DOKEZO Hospitali ya Wilaya ya Mlele – Katavi haina Mhasibu, watumishi wa kawaida ndio wanapokea fedha za Wagonjwa

DOKEZO Hospitali ya Wilaya ya Mlele – Katavi haina Mhasibu, watumishi wa kawaida ndio wanapokea fedha za Wagonjwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

NBica

Member
Joined
Sep 13, 2010
Posts
39
Reaction score
36
Tunaomba TAKUKURU ichunguze mapato ya Hospitali ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi haina Mhasibu yoyote tangu ianzishwe na Mapato ya Hospitali yanakusanywa Jengo la Nje la Wagonjwa (OPD) na Wauguzi ambao sio taaluma yao katika ukusanyaji wa pesa ya Hospitali.

Pia imeonekana na kusadikika kuwa pesa zinatunzwa na Mtumishi fulani wa OPD na kuna wakati watumish katika Hospitali hiyo walitoa mawazo yao kuwa aondolewe haraka huyo Muuguzi anayehifadhi pesa za hospitali lakini Mganga Mfawidhi anamkingia kifua.

Ujumbe huu ufike kwa mamlaka za juu kwa kuwa lengo letu ni Hospitali iweze kunufaika na mapato kwa kuletwa Mhasibu mwenye taaluma hiyo ili kila mgongwa alipe pesa katika njia sahihi.

Kukosekana kwa Mhasibu kunaweza kuwa chanzo cha upigaji na Serikali kupoteza mapato kwa wingi, lakini pia tutambue hii hospitali bado ni mpya inahitaji kuingiza fedha ili huduma ziendelee kuboreshwa.

Majibu ya Hoja soma hapa ~ Katavi: Mganga Mkuu wa Wilaya asema wapo kwenye mchakato wa kuajiri Mhasibu wa Hospitali ya Wilaya ya Mlele
 
Acha uswahili kituoni fanya kazi achana na yasiyokuhusu
 
Uhasibu sio ''core function'' ya hospitali; ingekuwa hakuna madawa, vitendea kazi, madaktari au watoa huduma wa afya hawapo, hapo hoja yako ingekuwa na mashiko.
 
Baada ya Getu kukukatalia sasa umeamuwa uje kwa gia nyingine
 
Tunaomba TAKUKURU ichunguze mapato ya Hospitali ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi haina Mhasibu yoyote tangu ianzishwe na Mapato ya Hospitali yanakusanywa Jengo la Nje la Wagonjwa (OPD) na Wauguzi ambao sio taaluma yao katika ukusanyaji wa pesa ya Hospitali.

Pia imeonekana na kusadikika kuwa pesa zinatunzwa na Mtumishi fulani wa OPD na kuna wakati watumish katika Hospitali hiyo walitoa mawazo yao kuwa aondolewe haraka huyo Muuguzi anayehifadhi pesa za hospitali lakini Mganga Mfawidhi anamkingia kifua.

Ujumbe huu ufike kwa mamlaka za juu kwa kuwa lengo letu ni Hospitali iweze kunufaika na mapato kwa kuletwa Mhasibu mwenye taaluma hiyo ili kila mgongwa alipe pesa katika njia sahihi.

Kukosekana kwa Mhasibu kunaweza kuwa chanzo cha upigaji na Serikali kupoteza mapato kwa wingi, lakini pia tutambue hii hospitali bado ni mpya inahitaji kuingiza fedha ili huduma ziendelee kuboreshwa.

Majibu ya Hoja soma hapa ~ Katavi: Mganga Mkuu wa Wilaya asema wapo kwenye mchakato wa kuajiri Mhasibu wa Hospitali
😃😃😃jikaze we nawe kazi zote hizi bado unapata muda wa kuleta upuuzi huu kweli🤭 binadamu bhana
 
Tunaomba TAKUKURU ichunguze mapato ya Hospitali ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi haina Mhasibu yoyote tangu ianzishwe na Mapato ya Hospitali yanakusanywa Jengo la Nje la Wagonjwa (OPD) na Wauguzi ambao sio taaluma yao katika ukusanyaji wa pesa ya Hospitali.
Weka picha yao tujiridhishe
 
Back
Top Bottom