Huawei yageukia kwenye ufugaji wa nguruwe kutokana na kushuka kwa mauzo ya smartphone

You said it all kupotez biashara ya 5b us dollar si lelemama ,tuone sasa hizo simicondut Kama watazipika wale na chai
.kimsingi trump kavuruga baadhi ya makampini ya USA kwa ujuaji
 
Hii habari inapatikana hata katika Chinese media outlets, sio BBC pekee. By the way, nimeweka vyanzo viwili vya taarifa ambapo unaweza kuchagua kimojawapo.

Semiconductor industry ni miongoni mwa sekta ngumu kama si ngumu zaidi kuliko sekta zote hasa katika uendeshaji wake, maana inahitaji sana ujuzi, tena wa hali ya juu sana katika masuala husika kuliko wengi wanavyofikiri. Si suala la kuwa na fedha tu. Industry ya semiconductors ya China bado ni ndogo sana ukilinganisha na nchi za magharibi kama Marekani pamoja na kwamba China ni soko kubwa la semiconductors. Sababu kubwa ni kutokana na upungufu wa wataalamu ambao wamebobea katika industry kwa muda mrefu. Elimu na mafunzo yao ya ndani pekee havitoshi kuijenga sekta.

Vyuo vya elimu vya China kufundisha masuala haya si suluhisho. China ina vyuo vizuri tu vya kiufundi lakini wataalamu katika ufundishaji, wakufunzi na maprofesa wa semiconductors waliobobea kwenye industry kwa muda mrefu wamejazana katika vyuo vya nchi za magharibi kama vile Marekani ambako ndiko kwenye sekta imara. Wanaohitimu vyuo wanaingia moja kwa moja kwenye kampuni kubwa kama Intel, Qualcomm, Texas Instruments na nyingine. Wengine wanaotoka hapo wanaelekea zaidi kwenye mataifa ya Korea Kusini, Taiwan n.k. Mataifa ambayo yanashabihiana kimaadili na Marekani. Kuzalisha wataalamu kama computer engineers ama scientists ni japo jepesi kwa China lakini linapokuja suala la kuzalisha wahandisi wa semiconductors wenye ujuzi unaohitajika katika industry, it's a different story.

Kitu kimojawapo ambacho China imekuwa ikifaidika nacho kupitia semiconductor industry ya Marekani ni katika kuwavutia kwa kuwapa incentives wahitimu wa mafunzo ya juu kutoka katika hivyo vyuo vya Marekani, ambao ni raia wa China, ili walio wengi warudi nchini China baada ya kupata ujuzi. Hili ni mojawapo ya factors kubwa ambazo zimekuwa zikiisaidia China kukuza sekta zake nyingine pia ukiachana na semiconductors.

Process ya ku-design na manufacturing ya high-end microchips kunahitaji uwekezaji na utafiti wa muda mrefu. Sekta ya semiconductors ya China bado ni changa sana na inategemea sana teknolojia ya kigeni. Mwaka jana pekee, kulingana na ripoti mbalimbali za kimataifa (kama umekuwa ukifuatilia), China ilizalisha microprocessor chips kwa kiwango cha asilimia takribani 16 huku kampuni za kigeni zilizowekeza nchini China hususani Samsung na TSMC zikihusika kwa kiasi kikubwa katika uzalishaji. Taarifa tofauti na hizo ambazo ni kwa mujibu wa Wachina wenyewe zinadai kuwa kiwango cha uzalishaji cha ndani kilifikia asilimia 30 pekee. Maana yake ni kwamba, bado sekta ya uzalishaji wa microprocessors nchini China ni ndogo.

Sababu nyingine ya China kuagiza zaidi semiconductors kutoka nje ni gharama za uzalishaji. Wanaamua kuwa economical kwa sababu manufacturing ya chips [from scratch] ina-cost fedha nyingi sana kwa ajili ya research, miundombinu: fabrication plants, machinery n.k. Pia, errors zozote zile zatika design & manufacturing ni hasara kubwa sana kwa kampuni hata kama ina msuli kifedha. Ili kuepukana na hasara kutokana na makosa katika uzalishaji, muda mrefu wa R&D unahitajika bila kusahau wataalamu waliobobea katika sekta kitu ambacho bado ni changamoto sana kwa China kama nilivyosema hapo awali. Kampuni kubwa kama Samsung na TSMC pamoja na uzoefu wao katika sekta wanafanyia R&D Silicon Valley (Marekani) na kwenye mataifa mengine yenye uzoefu kama Israel. Kampuni maarufu ya semiconductor ya China, HiSilicon, ilikuwa ikizalisha microchips kupitia kampuni ya TSMC ya Taiwan, hivyo ilikuwa rahisi kwao kufanya uzalishaji. Hiyo ni kabla ya vikwazo.

Jambo la mwisho; unaposema kuwa China inaongoza duniani kwa kuunda fastest supercomputers unazungumzia wakati gani? Maana katika kipindi hiki cha sasa, Japan na Marekani kupitia kampuni za Fujitsu na IBM ndio vinara katika kuunda supercomputers zenye kasi duniani kwa mujibu wa tafiti zilizopo na zinazokubalika zaidi. Pia, kuunda supercomputer hakukufanyi ukaweza kuunda competitive, high-end microchips. Hivyo ni vitu viwili tofauti.
 
Kuiba tech ni kosa kisheria, it's a matter of time kabla ya wenyewe kukushughulikia. Intellectual property za watu hizo. Kuna watu wamepigika, usiku na mchana wameumiza vichwa ili ku-innovate alafu atokee mtu fulani ale jasho lao kiwepesi hivyo!
Kweli kabisa
Hiki ndio kinachotokwa kwenye pharmaceutical company za marekani , hata hizi Arv zinazoletwa huku africa kuna watu walienda ku lobby na kina pfizer, moderna etc Ili zitoe walau formula rahisi na nafuu , kupunguza idadi ya vifo africa , makampuni hayo moja ya madai yao ni kuwa wanatumia pesa nyingi sana kufanya research za dawa , nyingi ya research hizo hazifanikiwi na wanaishiwa kupata hasara , ndo maana wakipata working formula wanaiwekea patent na wanauza dawa ghali Ili kufidia research walizopoteza pesa.

Mchina production zake nyingi zina fall kwenye kundi hilo , tech zenye patents , Usa wanajua ni wapi watambana akianza kuota mapembe , Huawei ni kampuni ya nne kutoka china ,kama sikosei kukalishwa kwa sheria za patent .
 
Kama alikuwa anajua kwamba nguruwe zinalipa kwanini alikuwa anatengeneza smart phone
Just priority mkuu,
Unaweza kuwa na rundo la mambo ya kufanya but ni lazima uangalie kwa mapana jambo lipi lianze kwa sababu gani...
 
Sasa Kama wanamanufscyure 14nm from scratch ni swala la mda tu kufika hizi 7nm ..5nm .haiwezi kuwa ngumu Kama ulivyoelezea hapa mkuu .
 
Sasa Kama wanamanufscyure 14nm from scratch ni swala la mda tu kufika hizi 7nm ..5nm .haiwezi kuwa ngumu Kama ulivyoelezea hapa mkuu .
Wana-manufacture 14nm from scratch? Seriously?!

SMIC ndio kampuni kubwa zaidi ya semiconductor manufacturing ya Kichina. Hawa mpaka sasa wanatoa 14nm process node ambayo ndio 'most advanced' kwao wakati wenzao kama Samsung na TSMC wamekwisha fikia mpaka 5nm. Isitoshe, baadhi ya equipments ambazo SMIC imekuwa ikitumia katika uzalishaji wa hizo microchip ni teknolojia ya Kimarekani.

Huawei ilikuwa ikitumia microchips zinazozalishwa na kampuni ya Taiwan TSMC kabla ya kupigwa ban na walifikia mpaka kwenye 5nm process node katika chip zao (HiSilicon Kirin 9000). Baada ya kuwekewa zuio, Huawei ikahamia SMIC kwa ajili ya kupata microchips ili kwa kiasi fulani kukabiliana na vikwazo. Kilichotokea, SMIC nayo ikapewa zuio na Trump kutumia teknolojia ya Marekani hivi karibuni tu wakati anakaribia kuondoka madarakani.

Hilo suala la muda nimekwisha lizungumzia kwenye bandiko lililopita. Process ya uzalishaji "from scratch" kama unavyosema inahitaji muda mrefu. Isitoshe, si muda tu bali zaidi katika ujuzi wa kutosha. Unaposema "haiwezi kuwa ngumu" ni katika levels za kina Intel, Samsung na TSMC, ila kiuhalisia bado ni process ngumu kwa viwango vya SMIC. Pamoja na hayo, kupitia uwekezaji wa kutosha wanaweza kufikia hizo 7nm lakini wakati wanajipanga kufika hapo, hivi sasa kina Intel, Samsung na TSMC wako katika mchakato wa kuja na 3nm process node.
 
Usihofu mkuu kutangulia sio kufika .TSMC wao itakuwa maana wanapoteza soko kubwa Kama la Huawei. Au wataanza ufugaji wa sungura Kama option B .maana kitu kinachosumbua makampini mengi ni soko la uhakika kwa bidhaa unazozalisah au watafunga factory kabisa na kupunguza wafanyakazi
 
Ni kweli kwamba Huawei ilikuwa miongoni mwa wateja wakubwa wa TSMC. Lakini, ilibidi TSMC kuacha kufanya kazi na Huawei kutokana na vikwazo la sivyo, huenda nao wangepigwa ban kutumia teknolojia ya Marekani kama ilivyotokea kwa SMIC. Madhara yangekuwa makubwa zaidi kwao.

Hata hivyo hawajaathirika sana maana bado wana clients wakubwa kwenye industry. Apple ndiye mteja wao mkubwa zaidi kuliko wote, pia kuna wengine kama Qualcomm, MediaTek pamoja na AMD. Isitoshe, hivi karibuni wametangaza kuongeza wafanyakazi kutokana na kuongezeka kwa oda za 5nm microchips. Hili litapelekea kujazwa kwa nafsi iliyoachwa wazi na Huawei.
 
Sio glass za gorilla tu mkuu hadi hizo chip zao za kichina za MTK hawazipi kipaumbele kabisa na wametumia kwenye cm chache sana.
Msingi wa technologia walionao marekani na Western countries ni imara sana, ndo maana ili uwashinde kwenye ubunifu ni ngumu sana, sababu njia unazofikiria kuzipitia wao walishazipita kitambo sana
 
Msingi wa technologia walionao marekani na Western countries ni imara sana, ndo maana ili uwashinde kwenye ubunifu ni ngumu sana, sababu njia unazofikiria kuzipitia wao walishazipita kitambo sana
Sio maeneo yote US,yupo viziru kuna maeneo mengine wenyewe wanasubiri.
 
Kitu ambacho Hawakuelewi ni kwamba unatakiwa uwe unique na kuzalisha kitu Bora Zaid ya mwenzako, makampuni mengi ya kichina yamejengwa kwenye msingi wa kuvopy na kupaste technologia ndo maana inawawia vigumu sana na marekani ndo anatumia weakness

Alafu kitu ambacho watu hawajui ni kwamba marekani Wana technologia kubwa kupita maelezo hata mchina mwenyewe analijua Hilo

Na sio tu chipsets, hata engine za gari bado ajazimaster vizuri Kama Western countries company mfano wa Benz, au Volkswagen
 
Wakiwa ready waje africa fufanye nao contract farning....soko kubwa africa na kwao pia
 
Mchina hana lolote wizi laghai na muuaji wa africa yani nashangaa hawa viongozi kutaka makampuni ya wachina tutaumia sana
 
Tunapoambiwa kuwa mgogoro ujao wa kazi sio mazingira duni ya kazi au maslahi madogo bali ni kutokuwepo kabisa kwa kazi. AI devices ndio zinatumika kumchunguza mfugo kila wakati na kutoa taarifa kwa mfugaji taarifa hizi zinaunganishwa kwa madaktari na mamlaka za mifugo. Hapa inahitaji internet connectivity ya hali ya juu ili kuwezesha(internet of things), 5G. Taafsiri yake, data za mifugo Huawei atakuwa ndio mmliki. Wauza madawa ya mifugo watanunua data kwake. Data ndio utajiri. Ndio uone Ren zhenfen ni strategist wa namna gani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…