa kweli

Major

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2007
Posts
1,865
Reaction score
2,453
Roho yangu ni ngumu kuliko ninavyoweza kuielezea. haswa kwa masuala yanayohusu nchi yangu Tanzania. couse nilijua siku njingi kuwa tanzania ndiye mama yangu mpendwa, na sikupenda abadan kuikosea ama mtu aikosee nikiwa hai.Yametokea mengi sana ktk nchi hii mabaya na kila mtu mwenye akili timamu ameyajua. but, nijuavyo mimi kila kitu kibaya cha muda mrefu, lazima kinakuwaga na misingi mibaya iliyojengwa kwa muda mrefu.na kuking'oa inahitaji muda mrefu sana, na tena kinahitaji umakini mkubwa na roho ngumu sana.

Nafurahi sana na furaha isiyo na kifani leo hii kwa kutambua kwamba Rais wetu tena kuanzia leo nitakuwa namuita mpendwa wetu JAKAYA MRISHO KIKWETE Kuamua kwa moyo wake wa upendo kwa watanzania, kuamua kuwapa Watanzania nchi yao ili waweze kujitawala na kujiamulia mambo yao wenyewe.ki demokrasia. Mungu ambariki na ampe afya na maisha marefu.

Kitendo cha yeye kama raisi, kuruhusu kutungwa kwa KATIBA MPYA jambo hili siyo kitendo kirahisi kama watu wanavyofikiri kwa sababu, ni kwamba tangu tulipopata uhuru mwaka 1961, ni kama bado tulikuwa tunawaliwa bila ya sisi kujua, kwa kuwa kujitawala kwetu ilikuwa ni kwa mujibu wa sheria walizotuwekea wazungu.

Angeweza kwa mamlaka makubwa aliyo nayo kulikataa jambo hili, na hakuna ambaye angejaribu kama siyo kuthubutu kumwuliza kwa nini. lakni kwa upendo na uzalendo mkubwa alionao kwa nchi yake, ameamua rasmi kuutupilia mbali ukoloni.

Binafsi nimekushukuru mno. na najaribu kufikiri pengine hii ndiyo ile ahadi uliyowahi kutuahidi ya kwamba utakuja kufanya jambo ambalo hatutakaa tukusahau. kwa hiyo kama una jambo lingine ni sawa, lakini kwa hili mimi sintokaa nikusahau. MUNGU AKULINDE TENA NA TENA DAIMA
 
utendaji wake, uvumilivu wake, kuongea na watu wote, kujali walio chini hasa maskini ndio sifa zake kuu...
 
[h=3]Ngeleja ammwagia sifa JK - katekeleza ahadi zote Sengerema[/h]

Mgombea pekee wa Ubunge jimbo la Sengerema wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Madini amemmwagia sifa kedekede Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete alipokuwa Sengerema kuomba kura kutetea kiti cha urais tiketi ya CCM.

Baadhi ya maeneo aliyoyataja Mh Ngeleja ni kama ifuatavyo:
1. Ujenzi wa barabara ya kwenda Geita, ambayo imekamilika kuanzia Wilaya hii ya Sengerema. Ujenzi wa kuunganisha barabara nyingine kama ile ya kwenda Buchosa kwa kiwango cha lami inaendelea. Barabara nyingine zilizokamilika ni ile ya Misungwi.

2. Juhudi za kuunganisha Mwanza na nchi jirani kupitia kiungo cha Busisi na Bukongo zimemalizika. Pia juhudi za kuunganisha maeneo mbalimbali ya Mwanza kuvuka ziwa nazo zimefanyika na sasa kuna kivuko cha MV Misungwi. Pia ukarabati wa Kivuko MV Sengerema umekamilishwa na sasa Sengerema ina vivuko viwili.

4. Barabara nne kuu za kuingia na kutoka Sengerema zimejengwa kwa kiwango cha lami na hivyo kurejesha usafiri wa mabasi yaliyopotea miaka 20 iliyopita sasa umerudi.

5. Kwenye upande wa elimu, 2005 Sengerema ilikuwa na shule sita tu na sasa kuna shule zaidi ya 21 za sekondari. Sekta ya elimu imepewa kipaumbele sana kwenye jimbo la sengerema kwa juhudi za Mheshimiwa Rais Kikwete.

6. Vituo vya afya vimejengwa na huduma ya afya imeimarika, yote hayo ilikuwa ni jitihada za Mheshimiwa Rais na Serikali ya Awamu ya Nne.

7. Mradi wa Umeme - Jimbo la Sengerema na lile la Buchosa tuko kwenye mpango wa MCC ambapo majimbo haya mawili yatawaka taa muda si mrefu. Utaratibu wa kumpata mkandarasi aliyeshinda tenda umeanza na ataanza kutekeleza mpango huu mkubwa muda si mrefu. Pia kwenye umeme tuna mradi mwingine unaofadhiliwa na serikali wa kuleta umeme vijijini REA.

8. Maji: Suala la maji limesumbua sana wakazi wa Sengerema, lakini viongozi wa Wilaya wameamua kusimamia fedha za utekelezaji wa mradi huu ili kuhakikisha tatizo hili litatuliwe.

Mwisho Mbunge wa Sengerema Mh. Ngereja amemshukuru Rais Kikwete kwa kumpa dhamana ya kuongoza Wizara ya Nishati na Madini kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita. Ameeleza wana Sengerema kwamba amewaamini sana wao ndio maana amempa yeye madaraka hayo makubwa na nyeti.

Wakazi wa Sengerema walimsindikiza Mbunge huyo kijana kwa nderemo na vifijo huku wakiahidi kumchagua Rais Kikwete na wabunge na madiwani wote wa CCM kwa asilimia mia mbili!
 
Zitto: Kikwete ni Rais wa ajabu

Tangu June 3, 2013, na | Imesomwa mara 157 | Haina maoniNa Anicetus MwesaMBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), amesema Rais Jakaya Kikwete ni mtu wa ajabu na kueleza kuwa kama si uvumilivu wake nchi ingekuwa katika machafuko makubwa.Zitto ametoa kauli hiyo juzi, wakati akizungumza katika Kipindi cha Makutano kinachorushwa na Redio Magic FM ya jijini, Dar es Salaam ambapo alitakiwa kuelezea kipindi cha uongozi wa rais huyo ambaye amebakiza miaka miwili madarakani.Akijibu swali hilo, Zitto alisema kiongozi huyo wa nchi anapaswa kuheshimiwa kutokana na uamuzi wake wa kuruhusu uhuru wa maoni tofauti na ilivyo kwa viongozi wengi duniani.Mbunge huyo alisema, huchukia watu wanaposema, Rais Kikwete ni dhaifu na kuwataka kutotumia vibaya uhuru wa kutoa maoni.“Naomba nisieleweke vibaya, lakini ukweli ni kwamba, Rais Kikwete ameacha kiasi kikubwa uhuru wa watu kutoa maoni. Sasa rais anaweza kutukanwa lakini yeye hachukii. Ni vema wananchi wakaacha kutumia vibaya uhuru huo.“Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi kwamba nchi ingekuwa katika machafuko makubwa,” alibainisha Zitto.Pia alimwagia sifa, Rais Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa kimataifa na kuwezesha katika kipindi kifupi viongozi wawili wa mataifa makubwa kuja nchini.
“Rais ame balance (ameweka uwiano sawa) wa uhusiano wa kimataifa. Tunashuhudia ndani ya miezi mitatu marais wawili wanakuja nchini yani Rais wa China, Xi Jinping ambaye alikuja mapema mwaka huu na Rais wa Marekani, Barack Obama anayetarajia kuja nchini, Julai Mosi mwaka huu,” alisema mbunge huyo.
Mbali na sifa hizo, alimtahadharisha rais kuwa anapaswa kuwa makini na watu aliowaita wafaidhina ambao wanateka watu maarufu wakiwamo waandishi wa habari.Alisema watu hao wanaweza kufuta sifa za uongozi wa Rais Kikwete kutokana na tabia iliyoanza kujengeka nchini hususan ya utekaji, kung’oa kucha na kutoa macho kama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absolom Kibanda.“Matukio yanayoendelea nchini yanaweza kumwondolea sifa rais. Sasa tunashuhudia waandishi wanaanza kuuawa na wengine kuzuriwa ni vema akakemea vitendo hivyo visiendelee kuwepo ndani ya jamii yetu,” alisema.Zitto alimtaka rais kuhakikisha vurugu za kidini ambazo zimeanza kuchipukia nchini zinakomeshwa kwa nguvu zote ili Watanzania waendelee kuishi kwa kupendana kama ilivyokuwa miaka iliyopita.“Kuhusu suala la udini na vitendo vya rushwa, namuomba Rais Kikwete awe mkali kwa kuvidhibiti. Iwapo vitadhibitiwa mapema ni wazi atamaliza uongozi wake na heshima kubwa,” alisisitiza Zitto.
 
utendaji wake, uvumilivu wake, kuongea na watu wote, kujali walio chini hasa maskini ndio sifa zake kuu...

Mkuu mimi siyo mwana siasa na wala sintokuwa milele couse tangu mungu aliponijalia umri wa ujana wangu nilijipanga vizuri na napata mkate wangu bila bugdha ya mtu yeyote siku zote.. lakini.kuanzia leo nimemkubali huyu jamaa kiroho safi.hakuna zaidi yake Tanzania. big up my bro Jakaya
 
alikubali baada ya kugundua chadema walilikalia kooni swala la katiba.CCM must go wezi wakubwa wa kura nguvu ya umma imewabana
 
Roho yangu ni ngumu kuliko ninavyoweza kuielezea. haswa kwa masuala yanayohusu nchi yangu Tanzania. couse nilijua siku njingi kuwa tanzania ndiye mama yangu mpendwa, na sikupenda abadan kuikosea ama mtu aikosee nikiwa hai.Yametokea mengi sana ktk nchi hii mabaya na kila mtu mwenye akili timamu ameyajua. but, nijuavyo mimi kila kitu kibaya cha muda mrefu, lazima kinakuwaga na misingi mibaya iliyojengwa kwa muda mrefu.na kuking'oa inahitaji muda mrefu sana, na tena kinahitaji umakini mkubwa na roho ngumu sana.

Nafurahi sana na furaha isiyo na kifani leo hii kwa kutambua kwamba Rais wetu tena kuanzia leo nitakuwa namuita mpendwa wetu JAKAYA MRISHO KIKWETE Kuamua kwa moyo wake wa upendo kwa watanzania, kuamua kuwapa Watanzania nchi yao ili waweze kujitawala na kujiamulia mambo yao wenyewe.ki demokrasia. Mungu ambariki na ampe afya na maisha marefu.

Kitendo cha yeye kama raisi, kuruhusu kutungwa kwa KATIBA MPYA jambo hili siyo kitendo kirahisi kama watu wanavyofikiri kwa sababu, ni kwamba tangu tulipopata uhuru mwaka 1961, ni kama bado tulikuwa tunawaliwa bila ya sisi kujua, kwa kuwa kujitawala kwetu ilikuwa ni kwa mujibu wa sheria walizotuwekea wazungu.

Angeweza kwa mamlaka makubwa aliyo nayo kulikataa jambo hili, na hakuna ambaye angejaribu kama siyo kuthubutu kumwuliza kwa nini. lakni kwa upendo na uzalendo mkubwa alionao kwa nchi yake, ameamua rasmi kuutupilia mbali ukoloni.

Binafsi nimekushukuru mno. na najaribu kufikiri pengine hii ndiyo ile ahadi uliyowahi kutuahidi ya kwamba utakuja kufanya jambo ambalo hatutakaa tukusahau. kwa hiyo kama una jambo lingine ni sawa, lakini kwa hili mimi sintokaa nikusahau. MUNGU AKULINDE TENA NA TENA DAIMA

Are you serious?
Mkakati wa katiba mpya uliasisiwa mara baada ya kuruhusiwa kwa vyama vingi vya siasa nchini. Katiba tuliyonayo ilikuwa ina fit kwenye serikali ya chama kimoja. Hii katiba mpya imechelewa kwa kuwa watanzania tuko slow lakini mpango haukuanza jana ama juzi. Kama haujui waulize wakina marando, mrema, cheyo, lipumba,mapalala,makaidi na wengineo waliopo kwenye siasa za TZ kwa muda mrefu. Ni muda tu ulikuwa haujafika hakuna raisi yeyote ambaye angekuwa na uwezo wa kuzuia katiba mpya isiandaliwe, kufikiria hivyo ni kujidanganya. Walichoweza kufanya ni ku delay kwa ku take advantage kipindi kile ambacho upinzani ulikuwa sifuri, kwa sasa hivi upinzani ni moto ndio maana wameshindwa kuendelea ku delay zaidi. Tuwape sifa zao wapinzani hata kama hatuwapendi ukumbuke ndio wao ambao wame push mjadala wa katiba mpya bungeni hadi kuweza kufika hapa tulipo leo hii.
 
Back
Top Bottom