Hongera sana Wana-CHADEMA kwa Busara na Hekima kipindi hiki

Hongera sana Wana-CHADEMA kwa Busara na Hekima kipindi hiki

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
59,045
Reaction score
94,974
Poleni kwetu sote juu ya kuondokewa na Mzee wetu John Magufuli, kifo ni kifo na kamwe hakizoeleki.

Napenda kuwashukuru sana Wafuasi na Wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo kwa maneno ya busara hasa katika kipindi hiki cha msiba, naomba nieleweke kuwa wenzetu wa CCM wasingeweza kuwa na ustahimilivu hata punje jambo kama hili lingetokea upande wa CHADEMA.

KWA MFANO
Mali za Mbowe zilipoharibiwa hakuna mwana CCM aliyehuzunika wala kukemea jambo lile, Lissu aliposhambuliwa kwa risasi mchana kweupe, aliitwa msaliti, nakumbuka Mwenyekiti wa CCM Iringa (sina uhakika) aliwahi kurekodiwa akihamasisha "kumalizwa kwa wasaliti", Lowasa alitukanwa kila aina ya tusi, Lissu aliitwa, ameitwa na anaendelea kuitwa SHOGA na wana CCM na hakuna anayekemea, Mawazo inasadikika aliuwawa mchana kweupe na watu waliosadikika kuwa wafuasi wa CCM, hakuna mwana CCM hata mmoja alipaza sauti.

Ni mengi ya kuelezea, pengine kwa mtazamo wangu, CHADEMA wangeweza kuitumia hii fursa kulipiza kisasi ila kwa hakika wametoa pole na wote tumekuwa kitu kimoja. Niwashukuru sana na msiba huu wa Mzee Magufuli utumike kuwa CHACHU ya kutuunganisha na kuijienga Tanzania. Tujiponye na kuanza upya, hatujachelewa.

Nitamkumbuka Magufuli kwa kukataa hotel ya SUGU Mbeya isibomolewe kwa visa tu vya kisiasa.

Pumzika kwa amani John
 
Wanachadema wanatahili TUZO ya uvumilivu kwa kweli! Ni mambo mengi yasiyo haki wametendewa ila wakabakia kimya - kwa mfano kitendo walichofanyiwa hasa kwenye uchaguzi wa Serikall za mitaa na huu Uchaguzi Mkuu ni vitendo viovu mno - ila wakasamehe na wengine maskini wakaamua kujiondokea nchini kwa muda ili kuepusha shari.

Kwa huu msiba wameshasaheme na wameungana na watanzania wengine kuomboleza, kwa kweli ni uungwana ulioje.

Hongera sana CHADEMA!
 
Wanachadema wanatahili TUZO ya uvumilivu kwa kweli !! Ni mambo mengi yasiyo haki wametendewa ila wakabakia kimya - kwa mfano kitendo walichofanyiwa hasa kwenye uchaguzi wa Serikall za mitaa na huu Uchaguzi Mkuu ni vitendo viovu mno - ila wakasamehe na wengine maskini wakaamua kujiondokea nchini kwa muda ili kuepusha shari.

Hongera sana CHADEMA !! wameshasaheme na wameungana na watanzania wengine kuomboleza msiba wa Mzee wetu.
Ni kweli ndugu yangu, Yule mweneykiti wa CHADEMA Njombe yuko ndani kwa kesi ya mauwaji, yaani ukifika ukiuliza wenyeji, hakuna anayekubaliana kabisa na yale maelezo.
 
Muheshimiwa mleta uzi, mzee Magufuli alikuwa ananikera lakini leo nimelengwa na machozi. Yule mzee nitamkumbuka.😢😢😢😢
 
Back
Top Bottom