Huawei yageukia kwenye ufugaji wa nguruwe kutokana na kushuka kwa mauzo ya smartphone

Huawei yageukia kwenye ufugaji wa nguruwe kutokana na kushuka kwa mauzo ya smartphone

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2016
Posts
5,500
Reaction score
8,060
Habari!

Kampuni kubwa ya teknolojia ya Kichina Huawei (Huawei Technologies Co., Ltd.) imezindua mradi wa ufugaji wa nguruwe kupitia teknolojia ya Akili Bandia (Artificial Intelligence) Jumatatu wakati kampuni hiyo ikigeukia katika maeneo mengine ya kibiashara wakati biashara yake ya simu janja (smartphone) ikikabiliwa na vikwazo vya kibiashara vya Marekani.

Kampuni hiyo kubwa ya simu nchini China ilizuiliwa kupata vifaa muhimu vinavyotumika katika uzalishaji wa bidhaa zake za simu janja baada ya serikali ya Trump kuitangaza kampuni hiyo kuwa tishio kwa usalama wa kitaifa wa Marekani.

Mauzo ya simu janja za Huawei yaliporomoka kwa 42% katika robo ya mwisho ya mwaka 2020 kutokana na upatikanaji hafifu wa vifaa muhimu vinavyofahamika kama 'microchips' kulikotokana na vikwazo hivyo.

Kutokana na kudorora huko kwa mauzo ya simu janja, Huawei inatafuta vyanzo vingine vya mapato kwa teknolojia yake. Pamoja na teknolojia ya Akili Bandia kwa wafugaji wa nguruwe, Huawei pia inafanya kazi na sekta ya madini ya makaa ya mawe.

Kwa upande wa teknolojia mpya ya mawasiliano ya 5G, vikwazo pia vimeiathiri Huawei kupata baadhi ya vifaa muhimu vya usimikaji wa mtandao huo huku pia ikizuiliwa kuhusika katika usimikaji wa mtandao wa 5G katika nchi kadhaa kutokana na hofu juu ya usalama wa kitaifa.

Kwa taarifa zaidi kuhusiana na hili, waweza kuzipata kupitia vyanzo vifuatavyo:

1) BBC | Huawei turns to pig farming as smartphone sales fall
2) South China Morning Post | Huawei turns to AI pig farming as the Chinese tech giant explores new growth areas outside smartphones
 
Cha mtu MAVI baada ya kupigwa stop kwenye wizi wa technology waliokuwa wakiufanya hasa USA sasa hawana jipya. Quarter ya kwanza baada ya Apple kutoa iPhone 12 sales zao zilivunja rekodi.
Kampuni kubwa ya teknolojia ya Kichina Huawei (Huawei Technologies Co., Ltd.) imezindua mradi wa ufugaji wa nguruwe kupitia teknolojia ya Akili Bandia (Artificial Intelligence) Jumatatu wakati kampuni hiyo ikigeukia katika maeneo mengine ya kibiashara wakati biashara yake ya simu janja (smartphone) ikikabiliwa na vikwazo vya kibiashara vya Marekani.

Kampuni hiyo kubwa ya simu nchini China ilizuiliwa kupata vifaa muhimu vinavyotumika katika uzalishaji wa bidhaa zake za simu janja baada ya serikali ya Trump kuitangaza kampuni hiyo kuwa tishio kwa usalama wa kitaifa wa Marekani.

Mauzo ya simu janja za Huawei yaliporomoka kwa 42% katika robo ya mwisho ya mwaka 2020 kutokana na upatikanaji hafifu wa vifaa muhimu vinavyofahamika kama 'microchips' kulikotokana na vikwazo hivyo.

Kutokana na kudorora huko kwa mauzo ya simu janja, Huawei inatafuta vyanzo vingine vya mapato kwa teknolojia yake. Pamoja na teknolojia ya Akili Bandia kwa wafugaji wa nguruwe, Huawei pia inafanya kazi na sekta ya madini ya makaa ya mawe.

Kwa upande wa teknolojia mpya ya mawasiliano ya 5G, vikwazo pia vimeiathiri Huawei kupata baadhi ya vifaa muhimu vya usimikaji wa mtandao huo huku pia ikizuiliwa kuhusika katika usimikaji wa mtandao wa 5G katika nchi kadhaa kutokana na hofu juu ya usalama wa kitaifa.

Kwa taarifa zaidi kuhusiana na hili, waweza kuzipata kupitia vyanzo vifuatavyo:
1) BBC | Huawei turns to pig farming as smartphone sales fall
2) South China Morning Post | Huawei turns to AI pig farming as the Chinese tech giant explores new growth areas outside smartphones
 
Mchina ni multipurpose katumwa hela. Nguruwe huko kwao nayo ni biashara kubwa sana maana ndo kama mboga ya taifa, watapata wafugaji wengi kuwauzia hizo teknolojia na zikitick huko kwao lazima watazisambaza kwa wakina sie biashara inaendelea. Uzuri makampuni yao karibia mengi kwa ndani mmiliki ni yuleyule c...c....p. Hata wakiendelea wakina xiaomi na oppo familia moja
 
Cha mtu MAVI baada ya kupigwa stop kwenye wizi wa technology waliokuwa wakiufanya hasa USA sasa hawana jipya. Quarter ya kwanza baada ya Apple kutoa iPhone 12 sales zao zilivunja rekodi.
iSheep
 
Mchina ni multipurpose katumwa hela.......nguruwe huko kwao nayo ni biashara kubwa sana maana ndo kama mboga ya taifa....watapata wafugaji wengi kuwauzia hizo teknolojia na zikitick huko kwao lazima watazisambaza kwa wakina sie biashara inaendelea........uzuri makampuni yao karibia mengi kwa ndani mmiliki ni yuleyule c...c....p. ...hata wakiendelea wakina xiaomi na oppo familia moja
Kama alikuwa anajua kwamba nguruwe zinalipa kwanini alikuwa anatengeneza smart phone.
 
Kama alikuwa anajua kwamba nguruwe zinalipa kwanini alikuwa anatengeneza smart phone
Fursa......mlango ukifungwa unaangalia mwingine........biashara alizokua anafanya sio smartphone tu maana upande wa mitandao hasa 5G kwa huku Africa sijajua kama kuna namna ya kumkwepa, soko bado analo na hata huko asia...................halafu Huawei na kampuni nyingine za china na Korea zinampango wa kwenda kuanzisha viwanda vya simu Uturuki....acha tuone hii karata itaenda vipi
 
Pia imewekeza kwenye artificial coal mining
 
Baada ya miaka kadhaa mtarudi hapa mkishangaa China kuwa kiongozi katika ufugaji wa mdudu na uzushi kibao kuwa haiwezekani, China kaiba teknolojia. Wachina wanaanzaga bizness hivi hivi kama utani ila baada ya muda ni world leaders kwenye issue husika
 
Baada ya miaka kadhaa mtarudi hapa mkishangaa China kuwa kiongozi katika ufugaji wa mdudu na uzushi kibao kuwa haiwezekani, China kaiba teknolojia. Wachina wanaanzaga bizness hivi hivi kama utani ila baada ya muda ni world leaders kwenye issue husika
Hata kwenye smartphone Huawei alianza kimzaha tu , baadae wanashtuka ameshawakaba kooni
 
Back
Top Bottom