Huawei yageukia kwenye ufugaji wa nguruwe kutokana na kushuka kwa mauzo ya smartphone

Baada ya miaka kadhaa mtarudi hapa mkishangaa China kuwa kiongozi katika ufugaji wa mdudu na uzushi kibao kuwa haiwezekani, China kaiba teknolojia. Wachina wanaanzaga bizness hivi hivi kama utani ila baada ya muda ni world leaders kwenye issue husika
So far mchina hajawahi kuwa world leader kwenye tech yoyote , yeye anachokifanya ni kuweka juhudi ya kutengeneza product zake kwa kutumia tech za wenzake iligally au legally ndo maana akibanwa anakosa namna . Huawei sio kampuni ya kwanza kufanyiwa hivyo , hata ZTE aliwahi banwa na kapotea . Na mbinyo ukiendelea kampuni za electronic nyingi za china zitapotea
 
Maskini Huawei...
 
Hata kwenye smartphone Huawei alianza kimzaha tu , baadae wanashtuka ameshawakaba kooni
Wakati Huawei yupo juu, simu zake zilikuwa zinatumia vioo vya Gorilla ,kutoka Corning Inc ya new york
Na sio yeye tu , Hadi leo hao best sellers xiaomi , oppo and the like wapo busy kusifia how latest gorrila glass they have kwenye simu zao, na. Ni selling factor kubwa
 
Wakati Huawei yupo juu, simu zake zilikuwa zinatumia vioo vya Gorilla ,kutoka Corning Inc ya new york
Ishu kwao mauzo, tech iwe yao ama ya kuiba ishu ni sales tu kwao
 
Yani wewe ni bora tu uonekane umetetea Huawei?

Hujui makampuni hayo ya simu wamiliki ni mabeberu? Au unamaanisha TTCL anaweza leta teknolojia hiyo na kumuinulia mapato Huawei?

Yes Uturuki ni sawa na utakua unajenga uchumi wa Uturuki kiasi kikubwa kuliko wa China, Ni sawa na wewe mtanzania ukafungue kiwanda Kenya unafikiri atakaefaidika ni TZ au KE?
 
Sio glass za gorilla tu mkuu hadi hizo chip zao za kichina za MTK hawazipi kipaumbele kabisa na wametumia kwenye cm chache sana.
 
Iphone zimetengenezwa China .....Mmarekani hakua anafaidika? Wameshapiga hesabu zao wameona watafaidika vipi.........sio lazima ubebe 100% yote mambo ndo yanaenda hivo blaza acha kukariri....kwani huawei ndo itakua kampuni ya kwanza kufanya hivyo?
 
Iphone zimetengenezwa China .....Mmarekani hakua anafaidika? Wameshapiga hesabu zao wameona watafaidika vipi.........sio lazima ubebe 100% yote mambo ndo yanaenda hivo blaza acha kukariri....kwani huawei ndo itakua kampuni ya kwanza kufanya hivyo?
Iphone haitengenezwi china mkuu bali Iphone inakua assembled China, sijui kama unaelewa maana ya ku assemble mkuu. Na ni kazi ya vibarua wengi wa bei nafuu inatumika kuunganisha vipande toka kampuni ya Foxconn China. Pesa ya kubwa kwenye investment huwa haiendi mbali na USA.

Na kwa Taarifa yako hao Foxconn wameanza kuunganisha vipande vya simu hizo India pia sababu kuna vibarua nafuu. Marekani huwezi pata vibarua wengi kwa gharama nafuu sababu malipo yao kwa lisaa ni makubwa sana.
 
Huawei anaenda kufanya nini uturuki? Na hizo parts wanazo assemble zinatengenezwa wapi pia?angalia parts zote za iphone kuanzia chipset zinatengenezewa wapi
 
Jambo la msingi ni FOCUS.

Hata Apple baada ya kumfukuza Steve Jobs walianzisha fashion store.

Lakini je, hiyo ndio ilikuwa mission ya kampuni ???
 
Mchina ni mzuri zaidi kwenye ku-apply modern technology kuendana na mahitaji kuliko kufanya innovation. Na tech firms hasa za nchi za magharibi zinapo-innovate tech zao zinakuwa na hakimiliki (patents). Ili kuipata teknolojia husika ni lazima uilipie ama uingie makubaliano na mmiliki ili kupata leseni ya uzalishaji katika kampuni yako.

Madhara yake ni kuwa, ukifutiwa leseni tu ya matumizi ya hiyo teknolojia kwa sababu zozote zile, huwezi tena kuendelea kuitumia hiyo teknolojia katika uzalishaji wa bidhaa yako kwa sababu pia utakosa suppy ya components muhimu zinazohusika katika hiyo teknolojia. Hili ndilo linaloikabili Huawei kwa sasa.
 
Huawei ni mzuri katika telecommunication hardware components toka zamani lakini tatizo moja linalowakabili ni kwamba, asilimia kubwa ya teknolojia yao wanayoitumia katika core components zao wanaitoa kutoka nchi za magharibi.
 
Ishu kwao mauzo, tech iwe yao ama ya kuiba ishu ni sales tu kwao
Kuiba tech ni kosa kisheria, it's a matter of time kabla ya wenyewe kukushughulikia. Intellectual property za watu hizo. Kuna watu wamepigika, usiku na mchana wameumiza vichwa ili ku-innovate alafu atokee mtu fulani ale jasho lao kiwepesi hivyo!
 

Source: BBC, mkuu unategemea nini kutoka kwenye media ambazo ni overly obsessed kwa kubeza kuhusu maendeleo ya kisayansi,teknolojia na kijeshi ya Uchina - lini waliwahi kutuletea habari nzuri kuhusu Uchina?

Mauzo ya smartphone yanaweza kuwa yamepungua kidogo, lakini hata siku moja Huawei haiwezi kuteteleka hata kidogo,wanejiwekea safety net kila kona, actually service providers wa cellphone network wenye akili wanaendelea kutumia system za Huawei 5G,hawasikilizi tena propaganda za USA zenye lengo la kumwaribia biashara Huawei kwa kuwa USA inajua hiko nyuma sana kwenye teknolojia hii ya mawasiliano ambayo ni hot cake, tatizo hapo ni ushindani wa kibiashara haya mambo yaskudai eti Huawei inatumia vifaa vyao vya mawasiliano kupeleleza Serikali sijui za Amerika na Ulaya - huo ni ulaghai mtupu unao tumiwa na USA kuleta taharuki Duniani ie ni usanii, mwaka juzi Wachina waliwapatia Wajerumani source code inayo tumika kuendesha 5G systems za Huawei, wana sayansi wa Kijerumani walisema source code za Huawei hazina an embedded program yoyote yenye lengo la kufanya ujasusi hata Uingereza ili draw same conclusion, wakina Trump na Pompeo walipokuwa confronted na ushahidi huo, wakaishia kusemaa" Well, you cannot trust Chinese Communist Party! " badala ya kuzungumza masuala ya teknolojia na biashara wanakimbilia kulahumu chama cha kikomunist cha Uchina, lengo kama nilivyo sema tangu mwanzo ni kutaka kuharibu biashara za teknolojia ya mawasiliano ya kampuni ya Huawei - USA inaona hisiwe tabu ngoja wote tukose - ndio walivyo roho mbaya na wivu wa kike.

One more thing, hii dhana iliyo jengeka kwamba: eti Uchina haina uwezo wa kuunda semiconductors zao specifically Microprocessors na Chipsets - habari hizi zina ukweli gani? Nani kawambieni Vyuo vikuu vya Uchina na Vyuo vya ufundi hawafundishi solid state physics - nani? Nani kawambieni wachina hawana viwanda vya ku-fabricate mpaka nanometer yechnology size semicondoctors - hivi sasa Taifa lao ndio linaongoza Duniani kwa kuunda fastest super computers au nyie hilo hamlijui? Super computers za Uchina zinatumia microprocessor zilizo zakishwa uchina,Memories and other steering logics zinazo tumika kwenye super computers, hawakutumia component hata moja kutoka USA, Taiwan au Korea ie hakuna Intel, AMD au Motorola microprocessor iliyo tumika - what does that tell you?

Uchina/Huawei ku-source some mission critical semiconductors kutoka silcone Valley hakuimanisha kwamba Wachina hawana uwezo wa kujenga viwanda vya ku-mould na kufabricate semiconductors, wachina uwezo huo wanao sana we sema wakiwachia Wamerica wawauzie semiconductors ili waendeleze mahusiano mazuri ya biashara baina ya Uchina na USA, Trump na mpambe wake Pompeo na akili zao fyatu waka-turn everything up side down inside out, vita yote hii USA imefahidika nini mbona tena Makampuni ya kuzalisha semiconductors wanakwenda kubembeleza Serikali yao ilirudishe mahusiano mazuri na Uchina ili kununua semiconductors zilizo rundikana kwenye maghara yao,wafanya kazi wengi wamehachishwa kazi na wengine kuendelea kulipwa nusu mshahara - uwezi kuchezea Taifa linalo nunua almost 95% ya bidhaa zako za semiconductors ukawa salama kibiashara - kutoana mbali kwa USA Administration kumeanza kuwa cost dearly.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…