Huawei wamezindua luxury EV sedan Maextro S800: Copy na Paste ya Maybach kwa nusu bei ila more tech!

Huawei wamezindua luxury EV sedan Maextro S800: Copy na Paste ya Maybach kwa nusu bei ila more tech!

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Huawei wakiwa wameungana na JAC wamezindua gari yao ya kwanza inayoenda kwa model name Maextro, ikiwa na lengo la kushindana na Maybach na Rolls.
IMG_0747.jpeg
IMG_0748.png
IMG_0749.jpeg

Kuhusu bei, itauzwa kuanzia $140,000 tu, na ndio itakua gari ya bei kali kuliko zote kutoka China hadi leo.
IMG_0750.jpeg
 
Speed ya Mchina ni kubwa sana, ila bidhaa zake kushindana na Ulaya au North America nadhani bado sana
Pasipo kuzipiga ban amini nakwambia alikuwa anaenda kushindana nao. Ulaya wamepiga tarrif ya about nadhani 40% ya EVs za china kwa sababu zilikuwa zishaanza kuingia kwao kwa sababu ya pricing techniques.
Mchina ana speed sana now huawei hawa hawa wame patent technology mpya ya lithography ikiwa na maana wanaweza siku za mbele wakawa wapinzani wa ESML.
 
Pasipo kuzipiga ban amini nakwambia alikuwa anaenda kushindana nao. Ulaya wamepiga tarrif ya about nadhani 40% ya EVs za china kwa sababu zilikuwa zishaanza kuingia kwao kwa sababu ya pricing techniques.
Mchina ana speed sana now huawei hawa hawa wame patent technology mpya ya lithography ikiwa na maana wanaweza siku za mbele wakawa wapinzani wa ESML.
Huawei mpaka 2025 bado atakuwa anatumia 7nm wakati hadi sasa kina TSMC wapo kwenye 3nm.

Tatizo la teknolojia unafukuzia iliyopo lakini na iliyopo bado inakuzwa. Sasa hivi Huawei wakipambana wakijitahidi sana wanatoa chip inayolingana na Qualcomm Snapdragon 888 Gen. 1 ya miaka minne iliyopita. Qualcomm wameishatoa Gen 2, Gen 3 na sasa wapo Elite na kila mwaka wanatoa.

China anabidi apate breathrough kwenye lithography na wafers ambazo bado tpe muda. Nimeona Xiaomi wanataka kuwa na processors zao lakini njia ni zilezile kutoka American patents.
 
Huawei mpaka 2025 bado atakuwa anatumia 7nm wakati hadi sasa kina TSMC wapo kwenye 3nm.

Tatizo la teknolojia unafukuzia iliyopo lakini na iliyopo bado inakuzwa. Sasa hivi Huawei wakipambana wakijitahidi sana wanatoa chip inayolingana na Qualcomm Snapdragon 888 Gen. 1 ya miaka minne iliyopita. Qualcomm wameishatoa Gen 2, Gen 3 na sasa wapo Elite na kila mwaka wanatoa.

China anabidi apate breathrough kwenye lithography na wafers ambazo bado tpe muda. Nimeona Xiaomi wanataka kuwa na processors zao lakini njia ni zilezile kutoka American patents.
Elon musk aliwahi cheka alipoambiwa BYD inataka kutengeneza EV akaulizwa kama anahisi italeta challenge kwake.
Intel waliwahi kuona TSMC ni underdog kiasi kwamba wao wamehusika sana kutengeneza tech ya lithography halafu hawakuitumia, sasa TSMC ikaanza kuitumia kabla yao na sasa ni kama wamebaki nyuma sana wameshindwa kuendana tena na ushindani.
CEO wa ESML baada ya kusikia kuwa china kapatent tech ya lithography, kasema kabisa in the tech world never say never.
 
Ushindani ni mzuri na maendeleo ni mazuri ila hii ya kucopy alichofanya mwenzako tena kionekane vilevile haiko sawa.

Huko ni kujidumaza. Maana yake ikiwa watahitaji kupita kwenye njia zao wenyewe inaweza isiwaletee matunda.

Toyota wakaja na Toyota Century hii ni copy ya Rolls Royce Cullinan nadhani...

Hii kitu ya kucopy itadumaza akili zako na kumfanya uliyemcopy aonekane Bora Kila muda.
 
Ushindani ni mzuri na maendeleo ni mazuri ila hii ya kucopy alichofanya mwenzako tena kionekane vilevile haiko sawa.

Huko ni kujidumaza. Maana yake ikiwa watahitaji kupita kwenye njia zao wenyewe inaweza isiwaletee matunda.

Toyota wakaja na Toyota Century hii ni copy ya Rolls Royce Cullinan nadhani...

Hii kitu ya kucopy itadumaza akili zako na kumfanya uliyemcopy aonekane Bora Kila muda.
Shida unakuta designer wa magari walioajiriwa na hayo makampuni ndio waliokuwa hao hao madesigner wa magari huko europe.
 
Elon musk aliwahi cheka alipoambiwa BYD inataka kutengeneza EV akaulizwa kama anahisi italeta challenge kwake.
Intel waliwahi kuona TSMC ni underdog kiasi kwamba wao wamehusika sana kutengeneza tech ya lithography halafu hawakuitumia, sasa TSMC ikaanza kuitumia kabla yao na sasa ni kama wamebaki nyuma sana wameshindwa kuendana tena na ushindani.
CEO wa ESML baada ya kusikia kuwa china kapatent tech ya lithography, kasema kabisa in the tech world never say never.
Sijasema haiwezekani nimesema tuwape muda. Wakati wanaanza kuna wanaoendelea kwahiyo ushindani utaendelea kuwepo na hatua zinachukuliwa na kila mmoja. Hii assumption ya kuamini Wachina ndio wako kwenye research peke yao ni ya makosa.

Huawei wametoa Mate 70 Pro jana na ina 7nm node. Qualcomm node yao ya 7nm ilikuwa 2019 na kila mwaka wanashusha nanometers kuzidisha performance. Mwaka huu wana 3nm, mwakani bado Huawei atakuwa na 7nm alafu labda Qualcomm wawe na 2nm. Unamkimbiza anayekimbia.

Miaka kadhaa ndio wanaweza kuwa sawa ila sio haraka hivyo.
 
Shida unakuta designer wa magari walioajiriwa na hayo makampuni ndio waliokuwa hao hao madesigner wa magari huko europe.
Mkuu Kwa namna hii ikiwa wanaonyesha wazi haya machache Kwa nje Yale waliyocopy basi Yale waliyocopy ambayo hawatuoneshi ni mengi zaidi.

Mtu wa aina hiyo daima ni mtumwa, hawezi kuwa huru.
 
Sijasema haiwezekani nimesema tuwape muda. Wakati wanaanza kuna wanaoendelea kwahiyo ushindani utaendelea kuwepo na hatua zinachukuliwa na kila mmoja. Hii assumption ya kuamini Wachina ndio wako kwenye research peke yao ni ya makosa.

Huawei wametoa Mate 70 Pro jana na ina 7nm node. Qualcomm node yao ya 7nm ilikuwa 2019 na kila mwaka wanashusha nanometers kuzidisha performance. Mwaka huu wana 3nm, mwakani bado Huawei atakuwa na 7nm alafu labda Qualcomm wawe na 2nm. Unamkimbiza anayekimbia.

Miaka kadhaa ndio wanaweza kuwa sawa ila sio haraka hivyo.
Mkuu unachopaswa kukumbuka, ni kwamba walipotoa hiyo 7nm ilikuwa story wamewezaje hata kutengeneza kitu hicho ndani ya muda mfupi baada ya vikwazo. Yani hiki kitu haikuwachukua hata miaka 4 kuweza kufanya hivyo. Kumbuka ilikuwa inatabiriwa wataweza walau kubreak through mwaka 2027 wengine hadi wakisema 2030.
So, mchina si wa mchezo mchezo. Leo nilikuwa natazama documentary kwanini japan ilitoka kuwa na 50% market share duniani kote mpaka now kuwa kama haiko kwenye hilo game. Toshiba ilikuwa among the leading semi conductor manufacturers. Mwisho kumbe aliyeiua ni US. It seems US hataki kampuni kutoka kwingine ziwe ahead kwenye technology fulani.
Wanasema alichokifanya kwa Japan, ndicho anachojaribu kufanya kwa china bahati mbaya china kajiandaa na amechelewa kumuwahi.
 
Mkuu Kwa namna hii ikiwa wanaonyesha wazi haya machache Kwa nje Yale waliyocopy basi Yale waliyocopy ambayo hawatuoneshi ni mengi zaidi.

Mtu wa aina hiyo daima ni mtumwa, hawezi kuwa huru.
Ni trend tu ya mwonekano wa magari siku hizi ni kama magari mengi yanafanana. But narudi pale pale makampuni ya china yameajiri wa designer waliokuwa wana design kwenye kampuni kubwa za ulaya ndo madesigner wa magari mengi mashuhuri.
China is a copycat, but copycat yake now imekuwa next level kiasi kwamba inaua bidhaa genuine ambazo zinakuwa za bei kali.
 
Huawei mpaka 2025 bado atakuwa anatumia 7nm wakati hadi sasa kina TSMC wapo kwenye 3nm.

Tatizo la teknolojia unafukuzia iliyopo lakini na iliyopo bado inakuzwa. Sasa hivi Huawei wakipambana wakijitahidi sana wanatoa chip inayolingana na Qualcomm Snapdragon 888 Gen. 1 ya miaka minne iliyopita. Qualcomm wameishatoa Gen 2, Gen 3 na sasa wapo Elite na kila mwaka wanatoa.

China anabidi apate breathrough kwenye lithography na wafers ambazo bado tpe muda. Nimeona Xiaomi wanataka kuwa na processors zao lakini njia ni zilezile kutoka American patents.
Unawajua wachina lakini wakikomalia jambo lao ?

Kwa vikwazo alivyowekewa Huawei ilipaswa kufa siku nyingi sana.

Huawei wapo na ushirikiano sasa na SMIC

Na serikali ya Beijing imeliamulia suala la chips ni agenda ya kitaifa.

Walichokifanya kwenye clean energy ndicho kinacho enda kutokea kwenye Chips suala la muda tu subiri kuona matokeo uzuri MSS hawalali.
 
Sijasema haiwezekani nimesema tuwape muda. Wakati wanaanza kuna wanaoendelea kwahiyo ushindani utaendelea kuwepo na hatua zinachukuliwa na kila mmoja. Hii assumption ya kuamini Wachina ndio wako kwenye research peke yao ni ya makosa.

Huawei wametoa Mate 70 Pro jana na ina 7nm node. Qualcomm node yao ya 7nm ilikuwa 2019 na kila mwaka wanashusha nanometers kuzidisha performance. Mwaka huu wana 3nm, mwakani bado Huawei atakuwa na 7nm alafu labda Qualcomm wawe na 2nm. Unamkimbiza anayekimbia.

Miaka kadhaa ndio wanaweza kuwa sawa ila sio haraka hivyo.
Tatizo sio kumkimbiza anaye kimbia ila anaye kukimbiza anakimbia kwa namna gani ?

Uzuri ni kuwa mzungu anashindana na watu wenye akili sisi ni kufurahia tu kuona ushindani wao kwa manufaa ya dunia.

Miracle tu China waliyofanya kwenye maendeleo kwa kipindi kifupi haikuwahi kufanywa na taifa lolote lile.
 
Unawajua wachina lakini wakikomalia jambo lao ?

Kwa vikwazo alivyowekewa Huawei ilipaswa kufa siku nyingi sana.

Huawei wapo na ushirikiano sasa na SMIC

Na serikali ya Beijing imeliamulia suala la chips ni agenda ya kitaifa.

Walichokifanya kwenye clean energy ndicho kinacho enda kutokea kwenye Chips suala la muda tu subiri kuona matokeo uzuri MSS hawalali.
Clean energy kutengeneza solar na wind turbines ni dedication na mtaji. Chip making ni science kali mno na investment ya muda sio unaweka hela miaka mitatu unataka uwe zaidi ya uliowakuta.

Huawei asingekufa bali alipunguzwa nguvu, kuzuiwa kutumia Android na kuzuiwa the best microchip tech hakungeifanya ife wakati China tu ina mamia ya mamilioni ya wateja ambao hawatumii Android na si lazima watumie best performing microchips. Mengineyo Huawei alibaki nayo kama screen tech, battery, camera, 4G na 5G ambayo hii ya mwisho ndio mbabe wake.
 
Tatizo sio kumkimbiza anaye kimbia ila anaye kukimbiza anakimbia kwa namna gani ?

Uzuri ni kuwa mzungu anashindana na watu wenye akili sisi ni kufurahia tu kuona ushindani wao kwa manufaa ya dunia.

Miracle tu China waliyofanya kwenye maendeleo kwa kipindi kifupi haikuwahi kufanywa na taifa lolote lile.
China kuendelea sio miracle, usipumbazwe na upuuzi wa sisi Waafrika kutoendelea ukaona ndio standard ya dunia.

China ina watu wa jamii almost moja, ina watu wengi zaidi ya 1.3 billion ambao ni wazalishaji na wanunuzi wao wenyewe, ina eneo kubwa la kijiografia, ina maliasili nyingi mno kuanzia chuma, rare earth metals, makaa ya mawe, mafuta, gesi, ardhi ya kutosha, mito mikubwa mno kama Yangtze na mto wa njano, ina maporomoko mengi makubwa ya maji yanayozalisha umeme na kumwagilia mashamba, ina kanda tofauti za kilimo na misimo tofauti na hali ya hewa tofauti inayostawisha mazao mbalimbali kwa misimu tofauti.

China ina kila kitu cha kuifanya iwe bora. Ni kama India iwe kubwa kiuchumi alafu watu waanze kushangaa wakati ina advantage nyingi tu. Maajabu ni mfano Iceland au Israel kuwa kubwa kiuchumi, sio China.
 
Clean energy kutengeneza solar na wind turbines ni dedication na mtaji. Chip making ni science kali mno na investment ya muda sio unaweka hela miaka mitatu unataka uwe zaidi ya uliowakuta.

Huawei asingekufa bali alipunguzwa nguvu, kuzuiwa kutumia Android na kuzuiwa the best microchip tech hakungeifanya ife wakati China tu ina mamia ya mamilioni ya wateja ambao hawatumii Android na si lazima watumie best performing microchips. Mengineyo Huawei alibaki nayo kama screen tech, battery, camera, 4G na 5G ambayo hii ya mwisho ndio mbabe wake.
Kama ambavyo clean energy ilikuwa moja ya national plans ndivyo ilivyo kwenye chips sio mpango wa leo wala jana bali toka 2010s huko.

Na clean energy usichukulie kiwepesi tu kuwa ni dedication na mtaji tu rahis tu hivyo pasipo umuhimu wa teknolojia
 
China kuendelea sio miracle, usipumbazwe na upuuzi wa sisi Waafrika kutoendelea ukaona ndio standard ya dunia.

China ina watu wa jamii almost moja, ina watu wengi zaidi ya 1.3 billion ambao ni wazalishaji na wanunuzi wao wenyewe, ina eneo kubwa la kijiografia, ina maliasili nyingi mno kuanzia chuma, rare earth metals, makaa ya mawe, mafuta, gesi, ardhi ya kutosha, mito mikubwa mno kama Yangtze na mto wa njano, ina maporomoko mengi makubwa ya maji yanayozalisha umeme na kumwagilia mashamba, ina kanda tofauti za kilimo na misimo tofauti na hali ya hewa tofauti inayostawisha mazao mbalimbali kwa misimu tofauti.

China ina kila kitu cha kuifanya iwe bora. Ni kama India iwe kubwa kiuchumi alafu watu waanze kushangaa wakati ina advantage nyingi tu. Maajabu ni mfano Iceland au Israel kuwa kubwa kiuchumi, sio China.
Miracle inayo shangaza na kuweka historia ni kipindi kifupi walicho tumia kupata maendeleo yote katika historia hakuna nchi iliyowahi kufanya hivyo jambo ambalo hata kwa India limeshindikana sizungumzii miujiza ya mwamposa hapa.
 
Miracle inayo shangaza na kuweka historia ni kipindi kifupi walicho tumia kupata maendeleo yote katika historia hakuna nchi iliyowahi kufanya hivyo jambo ambalo hata kwa India limeshindikana sizungumzii miujiza ya mwamposa hapa.
Singapore ndio walipata maendeleo muda mfupi bila rasilimali, hayo ndio maajabu. China wana sababu za kuwa na maendeleo kila kitu kilichofanya waendelee hakijatoka nje labda FDI.

Japan kwa mfano kila kitu kinachofanya wawe na uchumi mkubwa walikitafuta nje kwa gharama. China ina vitu kibao inavyo bure hapo kwake.
Ni kama Marekani tu, ina neema ilijikuta nazo ikaendelea juu kwa juu tofauti na Uingereza vitu vingi sana ilifuata nje hadi watumwa, hadi makoloni. Uingereza hata viungo vya chakula ilifuata India.
 
Mchina anachofanya ni sahihi?hayo magari ya Europe wameyaover overprice ,mfano engine ya Maybach Ndio ipo kwa Mercedes s class,zaidi maybach wanakuuzia fenichaza ndani tu ambazo mchina Ana design nzuri tu kushinda wao
 
Back
Top Bottom