Dah! Ni miaka kadhaa imepita bila kukutana na NONDO za namna hii kutoka kwako mkuu hapa JF!Wanabodi,
Kama kawaida yangu, kila nikipata fursa, huja na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa"
Hili ni maslahi ya taifa ya pongezi kwa TRL, nimeona mzigo wa mabehewa mapya ya kisasa ya reli ya kisasa ya SGR ukipokelewa bandarini, DSM, hivyo hatua ya kwanza ni kutoa pongezi kwa TRL
Tulichoelezwa ni hiki
Kwa sisi baadhi yenu, tulioishi nchi za wenzetu, tumepanda treni hizi za kisasa za kasi zinazoendeshwa kwa umeme, bulet trains, ambazo zinakwenda hadi kasi ya speed 160kmh kwa saa!, ila mabehewa ya abiria ya wenzetu tuliyo yapanda, sio kama haya tunayo letewa sisi!, hivyo kwanza natoa hongera sana TRL kwa mabehewa haya.
Kwavile SGR ni reli mpya ya kisasa, je vichwa, mabehewa haya tulioletewa ni mabehewa mapya ya kisasa? Kwa jicho tuu la kawaida, behewa hilo ni lile la kwenda mwendo kasi wa 160kmh?. Naona kama sio! Kama tumenunua mabehewa mitumba, tuelezwe tuu, Watanzania ni watumiaji wazuri wa vifaa used, na hakuna ubaya wowote kutumia vitu vilivyotumika yaani used au mitumba, Ila kitu muhimu ni kwa Watanzania tuelezwe tu ukweli kuwa mabehewa haya ni used, na sio viongozi wetu watueleze tumenunua mabehewa mapya ya kisasa, kumbe ni mabehewa mitumba yaliyo karabatiwa, kupakwa rangi na kufanyiwa nakshi nakshi tu?
Hapa ninachokisoma na kinachokanushwa ni vitu viwili tofauti, kwanza Watanzania tunapaswa kuambiwa ukweli
1. Taarifa ya TRC inasema vichwa vipya na mabehewa mapya, lakini ukweli ni kuwa ni vichwa mitumba na mabehewa mitumba kama ya mwaka '1947'!.
2. Ukiyaangalia kwa ndani, haya mabehewa ni kama yana madirisha only one sided!, hiki ni kuashiria originally haya ni mabehewa ya underground trains na sio ya terestrial train!. Sisi SGR yetu ni terestrial, moja ya faida kubwa kusafiri na treni ni pamoja na kuenjoy kitu kinachoitwa scenery enjoymement, madirisha makubwa both sides abiria kuona nje, hizi behewa za madirisha ya upande mmoja, hebu mfikirie abiria wa Kigoma, seat ya upande usio na dirisha!, kuna tofauti gani na chumba cha jela?.
3. Mkataba ni wa ukarabati na kutiwa nakshi nakshi kwa vichwa na mabehewa mitumba!, na sio kuundwa kwa vichwa na mabehewa mapya!, kwanini Watanzania hatuelezwi ukweli?.
Hakuna ubaya nchi kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, kitu muhimu ni Watanzania tuelezwe ukweli!.
4. Je, hivyo vichwa viliundwa lini, wapi?, jee originally vimetumika wapi na kwa muda gani kabla sisi hatujauziwa?
5. Mitumba hiyo imenunuliwa kwa bei gani, ikakarabatiwa kwa bei gani, na kusafirishwa kwa gharama gani?
6. Tufanyiwe comparative analysis, kama tungenunua vichwa vipya na mabehewa mapya, tungetumia gharama kiasi gani, compared na kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, ili tujue tumeokoa fedha kiasi gani kwa kununua mitumba hiyo?
7. Japo gharama za kununua vitu vipya ni juu ila maintance cost ni ndogo, unaweza kununua mitumba kwa bei poa kumbe ni mitumba choka mbaya, hivyo maintenance cost ikawa juu.
8. Sii wengi wanajua kazi ya CAG sio kutoa tuu zile ripoti za hesabu za serikali, CAG ni Mdhibiti na Mkaguzi, ufhibiti unafanywa kabla ya manunuzi, je, kulifanyika tathmini yoyote rail worthness report ya vichwa na mabehewa hayo mitumba kabla hayajanunuliwa?. Then CAG atufanyie value for money audit, msikute mitumba hiyo tumepewa bure, huku watu wakipiga kubwa tunauziwa kwa bei ya mapya!.
9
. Ukiingia mkataba wa manunuzi, kwa matengenezo, mzigo ukanunuliwa, delivery ndio ikachelewa, huwezi kuvunja mkataba huo ukabaki salama, hivyo kesi ikifunguliwa, Tanzania tunashindwa hata kabla kesi haijaanza!.
10. Tulivunja mkataba wa Dowans, tulishitakiwa, tukashindwa, tukadaiwa tukasema hatulipi!, watu wakajiapisha "over my dead body", hatulipi!.
ukweli ni kuwa tumelipa kwa siri, Watanzania hatukuambiwa!.
11. Tulipo vunja mkataba wa Dowans, Zitto akashauri tuitaifishe mitambo ile, Wabunge wetu wakagoma kuwa Tanzania hatununui mitambo chakavu, mitambo mitumba!
12 Mitambo ile ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule wa Dowans, watu wale wale walio ikataa dowams, ndio hao hao danced to the tune na Hilary Clinton kuzindua Simbion kwa mkataba ule ule tuliovunja!, kwa gharama zile zile!, na capacity charge ile ile!, na tukawalipa!.
13. JPM alipoingia tukavunja mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, JPM akagoma kulipa!, ila baada tuu ya JPM kuitwa kule alipoitwa huku nyuma, sisi sio tuu tumelipa!, bali pia tumeinunua ile mitambo ya Simbion kwa bei ya ajabu!, sasa mitambo ile tuliosema ni chakavu, mtumba, na serikali yetu hatununui, mivitu chakavu, sasa ndio tumeinunua!, sasa mitambo ile ya Simbion ni mitambo yetu, ni mali yetu! na malipo yote yaliisha fanyika chap chap fasta fasta!, bila bajeti yake kuombwa popote!, bila Bunge letu kuijadili, bila CAG kuidhinisha malipo hayo!, na haya yote yamefanyika bila iWatanzania kuambiwa!.
14. NB. Unapohoji vitu kama hivi, huchelewi kunyooshewa vidole vya kukosa uzalendo au kutokuwa na nia njema!, no!, wala sijasema kilichofanyika ni wrong!, no!, ninachosema hapa ni sisi
Watanzania wa sasa ni waelewa, tuwe tuu tunaambiwa ukweli,
15. Kwa vile mambo kama haya kwenye manunuzi makubwa yaliwahi kutokea kule nyuma kwenye ununuzi wa Rada mtumba toka BAE, watu wakaweka cha juu kikubwa tuu, tukalipa fasta!, Mama Mzalendo wa kizungu, Linda Chalkel akabaini, akatupigania tukarudishiwa chenji ya Rada!.
16. Ununuzi wa ndege ya rais Gulf Steeam bei ikapaishwa zaidibya mara tatu!, John Cheyo akaonyesha bei ya kiwandaji watu wakatia pamba masikioni tukalipa fasta!.
17. Kuna vifaa vya kijeshi chakavu tumeuziwa hapa!, tangu vimenunuliwa havijawahi kutumika mpaka leo!. Hivi naomba nisivizungumzie wala msiniulizie!, maana hata sisi waandishi wa habari haturuhusiwi kuzungumzia mambo ya jeshi na usalama wa taifa, ila fedha zilizotumika sio fedha za jeshi au za usalama wa taifa, ni fedha za Watanzania, kuzungumzia vifaa vya jeshi, tuliuziwa nini mitumba ni vifaa vya nini na viko wapi, hii ni no!, hatuzungumzi, lakini tulilipia fedha kiasi gani, ni haki ya Watanzania kujua!.
18. Tukanunua Boti mtumba ya MV Bagamoyo, ikafanya safari moja tuu mahali pa 30 min, ilitumia masaa 3!, Hii pia sasa ni kufaa cha kijeshi!, isizungumzwe!, ila fedha zake ni fedha za Watanzania!.
19. Hivyo kweli hivi vichwa na mabehewa haya, ni bora tukaelezana ukweli tangia mwanzo!.
20. Namalizia kwa msisitizo, hakuna ubaya kutumia vitu used!, tena vingine ni vizuri, imara, bora, madhubuti kuliko hata vipya!, na Watanzania walio wengi, kutokana na low purchasing power due to umasikini uliotopea, wengi wetu affordability yetu ni mitumba kuanzia magari, nguo hadi mitambo, hivyo tumezoea, tunachohitaji ni kuambiwa ukweli tuu!,
tutaelewa tuu kuliko...
Wasalaam.
Paskali.
Kwani Magufuli ndiye aliyekuwa mnunuzi wa hicho kivuko? Magufuli alikuwa Waziri wa ujenzi Wakati huo, wizara ina Makatibu wawili na maafisa ugavi (Wanunuzi) ambao ni wateule wa Rais, Waziri yuko bale kwa nafasi ya kisiasa kutimiza ilani ya chama, Yeye anaitwa kuzindua kwa niaba ya kumwakilisha Rais, Waziri ana mamlaka ya kumwajibisha katibu mkuu au wakurugenzi wa wizaya.Hivyo kumtwisha mzigo Magufuli wa kivuko ni ujinga mtupu.Kama hajui tu, Magufuli ndio bingwa wa kucheza hii michezo michafu ya upigaji, ununuzi wa mitumba kwa bei ya mpya na ulaghai.
Hivi unakumbuka ile boti (pantoni?) ya mwendokasi (MV Bagamoyo) aliyoinunua Magufuli ili kufanya usafirishaji wa watu kutoka Bagamoyo kuja Dar?
Hivi unajua ile boti ilikuwa ni scraper iliyookotwa kutoka jalala la kutupia meli chakavu huko Asia na kupakwa rangi kisha kuletwa Tz kama meli mpya?
Hivi unajua ile meli ilitua Tz ikiwa imejaa kutu.
Hivi unajua toka inunuliwe haikuwahi kufanya kazi popote zaidi ya kufanya majaribio.
Hivi unajua kwa aibu Magufuli aliamua kwenda kuificha kwenye stoo za jeshi mpaka leo.
CCM ni ile ile.
Samia na Magufuli kwenye upigaji ni wale wale.
SGR ni daraja la kati la Treni ziendazo kasi!
Fastest train inakwenda 360KMH.
Nadhani iko elimu zaidi ya kutambua hizi technologies..
Na zile Behewa ziko ktka madaraja mbalimbali...
Nakumbuka PM alisema zile behewa ni Daraja la 3...
Halafu singe piece cabin haliwezi kutoa taswira ya muonekano wa Train nzima pamoja na Kichwa chake....
Picha zitatutoa Roho...
Hivi kweli watanzania hatuwezi kuassembo mabehewa yetu kweli Taasisi zote hizi na watu binafsi wanajishughulisha na masuala ya kihandisi kweli hatuwezi?kuambiwa ukweli tuu!,
tutaelewa tuu kuliko...
Kama haikumhusu Kwanini alienda kujificha jeshini?Yeye si alikua mtumbua majipu hodari kwanini hakuwachukulia hatua hao walionunua?Kwani Magufuli ndiye aliyekuwa mnunuzi wa hicho kivuko? Magufuli alikuwa Waziri wa ujenzi Wakati huo, wizara ina Makatibu wawili na maafisa ugavi (Wanunuzi) ambao ni wateule wa Rais, Waziri yuko bale kwa nafasi ya kisiasa kutimiza ilani ya chama, Yeye anaitwa kuzindua kwa niaba ya kumwakilisha Rais, Waziri ana mamlaka ya kumwajibisha katibu mkuu au wakurugenzi wa wizaya.Hivyo kumtwisha mzigo Magufuli wa kivuko ni ujinga mtupu.
Magufuli asinge weza kuwatumbua sababu alikuwa ana mamlaka ya kuwawajibisha, yeye anampelekea Rais mwenye kuwateua, Rais akikataa basi,na kumbuka Waziri ukitaka mambo yako yafanikiwe ni lazima ushirikiane na Katibu na wakurugenzi wa wizara yako,ukijifanya kichwa lazima utakwama Maana wao ndio watendaji wakuu.Kama haikumhusu Kwanini alienda kujificha jeshini?Yeye si alikua mtumbua majipu hodari kwanini hakuwachukulia hatua hao walionunua?
Kiukweli tunaweza kabisa!. Tuna karakana kubwa ya reli pale Mang'ula Morogoro ianweza!. Mabehewa mitumba kama hiyo, tunayo, tulihitaji tuu matairi ya SGR, ukarabati tukafanya wenyewe!.Hivi kweli watanzania hatuwezi kuassembo mabehewa yetu kweli Taasisi zote hizi na watu binafsi wanajishughulisha na masuala ya kihandisi kweli hatuwezi?
Mimi nasema TUJITEGEMEE, kwani tunaweza kufanya kazi hizi wenyewe. Wizara ya viwanda; Wizara ya Elimu ,Sayansi, na Teknolojia, Wizara zinazohusika na miundombinu, mambo ya Nje na uwekezaji zishirikiane kutimiza Jambo hili. Tuache mambo ya kufanyiwa tufanye wenyewe!
TRCAsante kwa maelezo
Hivi Ni TRC au TRL?
Alivyokua rais aliwachukulia hatua gani hao walionunua meli mbovu?usiseme ooh sijui hawakua madarakani Tena maana ameshafukua makaburi Mara kibao.Magufuli asinge weza kuwatumbua sababu alikuwa ana mamlaka ya kuwawajibisha, yeye anampelekea Rais mwenye kuwateua, Rais akikataa basi,na kumbuka Waziri ukitaka mambo yako yafanikiwe ni lazima ushirikiane na Katibu na wakurugenzi wa wizara yako,ukijifanya kichwa lazima utakwama Maana wao ndio watendaji wakuu.
Naunga Mkono hoja.Kiukweli tunaweza kabisa!. Tuna karakana kubwa ya reli pale Mang'ula Morogoro ianweza!. Mabehewa mitumba kama hiyo, tunayo, tulihitaji tuu matairi ya SGR, ukarabati tukafanya wenyewe!.
Tanzania tuna tatizo la upangaji wa vipaumbele vyetu na kutokuwa na strategic planing!.
Wakati tunaanza ujenzi wa SGR, tulipaswa pia kuweka order ya vichwa na mabehewa, SGR ya Dar - Moro inaenda kukamilika ndio serikali inatafuta mzabuni wa kusupply vichwa 2 na mabehewa 50 in 9 months!. Hapo ni lazima utanunua ready made ya wengine yalitotumika ila sikujua kama yatakuwa this old!.
Sasa tunajenga bomba la mafuta ya Uganda, tulipaswa tujenge refinery yetu pale tanga ili Tanzania tusafishe mafuta yetu tuache kuagiza mafuta ya waarabu!. Bomba likiisha kamilika ndio utasikia tenda ya refinery!.
Tunajenga mtambo wa kuchakata gesi ya LNG pale Mandimba, gesi ikiisha chakatwa ndio mtasikia tenda ya kuisambaza domestic ikitangazwa!.
We seriously need visionary leaders wenye uwezo wa kuona mbali, sio baadhi ya hawa waliopo ambao uoni waa ni hadi mwisho wa urefu wa pua zao tuu!. Tanzania bado tuna tatizo la upangaji vipaumbele vyetu, baada ya Elimu, Afya na kilimo, ilipaswa ije nishati!. Ni aibu na hatari kupikia kuni na mkaa!
P
Nyinyi Watu wanafiki sana kwani Magufuli kawakamata wangapi na kuwaweka ndani mkaanza kusema Magufuli anavisasi na watu wa karibu na Kikwete, wengi sana wamekatwa, Sasahivi ndio wanatolewa na Samia, Wengine walilipa ela wakatoka.nasema tena Magufuli hausiki na kununua kivuko yeye alikuwa Waziri tu hiyo mgemuliza Kikwete ndiye aliyeteua matibu na wakurugenzi.Mbona Sasahivi mnamlaumu Kadogosa na sio Waziri wa miondombinu?Alivyokua rais aliwachukulia hatua gani hao walionunua meli mbovu?usiseme ooh sijui hawakua madarakani Tena maana ameshafukua makaburi Mara kibao.
Pia nimekuuliza tena kwanini alienda kuificha hio meli Jeshini na akasema kabisa kwa mbwembwe eti 'kwa wale mliokua mnaisema sema hii meli Sasa mjue hii Ni Mali ya Jeshi'.
Mimi nitakuunga mkono kwa asilimia Mia moja kwani sio wao tu wenye mafuno ya kutisha watu Na kwa pamoja safari hii wakikwita tena Dodoma tutakuwa wote na nitawaomba wanajamii forum kwa Mara hii twende wote Dodoma wakatujuze Na utakuwa mwishobwa Wa kuwa nyuma ya keyboard. Hatuwaogopi tunawaheshimu tu kwani bia tunakunywa wote pale Dodoma Na kwingineko.Kwenye mambo ya SGR, Watanzania tunapaswa kuambiwa ukweli wa kila kitu!, serikali yetu lazima iwe very transparent see through kwenye kila kitu including mikataba na financial maters kufuatia kuwahi kupigwa huko nyuma kwenye rada, kwenye ndege, kwenye meli na sasa kwenye reli
Maswali haya yajibiwe kikamilifu
Maswali haya yanahitaji majibu ya kina na sio blah blah!.
Kama mtu kuuliza maswali kama haya, kutapelekea kuhojiwa uzalendo wake, mimi naomba kutumia kinga ya kihabari na kanuni ya kwanza ya mwandishi wa habari no seek the truth, and write nothing but the truth!, kuna kitu ninadhamiria sio tuu kuandika bali kukitengenezea a video documentary ya safari ya SGR ya Tanzania, tulipotoka, tulipo na tunapokwenda, ili huko mbele, likija kujitokeza liji white elephant fulani hivi ambalo sijui kama ni mimi tuu naliona, angalau dhamira yangu isinisute, niliona kabla, nikasema kabla, nikaandaa documentary kabla, nikaonyesha kabla, ili angalau jamii ya Watanzania wajue kuna watu waliona kabla na walisema kabla!.
Na labda kuwasaidia Watanzania wenzangu wasio jua, kwenye ile kashfa ya rada, BAE walikiri kutoa mlungula wa kickbacks, lakini sheria yao inawaruhusu non disclosure ya waliowapa mlungula, ilo usipoteze wateja wapya wapenda mlungula, kibiashara mlungula wa 10% ni halali!, ila ikijulikana kuwa umetoa mlungula, unapaswa ama uwataje uliowapa mlungungula, wakamuliwe wautapike huo mlingula, ama uwahifadhi usiwataje, na badala yake utozwe faini kwa uliowapa mlungula, na kuurejesha ule mlungula, na hicho ndicho kilichofanywa na BAE, kuwahifadhi waliowapa mlungula, na badala yake ikakubali kulipa faini na ndipo tukarejeshewa ile chenji ya rada.
Hii maana yake, kuna viongozi wetu walikula mlungula BAE akawakingia kifua kuwahifadhi kwa kulipia faini na ule mlungula ukarudishwa nchini kama chenji ya rada, endapo BAE wasinge wakingia kifua kuwahifadhi na kuwalinda, amini usiamini, hayo majina ya waliopokea mlungula na kuzihifadhi fedha zao kule Credit Suisse, yangetoka, Watanzania msinge amini macho na masikio yenu!.
Kashfa hii iliobuka kwasababu tuu kulitokea lijinga limoja, mgao wake yeye ukauhifadhi visiwa fulani ambavyo viko chini ya milki ya Uingereza, ndipo Muingereza akabaini, lakini kama wote wange bank Swiss banks, kule fedha zao ni very secure, hata bank manager, hajui majina ya customers na clients ni secret codes tuu zinatembea, hivyo wala kashfa ya rada isinge ibuka!.
Hivyo watu tunaoulizia kuhusu haya mabenewa, naomba mtuelewe ni wazalendo wa kweli wa nchi hii!.
Paskali
Mnafiki Ni wewe na huyo jamaa yenu aliyekua jizi huku akijificha nyuma ya Uzalendo uchwara.Nyinyi Watu wanafiki sana kwani Magufuli kawakamata wangapi na kuwaweka ndani mkaanza kusema Magufuli anavisasi na watu wa karibu na Kikwete, wengi sana wamekatwa, Sasahivi ndio wanatolewa na Samia, Wengine walilipa ela wakatoka.nasema tena Magufuli hausiki na kununua kivuko yeye alikuwa Waziri tu hiyo mgemuliza Kikwete ndiye aliyeteua matibu na wakurugenzi.Mbona Sasahivi mnamlaumu Kadogosa na sio Waziri wa miondombinu?
Kiukweli tunaweza kabisa!. Tuna karakana kubwa ya reli pale Mang'ula Morogoro ianweza!. Mabehewa mitumba kama hiyo, tunayo, tulihitaji tuu matairi ya SGR, ukarabati tukafanya wenyewe!.
Tanzania tuna tatizo la upangaji wa vipaumbele vyetu na kutokuwa na strategic planing!.
Wakati tunaanza ujenzi wa SGR, tulipaswa pia kuweka order ya vichwa na mabehewa, SGR ya Dar - Moro inaenda kukamilika ndio serikali inatafuta mzabuni wa kusupply vichwa 2 na mabehewa 50 in 9 months!. Hapo ni lazima utanunua ready made ya wengine yalitotumika ila sikujua kama yatakuwa this old!.
Sasa tunajenga bomba la mafuta ya Uganda, tulipaswa tujenge refinery yetu pale tanga ili Tanzania tusafishe mafuta yetu tuache kuagiza mafuta ya waarabu!. Bomba likiisha kamilika ndio utasikia tenda ya refinery!.
Tunajenga mtambo wa kuchakata gesi ya LNG pale Mandimba, gesi ikiisha chakatwa ndio mtasikia tenda ya kuisambaza domestic ikitangazwa!.
We seriously need visionary leaders wenye uwezo wa kuona mbali, sio baadhi ya hawa waliopo ambao uoni waa ni hadi mwisho wa urefu wa pua zao tuu!. Tanzania bado tuna tatizo la upangaji vipaumbele vyetu, baada ya Elimu, Afya na kilimo, ilipaswa ije nishati!. Ni aibu na hatari kupikia kuni na mkaa!
P
Mkuu, huo muonekano mzuri wa sgr unaochafuliwa na muonekano wa behewa hizi ni upi? Unafahamu kwamba behewa na vichwa vinavyofanya kazi kwenye reli yetu tuliyoachiwa na mkoloni hii Mgr huko zilikotoka zilikuwa zinafanya kazi kwenye sgr?Yale mabehewa hayafanani kabisa na uzuri wa reli ya SGR, yatafanya hata muonekano mzuri wa reli ya SGR upotee..
Ikibidi serikali itafute hata muwekezaji, imkodishie hiyo reli aje na mabehewa yake ya kisasa kuendana na muonekano wa reli, afanye biashara baada ya muda fulani serikali ichukue, japo pia inawezekana bei ya huduma ikawa kubwa.
Malizia kwa kusema "CCM OYEE". Kwa kweli watanzania ni zaidi ya hayawani. Yaani yote haya anayoeleza mayala anajua yanafanyika ktk utawala gn na serikali inayoundwa na kuongozwa na kirusi ganu na bado anajidi kukipenda hicho kirusi kinachowatafuna watanzania, pamoja na yeye mwenyewe. Cjui tumuiteje mtu km huyu.Wanabodi,
Kama kawaida yangu, kila nikipata fursa, huja na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa"
Hili ni maslahi ya taifa ya pongezi kwa TRC nimeona mzigo wa mabehewa mapya ya kisasa ya reli ya kisasa ya SGR ukipokelewa bandarini, DSM, hivyo hatua ya kwanza ni kutoa pongezi kwa TRL kwa kazi hii kubwa, ngumu nzuri yenye maslahi makubwa kwa taifa.
Kwa vile kabla ya kupokelewa kwa mabehewa haya, huko nyuma TRC, walitoa taarifa kwa umma kuhusu vichwa na mabehewa ya reli ya SGR, taarifa hiyo iliandamana ni picha za vichwa na mabehewa ya treni hizo, yakionyesha ni vichwa na mabehewa mchongoko!, lakini baada ya picha za mabehewa haya kuwasili na kuonyesha ni tofauti na zile za kwenye picha za mwanzo, mabehewa haya ni box body na sio mchongoko, hali iliyopelekea ujio wa mabehewa haya mapya, kupokelewa kwa mixed feelings, TRC Serikali na baadhi ya watu wakisema ni mabehewa mapya, huku wananchi na mitandaoni wakipiga kelele ni mabehewa used, mitumba, chakavu ya muundo wa kizamani, yaliyo karabatiwa na kutiwa nakshi nakshi tuu!.
Waziri Mkuu. Mhe. Kasim Majaliwa Majaliwa, alipotembelea nchini Korea Kusini kukagua kazi ya uundaji mabehewa yetu kampuni ya Sung Shin Rolling Stock Technology Company (SSRST) na hiki ndicho Waziri Mkuu alichokisema
Hii maana yake, mabehewa haya ni mapya kabisa kutoka kiwandani.
Kwa sisi baadhi yenu, tulioishi nchi za wenzetu, tumepanda treni hizi za kisasa za kasi zinazoendeshwa kwa umeme, ziko za aina mbalimbali, kuna zile za kasi, bullet trains, ambazo zinakwenda hadi kasi ya speed 360kmh kwa saa!, na kuna hizi za kawaida kama SGR yetu, yenyewe speed yake ni hadi 160 kph kwa saa.
Vichwa na Mabehewa ya treni hizi pia yana tofautiana ki usasa, mitindo na muonekano, ila mabehewa ya abiria ya wenzetu tuliyo yapanda, sio kama haya tunayo letewa sisi!, hivyo kwanza natoa hongera sana TRC kwa mabehewa haya mapya kuwasili nchini, hii ni hatua kubwa muhimu.
Kwa vile reli yetu ya SGR ni reli mpya na ya kisasa, je vichwa, mabehewa haya tulioletewa ni mabehewa mapya ya kisasa? Kwa jicho langu tuu la kawaida, naona kama behewa hilo ni na mtindo wa yale mabehewa ya kizamani, ila pia mabehewa kuonekana kwa mtindo wa mabehewa ya kizamani, sio issue, inawezekana ni muonekano tuu, sio lazima yawe ni mabehewa ya zamani, used, inawezekana kabisa, haya ni mabehewa mapya kabisa, ila yameundwa kwa mtindo wa kizamani, hivyo mabehewa haya ni mapya, sio mitumba, sio used, sio mabehewa chakavu ni mabehewa new brand!.
Ila hata kama yangekuwa ni mabehewa yaliyotumika, kumaanisha ni used, Watanzania tuelezwe tuu ukweli, Watanzania ni watumiaji wazuri wa vifaa used, na hakuna ubaya wowote kutumia vitu vilivyotumika yaani used au mitumba, Ila kitu muhimu ni kwa ubora, uimara na umadhubuti wa vifaa hivyo, kuna vifaa used ni bora, imara na madhubuti kuliko vifaa vipya!. Kama mabehewa haya ni used, Watanzania tuelezwe tu ukweli kuwa mabehewa haya ni used, na sio TRC na viongozi wetu watueleze tumenunua mabehewa mapya ya kisasa, kumbe ni mabehewa mitumba used yaliyo karabatiwa, kupakwa rangi na kufanyiwa nakshi nakshi tu!.
1. Nimemtafuta Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano TRC, Jamila Mbarouk, kwanza amethibitisha mabehewa haya ni mapya na sio mitumba, pili mabehewa yaliwasili nchini, ni mabehewa ya mkataba mpya wa mabehewa na Kampuni za Zeller KG Engineer (Austria), Baltic Port Service GmbH na Lueckemeir Transport Logistics GmbH (Germany) na sio yale mabehewa 30 na vichwa 2 vya mkataba uliovunjwa wa EUROWAGON ambao nao waliingia sub contract na walinunua vichwa 2 na mabehewa 30 kutoka kampuni ya Reli inayomilikiwa na serikali ya Germany, DB Regio, ili kuvikarabati na kuvitia nakshi nakshi, kisha vilisajiliwa kuwa mali ya TRC. Mkataba wa EUROWAGON ulivunjwa June 22 vile vichwa na mabehewa tayari yalikuwa ni mali na TRC, Hivyo kitendo cha mzigo kuwasili nchini ni ndani ya miezi 5 tuu!, mzigo wa mabehewa umetua nchini!, hii maana yake ni ama haya ni mabehewa mapya kabisa ya dukani, yaliyokuwa yakisubiri mnunuzi, baada ya kununuliwa kiwandani kabisa South Korea's Sung Shin Rolling Stock Technology Company (SSRST) na yametiwa nakshi nakshi na kuletwa nchini!, ama haya ni yale yale mabehewa mitumba ya EUROWAGON, hivyo hoja za jee mabehewa haya ni mapya ama used, bado zina mantiki!.
2. Ukiyaangalia kwa ndani, mabehewa yaliyowasili jana, yana madirisha pande zote, hivyo huu unaweza kuwa ni uthibitisho mabehewa haya ni mapya, ila yale mabehewa aliyoyakagua Waziri Mkuu kule kiwandani Korea, yana madirisha upande mmoja tuu, hiki ni kuashiria kuwa originally haya ni mabehewa ya underground trains na sio ya terrestrial train!. Sisi SGR yetu ni terrestrial, moja ya faida na raha za kusafiri kwa mabasi na treni ni pamoja na kuenjoy kitu kinachoitwa scenery enjoyment, madirisha makubwa ya abiria kuona nje mazingira.
3. Ule mkataba uliovunjwa, ulikuwa sio mkataba wa kuunda mabehewa, ule ni mkataba wa ukarabati na kutiwa nakshi nakshi kwa vichwa na mabehewa!, na sio kuundwa kwa vichwa na mabehewa mapya!, lakini Waziri Mkuu amezungumzia ujenzi wa mabehewa na sio ukarabati na nakshi nakishi, hivyo mabehewa yaliyowasili ni mabehewa mapya!, kwa nini Watanzania hatuelezwi ukweli tangu mwanzo, hivyo kutoa fursa kwa watu kudhania tumenunua mitumba?.
4. Japo ule mkataba wa EUROWAGON uliovunjwa ulikuwa ni vichwa na mabehewa used, by the time mkataba unavunjwa, hao EUROWAGONS waliisha lipwa malipo ya awali na kuvununua hivyo vichwa na mabehewa 30, ambayo tayari ni mali ya TRC, Watanzania tuna haki ya kuelezwa, hivyo vichwa na mabehewa ya EUROWAGONS, vilinunuliwa wapi, viliundwa lini, wapi?, vimetumika wapi na kwa muda gani kabla TRC hatujauziwa?
5. Watanzania tuelezwe gharama halisi za manunuzi, ukarabati, naksh naksh na usafirishaji mpaka yamepokelewa ili tufanyiwe a comparative analysis, kama tungenunua vichwa vipya na mabehewa mapya, tungetumia gharama kiasi gani, compared na kununua vichwa na mabehewa used ili tujue tumeokoa fedha kiasi gani kwa kununua used?
6. Japo gharama za kununua vitu vipya ni juu ila gharama za maintenance ni ndogo, unaweza kununua kitu used kwa bei poa kumbe ni kitu chakavu sana choka mbaya, hivyo gharama ya maintenance ikawa juu kuliko hata ungenunua kipya!.
7. Sii wengi wanajua kazi ya CAG wakidhani ni kutoa tuu zile ripoti za ukaguzi wa hesabu za serikali, CAG ni Mdhibiti na Mkaguzi, udhibiti unafanywa kabla ya manunuzi, je, kulifanyika tathmini yoyote rail worthiness report ya hivyo vichwa na mabehewa hayo used kabla hayajanunuliwa? Kama haikufanyika, then tusisubiri hadi mradi ukamilike ndipo CAG aikague SGR, baada ya kuanza hizi kelele kelele za mpya vs used, atufanyie a value for money audit, hiki kipande cha Dar- Moro, ili kama tumepigwa, tusiendelee kupigwa mpaka mwisho, tena usikute ni kweli tumeuziwa vichwa na mabehewa used kwa bei ya mapya!, watu wakajivunia viji 10% vyao vya maana tu!
8. Ukiingia mkataba wa manunuzi, kwa matengenezo, mzigo ukanunuliwa, delivery ndio ikachelewa, huwezi kuvunja mkataba huo ukabaki salama, hivyo kesi ikifunguliwa, Tanzania tunashindwa hata kabla kesi haijaanza!
9. Tulivunja mkataba wa Dowans, wanasheria wetu wakatuhakikishia hatutashitakiwa!, tukashitakiwa!, wanasheria wetu wakatuhakikishia tutashinda!, tukashindwa na tukadaiwa tozo ya Dowans, wanasheria wetu wakatuhakikishia hatutalipa na hawatatufanya lolote!, tena kuna wakajiapisha "over my dead body", hatulipi!
ukweli ni kwa tumelipa every cent kisiri siri bila Watanzania kuelezwa, bila Bunge kujulishwa na kuidhinisha, bila CAG kudhibiti na kukagua!. Kwanini hatuambiwi ukweli?
10 Tulipo vunja mkataba wa Dowans, Zitto akashauri tuitaifishe ile mitambo, waheshimiwa Wabunge wetu wakagoma kuwa Tanzania hatununui mitambo chakavu, mitambo mitumba, na kweli kwa wakati huo hatukuwa na sheria ya kununua mitambo chakavu.
11 Tulivunja mkataba ule wa Dowans kwasababu ya gharama kubwa cha capacity charges na umeme wenyewe!, Mitambo ile Dowans ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule wa Dowans!, kwa capacity charge ile ile!, watu wale wale walio ikataa dowams, ndio hao hao danced to the tune na Hilary Clinton kuzindua Simbion!, kwa mkataba ule ule tuliovunja!, kwa gharama zile zile!, na capacity charge ile ile!, na tukawalipa!.
12. JPM alipoingia tukavunja tena na mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, tukadaiwa, JPM akagoma kulipa!, ila baada tuu ya JPM kuitwa kule alipoitwa huku nyuma, sisi hao hao, sio tuu tumelipa!, bali pia tumeinunua ile mitambo ya Simbion kwa bei ya ajabu!, sasa mitambo ile tuliosema ni chakavu, mtumba, na serikali yetu hatununui, mitambo chakavu, sasa ndio tumeinunua!, sasa mitambo ile ya Simbion ni mitambo yetu, ni mali yetu! na malipo yote yaliisha fanyika chap chap fasta fasta!, bila bajeti yake kuombwa popote!, bila Bunge letu kuijadili, kuipitisha na kuidhinisha, bila CAG kuidhinisha malipo hayo!, na haya yote yamefanyika bila sisi Watanzania kuambiwa!, kwanini vitu vikubwa kama hivi hatuambiwi?.
13. Kwa vile mambo kama haya kwenye manunuzi makubwa yaliwahi kutokea kule nyuma kwenye ununuzi wa Rada mtumba toka BAE, watu wakaweka cha juu kikubwa tuu, tukalipa fasta!, Mama Mzalendo wa kizungu, Linda Chalkel akabaini, akatupigania tukarudishiwa chenji ya Rada!.
14. Ununuzi wa ndege ya rais Gulf Stream bei ikapaishwa zaidi mara mbili!, Mzee John Memosa Cheyo akaonyesha bei halisi ya kiwandani! watu wakatia pamba masikioni tukalipa fasta!. Kuna vifaa fulani chakavu vya taasisi fulani nyeti tumeuziwa hapa!, tangu vimenunuliwa havijawahi kutumika mpaka leo!. Hivi naomba nisivizungumzie wala msiniulizie!, maana hata sisi waandishi wa habari haturuhusiwi kuzungumzia mambo ya taasisi fulani fulani nyeti ila fedha zilizotumika sio fedha za taasisi nyeti, ni fedha za Watanzania, kuzungumzia vifaa vya nyeti sio sawa, hivyo hatuvizungumzii, lakini kwa vile tulilipia kwa fedha za Watanzania, hakuna mipaka yoyote ya kuzungumzia matumizi ya fedha za umma!, Watanzania wana haki ya kujua matumizi yote ya kodi zao!.
15. Tukanunua meli fulani moja mtumba iliyochoka, dholfu bin taaban, MV Bagamoyo, ikafanya safari moja tuu ya Dar - Bagamoyo, mahali pa safari ya dakika 30, ilitumia masaa 3!. Hii meli sasa imewekwa kwenye kundi la vifaa vya taasisi nyeti, hairuhusiwi kuzungumziwa hivyo isizungumzwe!, ila fedha zake ni fedha za Watanzania, Watanzania wana haki kujua!.
Hitimisho
Namalizia kwa msisitizo, hakuna ubaya kutumia vitu used!, tena vingine ni vizuri, imara, bora, madhubuti kuliko hata vipya!, na Watanzania walio wengi, kutokana na low purchasing power due to umasikini uliotopea, wengi wetu affordability yetu ni mitumba kuanzia magari, nguo hadi mitambo, hivyo tumezoea, tunachohitaji ni kuambiwa ukweli tuu!,
tutaelewa tuu kuliko...
Wasalaam.
Paskali.
NB. Makala hizi ni free kutumiwa na gazeti, jarida, mtandao wowote, hazina copyright, ila source na mwandishi wawe attributed.