Hongereni Yanga kubeba tuzo saba za TFF, Sio kwa bahati mbaya bali ubora wenu ndio unaowabeba

Majok majok

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2023
Posts
783
Reaction score
2,057
Tuzo za TFF zimeonyesha ni kwa namna gani timu ya wananchi ilivyokuwa bora msimu uliopita, walijipanga kwa usajili bora kuanzia kwa kocha mpaka Wachezaji.

Ukilima vizuri basi pia utavuna vizuri, uwezi kupanda bangi ukategemea kuvuna mahindi ulichokipanda ndicho utakachovuna, tumeona wengine wametoka kapa bila tuzo yoyote baada ya usajili wa wakina Pa Omar Jobe

Pongezi pia kwa kamati ya tuzo safari hii awakutaka kubalance mambo Kama zamani Kila aliyestahili kapewa tuzo yake ndivyo inavyotakiwa.

N:B Tunaomba mwakani pia ziwepo tuzo za sold out ili na sisi tuambulie chochote๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ
Soma zaidi: Leo ndiyo usiku wa tuzo za TFF kwa wanasoka waliofanya vizuri msimu wa 2023/2024



 
Na hiyo SOLD OUT yenyewe, subiria mapengo ya viti siku ya yenyewe
hata mimi nisingeenda,,sasa wanacheza nini,kombe wakose na tuzo tena oooh mashabiki kuvunjwa moyo
 
Asee tiefuefu tuleteeni tuzo ya matamasha na sie tujidai jameni
 
Simba ilivyokuwa inabeba miaka 4 mfululizo mlisema Karia hapendi Yanga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ