Hospitali ya Taifa Muhimbili yatoa ufafanuzi hoja ya Mdau kuhusu "Huduma zake ni janga kwa Wagonjwa"

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Baada ya Wanachama wa JamiiForums.com kuandika hoja zinazoitaja Hospitali ya Muhimbili - Mlonganzila kuwa na gharama kubwa na changamoto nyingine za kiutendaji, taasisi hiyo imetoa ufafanuzi. Kusoka hoja za Wadau bofya hapa chini:

~ DOKEZO: Serikali iimulike hospitali ya Mloganzila, Huduma zake ni janga kwa wagonjwa na ndugu wanaouguza pale

~ Gharama za Kujifungua Hospital ta Taifa Muhimbili MNH (Mloganzila) ni kufuru




UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ILIYOCHAPISHWA NA MTANDAO WA JAMIIFORUMS KUHUSU HUDUMA ZA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI-MLOGANZILA

DAR ES SALAAM: NOVEMBA 22, 2024
Mtandao wa JamiiForums umechapisha taarifa yenye kichwa cha habari "Serikali limulike Hospitali ya Mloganzila, huduma zake ni janga kwa wagonjwa na ndugu wanaouguza." Kutokana na taarifa hiyo, Uongozi wa Hospitali unapenda kutoa ufafanuzi ufuatao;

1. Wagonjwa 20 hadi 25 kufariki kwa siku
Miaka ya hivi karibuni hadi Novemba 21, 2024, idadi ya wagonjwa wanaoonwa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeongozeka kutoka wagonjwa wa nje 400 hadi 1,000 kwa siku na idadi ya wagonjwa waliolazwa wodini wakati wote imeongezeka kutoka 200 hadi 400 kwa siku. Hii ni kutokana na uboreshaji mkubwa wa mifumo na huduma uliofanywa hospitalini hapo na hatimaye kuvutia wananchi wengi kuitumia hospitali hiyo.

Idadi ya wagonjwa wanaofariki kwa siku hospitalini hapo kutokana na sababu mbalimbali ni kati ya wanne (4) hadi sita (6) kati ya wagonjwa 400 waliolazwa na siyo 20 hadi 25 kwa siku kama ilivyoelezwa katika taarifa iliyochapishwa na JamiiForums.

2. Kutoa taarifa za mgonjwa
Ni kinyume na maadili ya kitabibu kwa mtoa huduma kutoa taarifa za mgonjwa bila ridhaa yake na kwa wale ambao hawajiwezi taarifa hutolewa kwa ndugu aliyeandikishwa au kupewa idhini ya kupokea taarifa hizo (next of kin). Ndugu wengine wanaopenda kufahamu taarifa za mgonjwa wanazipata kutoka kwa mgonjwa mwenyewe au ndugu aliyeandikishwa endapo watapenda kufanya hivyo. Tutaendelea kusimamia jambo hili.

3. Gharama za matibabu kuwa juu
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila inapokea na kuhudumia makundi manne ya wagojwa ambayo ni wagonjwa wa bima, wanaolipa fedha taslimu, wagonjwa wa rufaa wanaochangia huduma na wagonjwa wa msamaha. Mwaka wa fedha 2023/2024, Hospitali imetoa huduma kwa njia ya msamaha zenye thamani ya TZS. 3.9 Bil na kwa robo mwaka wa fedha 2024/2025 huduma zenye thamani ya TZS. 970 Mil zimetolewa kwa wananchi wasiokuwa na uwezo.

Ikumbukwe kuwa, Hospitali hii ni ngazi ya nne (ngazi ya juu) ya utoaji huduma nchini, hivyo teknolojia ya huduma za uchunguzi na matibabu imebalidika kutoka za kawaida kwenda kwenye ngazi za ubingwa bobezi ili kumpa mgonjwa matibabu stahiki. Endapo kuna mgonjwa ana changamoto ya malipo utaratibu wa hospitali uko wazi kupitia Huduma za Ustawi wa Jamii.

4. Kauli za Watoa Huduma
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeendelea kutekeleza azma ya Serikali ya utoaji huduma bora kwa wananchi. Kauli zisizo na staha kutoka kwa watoa huduma zimepungua kwa kiasi kikubwa. Uongozi wa Hospitali hauvimilii kauli za namna hii. Tumelipokea jambo hili, tutaendelea kulifanyia kazi,

Aminiel Buberwa Aligaesha
MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMΜΑ
 
Mmmh!

Gharama za kitanda kwa siku zinaelezwa kuwa ni Tsh. 50,000/- bila ya huduma nyingine yoyote ile ya ziada, Je, kuna Ukweli gani kuhusu suala hili?

Mbona sasa gharama hizi ni kubwa sana kama gharama za Malazi kwenye Hoteli ya Kitalii ya kifahari kwa hapa Tanzania? Kulikoni Jambo hili?
 
Mnahitajika huku
 
Waambie ufafanuzi wao ni batili! Kwanini hawajaainisha gharama kama mlalamikaji alivyosema?

Lugha Chafu Hilo linasemwa na wengi hata huko Facebook wamekuwa wakisema.

Maandiko kadhaa nimesoma Nje na JF yanasema ukipelekwa Mlonganzila uwezekano wa kupona ni mdogo sana.
 
Kitu ambacho huwa sikielewi kwenye hospitali za serikali ni kwamba, LABDA KAMA HAWAPOKEI FUNGU LA KUENDESHEA HOSPITALI TOLA SERIKALINI. nijibuni maswali haya;

1. Hospitali hizi za serikali, zinajiendesha? au zinaendeshwa kwa kodi/bajeti ambayo ni kodi yetu. kama jibu siyo, kwanini?

2. Serikali huwa inanunua mitambo mara kwa mara. mfano; mtambo wa MRN, xray na mingine, na vipimo vingine. mitambo hiyo huwa inanunuliwa kwa pesa zinazotokana na kodi za wananchi au na pesa zinazotozwa hospitali?

3. Kama jibu namba 2 litakuwa vinanunuliwa kwa pesa za kodi, wanapata hasara gani wakiamua kupima watu bure badala ya kuwalipisha? Mashine umepewa na serikali haujanunua wewe au umepewa msaada, unao wafanyakazi wa kila siku uliowaajiri wa kuziendesha, umeme zinatumia wa kawaida hata usipozitumia bili inakuja hat akuongezeka itakuwa kidogo sana, kama mashine hizo ni zetu sisi watanzania, KINACHOWAFANYA MSIPIME WATU BURE NI NINI? Mngepata hasara gani? Au mna shetani wa kulipisha watu msipolipisha mtu akapata huduma bure mnajisikia vibaya sana? si mali yetu sote, hamjanunua, au mmenunua kwa pesa za kodi zetu, pimeni watu bure, wengi wanakufa kwa kukosa huduma ambazo kodi zao zimenunua vifaa mnavyotumia.

4. Serikali, inashindwa nini, kwa pesa hizo samia anabukia kwenye masafari yaliyojaa wasanii wasio na faida yeyote kwa nchi, wanashindwa nini kununua vitendea kazi mahospitalini ili ibaki kwa madaktari kuvitumia kwa watu bure. mnashindwa nini? Safari mbili za Samia zinanunua MRN moja. Hata hizi za mkoani zina garama sana. Pesa wanazotumbua na kuiba wangeweza kununua mashine nyingi, na kwa sababu ni za kwetu tutumie bure, na wafanyakazi tunao tayari hawatalipwa ziada kwa kuendesha mashine za vipimo.

5. Mnajisikiaje mtu kwenda hospitali ya umma leo hii, analipia hata ultrasound? au mnataka watu wawe wanakufa tu.
 
Imagine, upo kwenye familia, mkaamua mnunue kitendea kazi, mkakipata kwa juhudi za kila mmoja. au mmepata msaada.

Hivi, mkiamua kukitumia bila kuchajiana mtakula hasara gani? MRN, citiscan, exray, ultrasound etc mkizinunua au kupewa msaada, kwanini mnalipisha hela kubwaaa? MRN ni zaidi ya milioni wakati ilinunuliwa na pesa za kodi zetu.

Mtapungukiwa nini siku moja mtu aende hospitali asikie ultrasound bure, MRN bure, kumwona daktari bure kwa sababu ni mali za umma wa watanzania, ni mali zetu, na watanzania wenyewe ndio sisi.

Mtapungukiwa nini? Au ninyi ndio wapenda kuchangishachangisha mtu akipata kitu bila kuchangia mnaumia kweli kweli.
 
Ongeza na milion 700 za stars.
 
Mkuu sekta ya afya ni Pana sana Ina matibabu,Kinga na tafiti vyote vinahitaji pesa tukitaka huduma za Bure haiwezekani ikawa Bure labda iwe huduma zitolewe kwa bei nafuu sana. Naipongeza. hospital ya kisarawe iliyopo mkoani Pwani huduma pale zinatolewa ni za kibingwa kwa wananchi wengi wa mkoa wa Pwani wengi kutoka manerumango, chole,vikumbulu,Malui ni maskini kweli kweli lakini wanada ikiwa kupata matibabu kwa gharama nafuu sana.

Tunaposema matibabu yanaendana na Kinga na tafiti nani atagharamia hizo kinga na tafiti au tukae tukiwategemea wafadhili .

Hiyo mitambo inaharabika pesa ya service itoke Tena serikalini hapana ,inabidi tukubali matibabu yatolewe kwa kulipia kiasi sio hicho kopimo unaambiwa laki SITA operation unaambiwa milioni na nusu ,kitanda elfu hamsini hapana Kwa hospitali za serikali hizo ni bei za hospital binafsi ambazo hazipati msaada wowote kutoka serikalini.
 
Kwakweli inasikitisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…