House4Rent House for rent needed, budget TZS 18,000,000

House4Rent House for rent needed, budget TZS 18,000,000

Joined
Dec 26, 2016
Posts
17
Reaction score
106
Natafuta nyumba ya kupanga maeneo ya Mikocheni au Mbezi Beach kwa bajeti ya Sh. 1,600,000 per month.

Nipo tayari kulipa kodi ya mwaka.

Kama kuna mwenye kuwa na nyumba ambayo angalau ina vyumba 4 na inaendana na bajeti hii nitashukuru.
 
Mwenye nayo tafadhali tuwasiliane hapa JF. Hiyo 1,600,000 ni maximum I can pay kwa mwezi.

Asante
 
Upo serious au umekuja kupima upepo wa wenye hasira na uncle Juma? Hivi kwa bajeti hiyo ya 1.6m pm umekosa kweli? Mbezi beach maghorofa kibao yana fence,perving block,garden wanataka kilo 8 hadi mita moja.
Unaweza usiamini, nimezungushwa na madalali wananionyesha nyumba zinazokatisha tamaa.

Mbaya zaidi hawataki umjue mwenye nyumba
 
Unaweza usiamini, nimezungushwa na madalali wananionyesha nyumba zinazokatisha tamaa.

Mbaya zaidi hawataki umjue mwenye nyumba
njoo pm mkuu achana na madalali uchwara utakuja kutoa ushuhuda huku mbezi beach nyumba kibao ila mikocheni kwa bei hyo huwezi pata room nane kwa dollar 800
 
  • Thanks
Reactions: MC7
Kama Haujapata nistue nikuunge na Jamaa yangu akupe nyumba mbezi beach inayoendana na bajeti hiyo.
Sijapata mkuu wangu. Nazungushwa kwenye nyumba zipo location za ajabu tu.

Madalali ninaounganishwa nao wanakupeleka nyumba wanakwambia $2,500 per month, baada ya siku 4 wanakwambia imeshuka ni $1,500 na hata wanakuwa wamemwandaa landlord anasimamia same figure hataki kusikia kitu.

Wanakatisha tamaa
 
1,600,000 per month. Hii figure wengi tunaiandika tu ofisini wala hatujawahi kuifikiria kwenye bank account zetu, sasa kama wewe unalipia kodi kwa mwezi, heshma mkuu.
Hadi nakosa nyumba. Ujue bado ni kidogo (kwa viwango vya wenye nyumba zao)
 
It seems your standards of living are quiet high mkuu.
Mkuu,

Ujue nilishapanga room 1, enzi hizo nikilipia 15,000/- kwa mwezi.

Maisha yanabadilika, na unaona hata kwa hela hiyo unayodhani ni kubwa bado sipati nyumba sahihi. Manake wananitaka nitoe zaidi ya 2,000,000 kwa mwezi ndo angalau nifikie viwango vyao
 
Mkuu,

Ujue nilishapanga room 1, enzi hizo nikilipia 15,000/- kwa mwezi.

Maisha yanabadilika, na unaona hata kwa hela hiyo unayodhani ni kubwa bado sipati nyumba sahihi. Manake wananitaka nitoe zaidi ya 2,000,000 kwa mwezi ndo angalau nifikie viwango vyao
Duuuh kodi ya nusu mwaka hiyo
 
Back
Top Bottom