Hoteli gani inajengwa mkoani kwako?

Rene Jr.

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2014
Posts
3,714
Reaction score
2,376
Salaam wakuu,
nahitaji orodha ya hotels, lodges, na guest house zenye hadhi ambazo ziko under construction na ambazo zimefunguliwa hivi karibuni, popote Tanzania, kuondoa hapa Dar. Ukiandika na mawasiliano ya mmiliki au hata jina lake tu utakuwa umenisaidia sana, kuna kazi nahitaji kufanya na hawa wakuu. Natanguliza shukrani.
 
Lete hela mm nifanye hiyo kazi ya kutafuta hotel na guest pamoja na wamiliki wake, how coma mtu azunguke kukutafutia ww bure?
 
lete hela mm nifanye hiyo kazi ya kutafuta hotel na guest pamoja na wamiliki wake, how coma mtu azunguke kukutafutia ww bure?

naamini amekupata coz hakuna research isiyo na budget kwa ajili ya field assistants au data collectors. So tangaza kazi kisha mwingie mkataba na uwape questionnair, au maswali ya face to face interview vijana wakuletee information faster!!!!!!!





Natta wito
 
Wanaofahamu ndugu na jamaa wanaojenga hotels tufahamishane. Nature ya kazi yenyewe hailazimu niajiri mtu kunikusanyia hizo data kwa sababu sihitaji orodha ndeefu, nikipata mbili kila mkoa zinatosha sana. Nikifanikisha nachohitaji mkono wangu huwa mwepesi kusema asante kwa mtu yeyote aliyenisaidia katika njia hiyo. Kama ni lazima upewe pesa kwanza pia ni haki yako lakini hapana, asante.
 

Nadhani sio rahisi kufahamu jina la hotel ambayo bado iko under construction kama ambavyo ni vigumu kujua jina la mtoto ambaye hajazaliwa!
 
Nadhani sio rahisi kufahamu jina la hotel ambayo bado iko under construction kama ambavyo ni vigumu kujua jina la mtoto ambaye hajazaliwa!

ni kweli mkuu, lakini kama ni mwenyeji wa sehem husika ni rahisi kumjua mmiliki.
 
Kempiski 77 arusha ndio wanaanza kujenga jaribu pitia hapo pia
 
ni kweli mkuu, lakini kama ni mwenyeji wa sehem husika ni rahisi kumjua mmiliki.

Nakushauri uende kwenye mamlaka husika kama unafanya utafiti kweli na unahitaji majibu sahihi vinginevyo utaambiwa zote zinazojengwa kila mkoa ni za Rizimoja!
 
Nakushauri uende kwenye mamlaka husika kama unafanya utafiti kweli na unahitaji majibu sahihi vinginevyo utaambiwa zote zinazojengwa kila mkoa ni za Rizimoja!

Hahahaaa, kweli mkuu kila kizuri utaambiwa riz1! Siyo utafiti wa kitaaluma mkuu, ni utafiti wa kibiashara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…