Hongera TRA, hongera Rais Magufuli

Hongera TRA, hongera Rais Magufuli

Mtukudzi

Senior Member
Joined
Nov 14, 2013
Posts
103
Reaction score
408
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni!

Naipongeza mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) kwa mabadiliko makubwa mliyofanya kiasi cha kuifanya mamlaka kuwa rafiki badala ya kuwa adui kwa walipa kodi. Binafsi nimeona mabadiliko haya chanya kuanzia January 2021. Wafanyakazi wa Mamlaka hii wamekuwa wasikivu na wamekuwa watu waelewa sana kulinganisha na miaka ya nyuma tangu kuanza kwa utawala huu wa awamu ya tano.

Kisiasa, hii inamuweka juu Mh. Magufuli kwa sababu karata aliyoicheza ya kumpa Bw. Mwambe nafasi ya uwaziri wa viwanda kwa namna moja au nyingine imeleta tija kwa njia isiyoweza kuwa wazi.

Kabla ya uwaziri, Bw. Mwambe alikemea tabia mbaya ya TRA akiwa TIC. Naona baada ya kuingia kwenye Baraza la Mawaziri ametema nyongo na sasa matunda yanaanza kuonekana.

Rai yangu ni kuwa TRA endeleeni na spirit hii. Hata watu waliokimbiza mitaji yao nje watairejesha muda si mrefu.

Hongera TRA, hongera Waziri Mwambe, hongera Rais Magufuli.
 
Isije ikawa tu Mheshimiwa Mwambe umekuja kujifagili kiaina humu. Yaani katika bandiko lako hili hakuna hata sehemu uliyo mtaja Kamishna Mkuu wa hiyo TRA, au Waziri wa Fedha na Mipango!

Isipokuwa tu Mwambe kuanzia mwanzo mpaka mwisho!! Na ambaye kimsingi anahusika na Viwanda na Biashara!

Sawa. Hongera kama ni kweli.
 
Watuambie Rais yuko wapi, ili hii taharuki iliotanda nchini toka tarehe 27/02/2021 iondoke.

Mbona taharuki ilivyozuka ya Waziri Wa Fedha Dk. Mpango kwamba amefariki, iliwahi kukanushwa kwa kumburuza live kwenye vyombo vya habari. Taharuki ikaisha na raia wakaachana nayo.
 
Hata watu waliowakimbiza mitaji yao nje watairejesha muda si mrefu
Watu waliokimbiza mitaji watarudi muda si mrefu sio sababu ya TRA kujirekebisha bali watarudi kwa sababu tofauti kabisa!
 
Back
Top Bottom