Nshomile wa Muleba
JF-Expert Member
- Dec 5, 2015
- 2,166
- 5,620
Jambo Jambo?
Katika Tasnia nzima ya habari(upande wa luninga na redio) huwa nafurahishwa sana na hawa vijana wawili wakitokea stesheni ya STAR TV, Huwa wana udhubutu wa kuuliza maswali magumu kwa wanasiasa wa nchii hii hususani wenye madaraka.
Nakumbuka mwenyekiti wa CCM mwanza alipigwa maswali na Aloyce Nyanda katika kipindi chake cha THE BIG AJENDA, mpaka kumaliza glasi 3 za maji ndani ya dakika 20 tu, Halafu kwa ujanja kamera mani akawa ana”zoom” mara kwa mara glasi ya mheshimwa huyo wa CCM. Maswali yalimpelekea awe na kigugumizi cha ghafla kutokana na maswali magumu ya papo kwa hapo.
Hali kadhalika nilifurahiswa na mahojiano kati ya Edwin Odemba na Mbunge wa Biharamulo mashariki Eng. Ezra katika kipindi cha MEDANI ZA SIASA hapohapo STAR TV, na ni baada ya kupigwa swali mbunge huyo juu ya Tatizo za mtandao wilaya ya biharamulo mashariki kudumu kwa miaka zaidi ya 60 na serikali ipo na haina nia ya kulitatua tatizo hususani mbunge huyo.
1. Katika tasnia nzima ya habari (luninga na redio), hawa ndo wamebaki pekee kuwatwanga maswali yaliyonyooka na hupelekea wahojiwa hasa wa CCM kukimbia interview zao
(Fardhia Middle wa ITV na kipindi chake cha DAKIKA 45 anajitahidi ila bado hajawafikia hawa)
2. Hawa ndo waandishi pekee ambao huwa wapo mbele ya kamera na sijawahi kusikia wakisifia serekali kwa unafiki na kutegemea teuzi.
Kuna tetesi kuwa baadhi ya mawaziri huwa wanakimbia interview za hawa jamaa na badala yake huenda kwenye stesheni washirika zenye mtazamo wa kichama, ili wakaulizwe maswali mepesi na kabla ya interview huwa wanadokesewa maswali watakayoulizwa ili wajipange.
Katika Tasnia nzima ya habari(upande wa luninga na redio) huwa nafurahishwa sana na hawa vijana wawili wakitokea stesheni ya STAR TV, Huwa wana udhubutu wa kuuliza maswali magumu kwa wanasiasa wa nchii hii hususani wenye madaraka.
Nakumbuka mwenyekiti wa CCM mwanza alipigwa maswali na Aloyce Nyanda katika kipindi chake cha THE BIG AJENDA, mpaka kumaliza glasi 3 za maji ndani ya dakika 20 tu, Halafu kwa ujanja kamera mani akawa ana”zoom” mara kwa mara glasi ya mheshimwa huyo wa CCM. Maswali yalimpelekea awe na kigugumizi cha ghafla kutokana na maswali magumu ya papo kwa hapo.
Hali kadhalika nilifurahiswa na mahojiano kati ya Edwin Odemba na Mbunge wa Biharamulo mashariki Eng. Ezra katika kipindi cha MEDANI ZA SIASA hapohapo STAR TV, na ni baada ya kupigwa swali mbunge huyo juu ya Tatizo za mtandao wilaya ya biharamulo mashariki kudumu kwa miaka zaidi ya 60 na serikali ipo na haina nia ya kulitatua tatizo hususani mbunge huyo.
1. Katika tasnia nzima ya habari (luninga na redio), hawa ndo wamebaki pekee kuwatwanga maswali yaliyonyooka na hupelekea wahojiwa hasa wa CCM kukimbia interview zao
(Fardhia Middle wa ITV na kipindi chake cha DAKIKA 45 anajitahidi ila bado hajawafikia hawa)
2. Hawa ndo waandishi pekee ambao huwa wapo mbele ya kamera na sijawahi kusikia wakisifia serekali kwa unafiki na kutegemea teuzi.
Kuna tetesi kuwa baadhi ya mawaziri huwa wanakimbia interview za hawa jamaa na badala yake huenda kwenye stesheni washirika zenye mtazamo wa kichama, ili wakaulizwe maswali mepesi na kabla ya interview huwa wanadokesewa maswali watakayoulizwa ili wajipange.