Hotuba ya JK ya Mwaka Mpya 2010


Mkuu, kwa heshima nadhani umeangalia picha bila umeme, yaani umeshindwa kabisa kufikiria kwa ukubwa.

Kumbuka investment nilizozitaja yaani kwenye elimu, kilimo na afya ni basis ya kufumua uchumi wote na kukuza kipato kwa asilimia kubwa ya asilimia 80% ya wananchi wetu wanaotegemea kilimo na kuishi vijijini.

Sasa kwa kukusaidia tu ni kwamba, kama investment ya kweli itafanyika kwenye kilimo kwa asilimia kubwa basi wananchi vijijini watakuza vipato vyao na kuweza kuinvest hizo hela kwenye mahitaji yao muhimu mfano ujenzi wa nyumba, kupeleka watoto shule, kuanzisha biashara blah blah.

wafanyabiashara watafaidika kwa kusupply vitu, serikali itafaidika kwa kupata kodi, makampuni makubwa ya simu, bia, sigara, cement nk yote yatafaidika na kuongeza investment blah blah in SHORT UCHUMI MZIMA WA NCHI UTAKUWA.

Nchi zote zilizoendelea zinajali sasa kipato cha watu wa chini sababu wao ndio wanaobeba uchumi mzima, yaani watu wa chini wakiwa hawana pesa, basi PYRAMID YOTE INADONDOKA.
 

Mtanzania ataendelea kuwa masikini ikiwa mtazamo wa Rais wa Tanzania ni kama huu na uchambuzi wake wa mfumo wetu wa uchumi na vipaumbele vitatumia mantiki ya namna hii.

Lakini naona kasahau na kujisuta kwa hilo la mwisho ka wajibu wa kufanya kazi kwa makini, bidii na maarifa zaidi.

Mpaka sasa Mheshimiwa Rais, hujaweza kumuonyesha mtu yeyote duniani kuwa unafanya kazi kwa bidii, umakini na maarifa. Uongozi wako ni wa kivivu, kizembe, kulalamika, kukosa umadhubuti, hauna ufanisi, hauna mwelekeo , hauna maadili na ni kinyume kabisa na kauli zako na hotuba unazowahadaa Wananchi kujifanya u msikivu na mwelewa wa yanayoendelea Tanzania.

Umeongelea kwa kiduchu suala la uawjibikaji na kero zinazolisumbua Taifa za uhujumu na ufisadi na athari zake kwa jamii na uchumi wetu. Sidhani kama ulidhamiria hata kulizungumzia kwa maana linakusuta kwa kuwa umekumbatia na kushikamana na wahujumu wa Uchumi na Mafisadi!

Nikirudi kwenye hili la Uchumi, unaonyesha wazi ulivyo na udwanzi wa kuelewa mambo au ni dharau yako na Serikali yako na zaidi kuwakejeli Watanzania.

Kama Mapato ya Serikali yamepungua kwa asilimia 9, Serikali imechukua hatua gani kukaza mkanda na kupunguza matumizi ili hicho kidogo kende kwenye shughuli za maendeleo ambazo ndio muhimu katika kututumua na kuinua uchumi?

Iweje leo na halii hii mbaya ya Uchumi, chini ya Uongozi wako Tanzania inaendelea kukosa umeme wa kutosha, lakini Viongzi wanaendelea kujiongezea mishahara na marupurupu, matumizi yasiyo ya lazima na bila busara kama ujenzi wa nyumba ya Gavana na mkuu wa Shirika la Tanesco yameendelea na kwa gharama kubwa, Chama chako bila aibu kimeamua kuagiza magari 200 ya kifahari ili kukisaidia kiendehse kampeni ya uchaguzi ifikapo Oktoba, na matumizi mengine mengi yasiyoleta maana wala kueleweka lakin bado unatalii dunia nzima na bakuli kuitangaza Tanzania nakuomba omba kama Mzee Matonya?

Ni heri ungekaa kimya, na umalizie hotuba yako kwa kumshukuru Mungu kama ulivyofanya katika mwanzo wa hotuba yako.

Shame on you Mr. President!
 

Kitalolo,

Rahisi (sic) anaashiria kuwa kazi iliyomshinda kwa miaka minne na ahadi zote tangu mwaka 2005, atazifanya kwa ukamilifu kwa miezi 10 ili ikifik Oktoba, achaguliwe tena.

Kama itamchukua miezi 10 kufanya kazi ya miezi 48, alikuwa anachelewa nini na wapi kufanya hilo pale alipochaguliwa? Yaani turidhike naye kwa kukosa kuwajibika na mwamko wa kupima vipaumbele na kuleta maendeleo kwa kutudumaza kwa miezi 48?

Gademu shiti!
 
Kwani chanzo cha mgao wa umeme ni nini na rais wa nchi anawezaje kumaliza shida hiyo? MImi nilidhani TZ tulishaondoka katika zile zama za kufikiri rais tu ndiye anayeweza kuleta mabadiliko nchini peke yake. Matatizo ya Tanzania ni ya jamii nzima na yanahitaji kubadilika kwa mawazo ya jamii nzima. Imetuchukua muda mrefu kufikia kwenye hiyo hali mbaya tuliyonayo sasa hivi, na sote tunaelewa kwamba sababu si JK.Tutakuwa tunajidanganya kama tunategemea rais JK aimalize kwa muda mfupi. Kama tunataka kuwa waganga wakutibu maradhi yanayoisibu Tanzania inabidi tujue chanzo na namna bora na mpya za matibabu na kuyatumia kwa vitendo. Kulaumu tu wale wanaojaribu kutoa matibabu bila kusaidia kwa vitendo, hata kama uwezo wao ni duni hakutusaidii.
 
Usafiri wa Anga



Ndugu Wananchi;


"Kwa upande wa usafiri wa anga mwaka huu Serikali imeendelea na jitihada za kuimarisha utendaji na uendeshaji wa Shirika la Ndege la Tanzania. Pamoja na hayo, pia Serikali imeendelea na mchakato wa kupata mbia wa kushirikiana nae kuendesha shirika hilo. Ni matumanini yangu kuwa mchakato huo utakamilika mapema mwaka 2010 ili shirika letu tulipe matumaini mapya ya uhai na maendeleo"



Ni dhahili kwamba wasaidizi wa Jakaya hawamuambii ukweli kuhusu muwekezaji wa kichina ambaye hata bunge liliambiwa kuwa mchakato ulikuwa umefikia hatua za mwisho wa mbia huyo kuja kuwekeza; inaelekea mchina hana nia tena ya kuja kuwekeza ATCL na ndio maana watendaji wa wizara imewawia vigumu kuwasiliana nae na mara nyingi ahadi zake huwa hazitekelezi. hili linajidhihilika pale waziri Kawambwa na katibu mkuu wake walipopitia Uarabuni wakitokea China na kuwasiliana na waarabu ili waje kuwekeza ATCL!! Bahati mbaya kwa shirika ni kwamba wizara ndio iko mstari wa mbele katika kutafuta muwekezaji na hili lina athari zake kwani watendaji wengi wa serikali wakiwamo mawaziri kama tulivyoona sio waadilifu; wizara ya miundombinu haina capacity ya kuweza kuhandle ubinafsishaji wa shirika kwahiyo kuepuka yaliyotokea enzi za SAA ni vyema exercise hii ikafanywa na wataalam wakishirikiana na bodi ya wakurugenzi. Wengi tunahisi kitendo cha wizara kutaka kuendesha mambo ya ATCL ni njia ya watendaji kutafuta upenyo wa kufanya ufisadi!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…