Hili ni jambo zuri sana mmefanya kwakweli. Na kwa jinsi timu ilivyo na mashabiki mtapata wabia chapchap. Ila sasa jiji lisitake kujilimbikiazia hisa nyingi. Itakuwa sawa na kazi bure. Nyie bakini hata na 20% ili hao wabia wawe na uhuru mkubwa wa kuamua matumizi ya fedha zao. isitokee watu kwa maslahi binafsi wakataka jiji liwe na hisa nyingi ili waendelee kupiga ubwana kwenye timu. Mashabiki hatutaki timu ilete hela jijini, tunataka ilete vikombe so hisa nyingi kwa jiji ni kuvuruga huu mpango mzuri mlioanzisha.
Msimu ujao ntaanza tena kuangalia mechi zenu sokoine.