Hospitali Wilaya Mkuranga haina huduma ya X-ray

Hospitali Wilaya Mkuranga haina huduma ya X-ray

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
attachment.php
​
attachment.php


Wakazi wa Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, wamelalamikia Hospitali ya Wilaya hiyo kwa kutokuwa na huduma za X-ray, hivyo kuwalazimu kwenda katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), jijini Dar es Salaam kupata huduma hiyo.

Wakizungumza na NIPASHE kwa nyakati tofauti, wakazi hao walisema hospitali hiyo kukosa huduma za X-ray kunawasababishia gharama za kwenda jijini Dar es Salaam kupata huduma hiyo.

“Tunapopata matatizo ya kuumia au kuumwa na kufika hospitalini hapo, tunaambiwa hakuna huduma hiyo na kuambiwa twende Muhimbili kwa ajili ya kupata huduma hiyo,” walisema wakazi hao.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilayani humo, Rwey Jamal, alisema hiyo haikutakiwa kuitwa hospitali na ilitakiwa kuitwa kituo cha afya.

Alisema alipopata ajali ya pikipiki, alifikishwa hospitalini hapo na kupatiwa huduma ya kwanza, lakini akashauriwa kwenda Muhimbili kwa ajili ya kupata huduma ya X-ray kwa kuwa haipo katika hospitali hiyo.

Jamal alisema alishangaa kuambiwa hivyo na madaktari wa hosipitali hiyo, kwa kuwa huduma hiyo ilitakiwa kuwapo kutokana na kuwa ndiyo hospitali kubwa na kiungo katika barabara za mkoa wa Kusini na ajali za mara kwa mara huwa zinatokea.

Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk. Francis Mwanisi, alithibitisha kutokuwapo kwa huduma hiyo na kudai kuwa wapo mbioni kuiweka.

“Ni kweli hapa hospitalini inapotokea mgonjwa anatakiwa kupatiwa huduma ya X-ray, huwa tunamwambia aende Muhimbili. Lakini hivi sasa tumejipanga na muda siyo mrefu huduma hiyo itaanza kutolewa,” alisema Dk. Manisi.




CHANZO: NIPASHE

 

Attachments

  • kifuwa.jpg
    kifuwa.jpg
    3.9 KB · Views: 150
  • X RAY.jpg
    X RAY.jpg
    5.1 KB · Views: 95
Back
Top Bottom