Hotuba za mwalimu zinapatikana wapi?

Chambusiso

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2007
Posts
2,592
Reaction score
4,640
Siku nyingi sana najaribu kutafuta hotuba za mwalimu zile zilizokuwa zinatolewa kwenye ujumbe wa leo RTD enzi zake kwenye media yoyote Audio CD, cassetes, DVD etc. Ninapenda sana kusikiliza hizi record na kupata ujumbe lakini zinazopatikana ni chache na ni vipande vidogo vidogo. Najua wappo wengi wanaopenda zipatikane kwa njia yoyote kwa wananchi na watu tunaomuona kama mkombozi wa Tanzania tupate ule ujumbe na falsafa zake. Siku zote falsafa za kiongozi zinapatikana vizuri zaidi unaporudia kuzisikia na kuzisoma kazi zake mbalimbali.

Najua katika Tanzania ya leo ya mafisadi hakuna mwenye ujasiri wa kusikiliza ndani ya serikali na ni mwiba mkali kwa viongozi waliopo kusikiliza, nategemea wao ndio source kubwa ya kufanya zifichwe

Iwe ni familia yake, TBC, Serikali, Tasisi ya Mwalimu yoyote anayehusika hebu toeni kazi za mwalimu tutazinunua!! Waache ubinafsi wa kizificha tunataka elimu iliyopo tuichote na kuitumia. Watanzania tusipoangalia historia ya huyu mtu muhimu kwa nchi yetu ndio inazikwa hivyo jamani, kwa maslahi ya ubinafsi. Watawala hawataki kabisa kuona watu wanasikiliza ujumbe huu.

Ingewezekana kuelekea uchaguzi mkuu zipatikane in public kwa wingi najua watu watapata hekima iliyopo. Hebu kumbuka aliposema CCM si mama yangu! Watu wakipata ujumbe kama huu atakapokuja Makamba kusema CCM ni ya Nyerere, watu watakuwa na kitu cha kukumbuka mwenyewe alisemaje. Hebu kanzi katusaidie vyovyote

Nawakilisha
 
TBC

Vile vile unaweza kupata nyingine kwenye blog ya SUBI sikumbuki link yake, wewe google "subi"
 
Mwacheni nyerere.......

Kama hamuwezi kupata majibu ya matatizo ya nchi hii bila nyerere
then acheni mafisadi watawale...

Nyerere nyerere.
Enough...................
 
The Boss,
Obama alipokuwa anajiandaa kugombea urais alimulika zaidi marais watatu katika historia ya Marekani: Abraham Lincoln, Theodore Roosevelt na John F. Kennedy. Nyerere ni part of our history na kuna mengi aliyoyasema ambayo leo yanaonekana kuwa na mantiki zaidi.
 
Itikadi ya kuwanyima wananchi haki ya kumiliki vitega uchumi na kujiajiri utakusaidia kitu gani?

Katika Uislamu kuna nguzo inaitwa 'zakat', yaani kila mwenye mali lazima azote 2.5% ya mali yake kusaidia masikini. Huu ni ushahidi wa wazi kwamba Mungu ameruhusu watu kumiliki mali iliyopatikana kihalali. Nyerere msimamo wake ni kwamba kumiliki mali ni dhambi. Hata Yesu hakuwa na tatizo na biashara, alichokemea Yesu ni riba (usury).

Sisi wanafunzi wa maswala ya dini tuliamini kwa asilimia 100% kwamba Azimio la Arusha lingechemsha.

Binaadamu hawezi kuamka asubihi kwenda kufanya kazi kwa ajili ya wengine, watu hujituma kwa ajili yao wenyewe na wale walio muhimu kwao. Hii ni reality na Serikali inaweza ku capitalize na hii reality kwa kuwa na mfumo mzuri wa kodi sio kutaka kila mtu (mvivu na mchapa kazi) wawe sawa kimaendeleo.
 
Niliwahi kusikia kuwa jamaa wa TANAPA ndio waliopewa jukumu la kuhifadhi kumbukumbu zote za Nyerere, that means hata hizi hotuba huenda watakuwa nazo kwa wingi kabisa. So jaribu kufanya nao mawasiliano unaweza kupata ufumbuzi.
 
Tatizo hapa kwetu sera zina nafasi ndogo sana wakati nchi inapotakiwa kufikiria aina ya kiongozi anayetakiwa, ndio maana hata Nyerere anaonekana kama kichekesho anapotajwa siku hizi. Kinachopewa kipaumbele siku hizi ni fedha na uwezo wa kuwapiga zengwe wagombea wengine.
 

hujazitafuta acha unafiki....
 
Mwacheni nyerere.......

Kama hamuwezi kupata majibu ya matatizo ya nchi hii bila nyerere
then acheni mafisadi watawale...

Nyerere nyerere.
Enough...................

Nimekusoma Kamanda, matatizo yenu myamalize wenyewe, nyerere mwacheni apumzike, kama hamuwezi kuyatatua mkae kimya milele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…