Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,397
- 7,974
Nimesikiliza kwa makini hotuba ya JK pale Kigoma kupitia TBC1, wakati anaongelea uchaguzi hajatamka hata mara moja neno UCHAGUZI HURU NA WA HAKI. Kaongelea uchaguzi wa amani na utulivu na kutoa mifano kibao iliyo na vitisho. Sasa Watanzania tujiulize, je uchaguzi huu utakuwa huru na wa haki kweli? Ina maana rais wa nchi hajui kuwa ktk uchaguzi huru na wa haki damu huwa haimwagiki??? Nina mashaka makubwa na dhamira ya JK kuendesha uchaguzi huru na wa haki kwa kuwa neno hilo hajalitamka hata mara moja leo, huenda dhamira inamshitaki kutokana na mipango ya nyuma ya pazia kuchakachua uchaguzi.