#COVID19 Hongera Serikali kwa Mwongozo wa Kupambana na Covid 19

#COVID19 Hongera Serikali kwa Mwongozo wa Kupambana na Covid 19

Hamatan

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2020
Posts
3,197
Reaction score
7,677
Leo Serikali imetoa waraka mrefu unaoelezea namna Watanzania wanavyotakiwa kupambana na tatizo la Covid 19. Kiufupi mwongozo huo wa Wizara ya Afya, unaoelezea zaidi mambo yanayotakiwa kufanywa ili kupunguza maambukizi, wajibu wa mamlaka mbalimbali za usimamizi, na wajibu wa kila raia.

Mapungufu makubwa katika waraka huo ni kutoelezea kwa kina ukubwa wa tatizo, na namna tutakavyofanya monitoring ili kujua Kama tunafanikiwa au hatufanikiwi. Lakini pia kuna maneno mengi ya kuzungukazunguka, ambayo hayakuwa na umuhimu wowote. Muungwana angekuwa straight kwenye tatizo kubwa la sasa, ambalo ni Covid 19. Hadithi nyingine hazina maana.

Mafanikio ya kitu chochote, hupimwa kwa tafiti na data. Ni vema sasa, Serikali iruhusu kufanya upimaji, angalao kwa kuanzia na wale wagonjwa wote waliopo hospitalini. Hii itawasaidia matabibu wetu kuwa na uhakika na aina ya magonjwa wanayoyatibu. Daktari unapomweleza tatizo lako la afya kwa namna unavyojisikia, huorodhesha vipimo vinavyotakiwa kufanywa, lakini kwa sasa kutokana na misimamo mbaya uliokuwepo wa Serikali, daktari anaandika vipimo vyote lakini anaogopa kuandika Covid 19 test. Hii kasoro iondolewe Mara moja.

Mimi ni kati ya watu waliokuwa wamemdharau kabisa huyu Waziri wa Afya, na kujiuliza maswali mengi aliwezaje kuupata huo udaktari kutokana na matamko yake ya awali.

Waraka wake wa sasa, ukilisoma, ukiambiwa umetolewa na Waziri daktari wa afya, huwi na shaka, japo bado umekosa ujasiri wa kitaaluma.

Kuna watu, ambao ni viongozi wamefanya makosa mengi katika kukabiliana na ugonjwa huu wa corona. Lakini maadamu sasa wanakiri kukosea kwa kubadilisha kauli zao, wote tuungane na kumkabili adui yetu wa pamoja.

Hongera sana wote mliopiga kelele dhidi ya mapungufu ya Serikali katika kukabiliana na Covid 19. Shukrani nyingi kwa WanaJF wale wenye akili timamu na dhamira njema (ukiondoa ukiondoa wachache wanaoamini wanatakiwa kuitetea Serikali kwa kila kitu - ambao humu JF wanajulikana kwa jina Mataga), hongereni Maaskotu, hongera sana Baba Askofu Mkuu Jimbo Kuu Katoliki Dar, hongera shekhe Ponda, Hongera Askofu wa Lulenge, Hongera kwangu pia maana nami ni kati ya waliopandisha mada nyingi dhidi ya corona. Ni hizi sauti, naamini zimechangia katika kuifanya Serikali kujitafakari katika Yale ambayo ilikuwa ikiyafanya.

Narudia tena, mataga mjitafakari sana, kuona kama kweli ninyi ni watu wenye akili timamu. TWAWEZA kwenye utafiti wao, walibaini kuwa CCM inapendwa zaidi na watu wajinga, na kwenye mijadala mingi hapa jukwaani, imedhihirika hivyo. Wametudhihaki sana tuliokuwa tukiitaka Serikali kuchukua hatua, kutoa mwongozo, na kuelekeza usimamizi wake. Lakini mlitudhihaki, mlitutukana na kutukejeli sana. Sasa Serikali imeyachukua mawazo yetu, na inaenda kuyasimamia. Ninyi mtaendelea na misimamo yenu hasi ya kuona kuvaa barakoa, kuwapima watu, kupunguza misongamano, ni ujinga?

Mataga acheni ushabiki kwenye mambo ya msingi. Mnapofanya ujinga kushabikia ujinga hammsaidii Rais, hamuisaidii Serikali, hamuisaidii CCM wala Taifa hili kwa ujumla. Mambo ya kijinga mnayoshabikia, ndiyo yanayowafanya watu wenye akili kubwa na wasiopenda ushabiki, kujitenga na CCM.

Tujipe pole tuliondokewa na wapendwa wetu kutokana na Covid 19, huenda kungekuwa na tahadhari mapema dhidi ya ugonjwa huu, tungeokoa maisha ya baadhi ya marehemu. Makosa yaliyofanyika, hata tukafika hapa ambapo ni misiba kila sehemu, yatujenge katika kuhakikisha makosa ya namna hii hayatokee tena siku za mbeleni.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu wajalie ufahamu Watanzania ili wakati wote wapiganie kuwapata viongozi wa kuwaokoa badala ya kuwaangamiza.

Waraka wa Serikali huu hapa:

 
Tatizo letu kama nchi ni kutoelewa mtu mwenye matatizo ya akili yupoje? Siyo kila kichaa uokota makopo. Some of the features of a mad person are as follows:

1. Confused thinking
2.Denial of obvious problems
3. Delusions or hallucinations (seeing or hearing or believing things that are not really there)

Wetu kiongozi anazo sifa hizo zote.

Ili tuwe salama
a) Huyu mtu akamatwe, afungwe kamba na alazimishwe kutumia dawa zake za magonjwa ya akili.
b) Msaidizi wake achukue usukani wa kuongoza nchi
 
Hiyo wizara ni takataka tu.

Vipi kuhusu maisha ya watu waliofariki just because Rais Magufuli na kundi lake akiwemo huyu waziri kutokuthamini maisha ya watu waliowapa dhamana ya kuwaongoza kwa kuwaona wapuuzi na wao ndio wanajua kila kitu?

I personally siwezi kumsamehe Magufuli na kundi lake katika hili.
 
Kuna watu huwa mkilala, mkiamka mnawaza Corona tu sijui huwa hamna Mambo mengine ya kufanya zaidi ya kuwaza Corona!? Huyu jamaa kwa siku lazima alete nyuzi zaidi ya 3 kuhusu Corona.
 
Kuna watu huwa mkilala, mkiamka mnawaza Corona tu sijui huwa hamna Mambo mengine ya kufanya zaidi ya kuwaza Corona!?, Huyu jamaa kwa siku lazima alete nyuzi zaidi ya 3 kuhusu Corona.
Huwezi kujua nibkwa kiasi gani hizo nyuzi ninazozileta zimechangia kubadili msimamo wa Serikali. Na hujua nibkwa kiasi gani, kwa Serikali kubadili msimamo wake, na sasa kuamua kuchukua hatua, ni maisha ya watu wangapi yataokolewa.

Tuna kazi nyingi, nina kazi nyingi kuliko unavyodhania, lakini kazi hizo ni bure kama hatuishi.
 
Yaani unaipongeza sirikali kwa kutimiza wajibu wake ikiwa imechelewa?
 
Huwezi kujua nibkwa kiasi gani hizo nyuzi ninazozileta zimechangia kubadili msimamo wa Serikali. Na hujua nibkwa kiasi gani, kwa Serikali kubadili msimamo wake, na sasa kuamua kuchukua hatua, ni maisha ya watu wangapi yataokolewa.

Tuna kazi nyingi, nina kazi nyingi kuliko unavyodhania, lakini kazi hizo ni bure kama hatuishi.
Mkuu nakuhakikishia hakuna ulichochangia kubadili msimamo wowote kwenye serikali. Siku hizi Jamii Forums imejaa watu wajinga wajinga kama wewe kitendo cha kushinda unawaza uanzishe thread gani JF masaa yote tayari kinakupunguzia uwezekano wa kuanzisha thread ya maana.

Siasa za uccm na uchadema zimezalisha chuki za kijinga zinazowapunguzia uwezo wa kuanzisha mada zinazojenga. Angalia thread zako za wiki 2 zilizopita ni Corona,Corona, Corona as if wewe ndo mtaalam wa Corona duniani. Mbaya zaidi unajifanya ni kama Tanzania au Dunia ikikusikiliza ndo Corona itaisha. Nakuhakikishia unapoteza muda wako bure.

Hakuna mwenye solution ya Corona duniani mpaka dk hii, Ila sababu hauko bize na umewekeza kwenye kuanzisha thread za Corona 24/7 ongeza bidii.
 
Yaani unaipongeza sirikali kwa kutimiza wajibu wake ikiwa imechelewa?
Unatarajia Serikali itimize wajibu wake, lakini kuna wakati Serikali hazitimizi wajibu wake, kama ilivyotokea hapo kwetu. Inaporudi kwenye kuutimiza wajibu wake, tunazipongeza, japo kwa kweli wanaostahili kupongezwa zaidi ni wale waliosababisha au walioilazimisha Serikali kutimiza wajibu wake.

Watu wengi tusichotambua ni kuwa Serikali hulazimishwa na wananchi kutenda yale ambayo wananchi wanataka. Sisi hapa nchini petu ni kinyume, wananchi wanalazimishwa kufanya yale ambayo Serikali inataka. Hii ndiyo sababu kubwa ya Serikali kuwaburuza wananchi.
 
Unatarajia Serikali itimize wajibu wake, lakini kuna wakati Serikali haitimizi wajibu wake, kama ilivyotokea hapo kwetu. Inaporudi kwenye kuutimiza wajibu wake, tunaipongeza, japo kwa kweli wanaostahili kupongezwa zaidi nibwale waliosababisha au walioilazimisha Serikali kukazimika kutimiza wajibu wake.

Watu wengi tusichotambua ni kuwa Serikali hulazimishwa na wananchi kutenda yale ambayo wananchi wanataka. Sisi hapa nchini petu Ni kinyume, wananchi wanalazimishwa kufanya Yale ambayo Serikali inataka. Hii ndiyo sababu kubwa ya Serikali kuwaburuza wananchi.
Ni kupoteza muda tu.
 
Mkuu nakuhakikishia hakuna ulichochangia kubadili msimamo wowote kwenye serikali. Siku hizi Jamii Forums imejaa watu wajinga wajinga kama wewe kitendo cha kushinda unawaza uanzishe thread gani JF masaa yote tayari kinakupunguzia uwezekano wa kuanzisha thread ya maana. Siasa za uccm na uchadema zimezalisha chuki za kijinga zinazowapunguzia uwezo wa kuanzisha mada zinazojenga. Angalia thread zako za wiki 2 zilizopita ni Corona,Corona, Corona as if wewe ndo mtaalam wa Corona duniani. Mbaya zaidi unajifanya ni kama Tanzania au Dunia ikikusikiliza ndo Corona itaisha. Nakuhakikishia unapoteza muda wako bure. Hakuna mwenye solution ya Corona duniani mpaka dk hii, Ila sababu hauko bize na umewekeza kwenye kuanzisha thread za Corona 24/7 ongeza bidii.
Ungewaacha wenye uelewa waendelee kuchangia.

Watu wenye akili, siku zote, kwa wakati sahihi, hujadili kwaajili ya kuketa usahihi. Miaka 2 iliyopita usingesikia habari ya corona, kwa sababu haikuwepo, na hakukuwa tatizo.

Tangu mwakajana, Duniani kote, corona ndiyo inayozungumziwa kika siku na kila Taifa, kwa sababu ndiyo janga hatarishi kuliko jingineblolote kwa wakati huu.

Inaonekana una uelewa mdogo sana katika mambo mengi. Ingekuwa na uelewa japo kidogo wa management and leadership, usingeleta huu mchango wako hasi. Tunasema kuwa, ukiwa Manager, kila siku ukiingia ofisini unamwuliza secretary wako Kama ameandaa kahawa, utegemee baada ya wiki 1, kila ukiingia ofisini, utakuta kahawa ipo mezani. Hii ina maana Kama unataka Jambo fulani litendeke, kila mara na kila mahali, hakikisha Jambo Hilo linatamkwa.

Hivi unadhani kuna mtu ambaye mpaka leo hajui habari ya HIV? Kwa nini mabango yanaendelea kuwekwa maeneo mengi? Hao siyo wajinga. Pole kuna kitu unakosa, lakini Ulimwengu ni shule, lakini kwa wanaohiari.
 
Ungewaacha wenye uelewa waendelee kuchangia.

Watu wenye akili, siku zote, kwa wakati sahihi, hujadili kwaajili ya kuketa usahihi. Miaka 2 iliyopita usingesikia habari ya corona, kwa sababu haikuwepo, na hakukuwa tatizo.

Tangu mwakajana, Duniani kote, corona ndiyo inayozungumziwa kika siku na kila Taifa, kwa sababu ndiyo janga hatarishi kuliko jingineblolote kwa wakati huu.

Inaonekana una uelewa mdogo sana katika mambo mengi. Ingekuwa na uelewa japo kidogo wa management and leadership, usingeleta huu mchango wako hasi. Tunasema kuwa, ukiwa Manager, kila siku ukiingia ofisini unamwuliza secretary wako Kama ameandaa kahawa, utegemee baada ya wiki 1, kila ukiingia ofisini, utakuta kahawa ipo mezani. Hii ina maana Kama unataka Jambo fulani litendeke, kila mara na kila mahali, hakikisha Jambo Hilo linatamkwa.

Hivi unadhani kuna mtu ambaye mpaka leo hajui habari ya HIV? Kwa nini mabango yanaendelea kuwekwa maeneo mengi? Hao siyo wajinga. Pole kuna kitu unakosa, lakini Ulimwengu ni shule, lakini kwa wanaohiari.
Kila la heri kwenye kampeni zako za CORONA.
 
Kila la heri kwenye kampeni zako za CORONA.
Mimi najua corona ni janga kubwa, limenigusa na limegusa wengi. Nitaunga mkono jitihada zozote zinazolenga kupunguza au kuondoa tatizo hili. Simanzi niliyoipata mimi na wengine wote waliopoteza wapendwa wao, si kitu ambacho ningependa watu wengine nao wapitie.

Kama kelele zangu, zitasaidia kuokoa hata mtu mmoja, ninamshukuru Mungu kwa sababu nimeshiriki katika kuokoa maisha ya binadamu mwenzangu. Mimi siishii tu na maandishi hapa jukwaani, lakini naongee na ndugu, wafanyakazi wangu, wanajumuia wenzangu wa jumuia ndogo ndogo, na watu nilio na uwezo wa kuwafikia. Siishii tu kuongea nao, lakini inapobidi, natoa baadhi ya vifaa Kama masks, sanitizer, na kuwanunukia dawa baadhi ya wagonjwa ambazo kwa uzoefu wa wengine, inaonekana zinasaidia.

Na katika kufanya haya, Sina hisia za siasa uchwara.
 
Mimi najua corona ni janga kubwa, limenigusa na limegusa wengi. Nitaunga mkono jitihada zozote zinazolenga kupunguza au kuondoa tatizo hili. Simanzi niliyoipata mimi na wengine wote waliopoteza wapendwa wao, si kitu ambacho ningependa watu wengine nao wapitie.

Kama kelele zangu, zitasaidia kuokoa hata mtu mmoja, ninamshukuru Mungu kwa sababu nimeshiriki katika kuokoa maisha ya binadamu mwenzangu. Mimi siishii tu na maandishi hapa jukwaani, lakini naongee na ndugu, wafanyakazi wangu, wanajumuia wenzangu wa jumuia ndogo ndogo, na watu nilio na uwezo wa kuwafikia. Siishii tu kuongea nao, lakini inapobidi, natoa baadhi ya vifaa Kama masks, sanitizer, na kuwanunukia dawa baadhi ya wagonjwa ambazo kwa uzoefu wa wengine, inaonekana zinasaidia.

Na katika kufanya haya, Sina hisia za siasa uchwara.
Wewe ni mjinga mmoja hivi, hapa unajaribu kuongea as if ni mtu mwenye hekima. Na unadai hauhusishi Siasa. Jana ulianzisha thread moja ukidai Dunia nzima inaiongelea Tanzania,ukioridhesha nukuu toka vyombo vitatu vya nje.. hiyo ndo Dunia nzima!?.. unajua kinachoendelea duniani au umejikita kwenye propaganda za Corona. Nakuhakikishia wewe ni puppet tu huna lolote unalojua kuhusu Covid 19 inaonekana umejaa habari za Tanzania tu na unazojazwa na matapeli wa kidunia kwa mgongo wa WHO,UN etc, hujui ajenda yoyote nyuma ya Covid Ila upo hapa kuleta ujinga uliokaririshwa ukaamini. Fungua macho uone upande mwingine wa shilingi. Masks, sanitizer na hizo vaccines ni zubaisha bwege tu. Ukiamua waweza kuelewa bado hujachelewa.
 
Wewe ni mjinga mmoja hivi, hapa unajaribu kuongea as if ni mtu mwenye hekima. Na unadai hauhusishi Siasa. Jana ulianzisha thread moja ukidai Dunia nzima inaiongelea Tanzania,ukioridhesha nukuu toka vyombo vitatu vya nje.. hiyo ndo Dunia nzima!?.. unajua kinachoendelea duniani au umejikita kwenye propaganda za Corona. Nakuhakikishia wewe ni puppet tu huna lolote unalojua kuhusu Covid 19 inaonekana umejaa habari za Tanzania tu na unazojazwa na matapeli wa kidunia kwa mgongo wa WHO,UN etc, hujui ajenda yoyote nyuma ya Covid Ila upo hapa kuleta ujinga uliokaririshwa ukaamini. Fungua macho uone upande mwingine wa shilingi. Masks, sanitizer na hizo vaccines ni zubaisha bwege tu. Ukiamua waweza kuelewa bado hujachelewa.
Kama huwezi hata kuhesabu tu vyombo nilivyoorodhesha, nitajadiliana nini na wewe.

Telegraph
VoA
ALJEZIRA
BBC

Na kwa sababu hukuridhika na hivyo vyombo vya habari vikubwa vya habari Duniani, nilikuongezea vingine 3 toka Africa.

Kama hivi ndiyo unaita vyombo vitatu, hivi kweli wewe ni mtu ambaye nastahili kupoteza muda wangu kujadiliana?

Vichaa, mara nyingi huamini wana akili kuliko walio wazima. Ninachoweza kukusaidia, ni kukushauri, Kama una ndugu wa karibu, waulize wanakuonaje.

Siku zote napenda kujifunza, lakini najifunza kutoka kwa watu wenye akili na maarifa lakini nami natoa mchango wangu kwa Dunia kwa kupitia taaluma yangu na maarifa niliyo nayo. Nashukuru kwamba katika Dunia hii, sehemu pekee ambayo sijatoa mchango wangu wa moja kwa moja, Ni bara la Asia tu.
 
Kama huwezi hata kuhesabu tu vyombo nilivyoorodhesha, nitajadiliana nini na wewe.

Telegraph
VoA
ALJEZIRA
BBC

Na kwa sababu hukuridhika na hivyo vyombo vya habari vikubwa vya habari Duniani, nilikuongezea vingine 3 toka Africa.

Kama hivi ndiyo unaita vyombo vitatu, hivi kweli wewe ni mtu ambaye nastahili kupoteza muda wangu kujadiliana?

Vichaa, mara nyingi huamini wana akili kuliko walio wazima. Ninachoweza kukusaidia, ni kukushauri, Kama una ndugu wa karibu, waulize wanakuonaje.

Siku zote napenda kujifunza, lakini najifunza kutoka kwa watu wenye akili na maarifa lakini nami natoa mchango wangu kwa Dunia kwa kupitia taaluma yangu na maarifa niliyo nayo. Nashukuru kwamba katika Dunia hii, sehemu pekee ambayo sijatoa mchango wangu wa moja kwa moja, Ni bara la Asia tu.
Hapa ndo mwisho mwisho wa thread yako/zako kuhusu Corona. Watu wanaongelea Ilala kuwa jiji wewe endelea na story zako za Corona. Ila mwisho wa siku utajiona mjinga sana. Na hiyo siku haiko mbali.
 
Back
Top Bottom